Skip to content
Coat of arms of Tanzania

National Institute for Medical Research (NIMR)

Advancing Health Research, Enhancing Life

NIMR

Wizara ya Afya leo tarehe 26/09/2025 imezindua Baraza jipya la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), hatua muhimu inayolenga kuimarisha utafiti wa kisayansi, kukuza ubunifu na kuhakikisha mafanikio ya Taasisi kwa ustawi wa watanzania.
Akizindua Baraza hilo katika ofisi ndogo za NIMR Jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe ambaye alimwakilisha Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama, amesisitiza umuhimu wa Baraza kutoa ushauri wa kitaalamu, kusimamia utendaji wa NIMR, na kuhakikisha matokeo ya tafiti yanachangia kuboresha huduma za afya nchini.
Aidha Dkt. Shekalaghe amesisitiza kuwa ushirikiano baina ya Baraza, Menejimenti na Wizara ya Afya ni muhimu ili kuimarisha tafiti za afya na kuhakikisha matokeo yanatumiwa ipasavyo katika kutatua changamoto za kiafya za wananchi.
Akimkaribisha Katibu Mkuu kuzindua Baraza, Mwenyekiti wa Baraza jipya Prof. James Mdoe, ameahidi kuliongoza Baraza kwa weledi na uadilifu, akisisitiza kuwa litahakikisha NIMR inatoa ushauri sahihi kwa Serikali. Amesema pia Taasisi itatumia teknolojia za kisasa na fursa za Mapinduzi ya Nne ya Viwanda (Fourth Industrial Revolution) kuongeza tija katika shughuli za utafiti.
“Mheshimiwa Katibu MkuuTunapenda kukuhakikishia kuwa, tupo tayari kwa kazi. Tutaweka juhudi zaidi na maarifa katika kutoa mchango wetu wa ushauri kwa mapana zaidi ili Taasisi iendelee kufanya kazi zake kwa ubora zaidi siku hadi siku ili kufikia malengo yake kwa faida ya Watanzania”. Amesisitiza Prof. Mdoe
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, aliwasilisha mafanikio ya Taasisi kwa kipindi cha miaka mitatu (2022/23 hadi 2024/25), akibainisha kuwa NIMR imeongeza idadi ya Miradi ya Utafiti na kufikia 150, huku machapisho ya kisayansi yameongezeka hadi 220 kwa mwaka. Aidha, vijarida sera vimefika 40 kwa mwaka lengo likiwa ni kutumika na watunga sera na wafanya maamuzi ili kuboresha huduma za afya nchini.
Prof. Aboud pia alibainisha mafanikio katika ubunifu wa tiba ikiwemo ugunduzi na uendelezaji wa broadly neutralizing antibodies (bNab) katika kituo cha NIMR Mbeya kwa ajili ya tiba ya VVU na UKIMWI. Taasisi pia imeboresha utoaji wa vibali vya utafiti na kupunguza muda kutoka miezi mitatu hadi ndani ya mwezi mmoja, kukarabati majengo chakavu ya vituo vya Gonja (Same), Amani Hill (Muheza), Ngongongare (Arusha) na Tabora, kukamilisha kusimika mitambo ya uzalishaji katika kituo cha tiba asili NIMR Mabibo, kupata ithibati ya kimataifa ya majaribio nasibu katika dawa za wadudu dhurifu (Efficacy Studies on Insecticidal Products) toka SANAS katika maabara ya NIMR Amani (Muheza), kuongezeka kwa makusanyo kutoka vyanzo vya ndani vya mapato na bajeti ya Taasisi kukua kutoka Sh. bilioni 51.5 hadi Sh. bilioni 89.7 bilioni huku ikiongeza rasilimali za ndani kwa ajili ya uendeshaji wa vituo vyake.
Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Mwenyekiti mpya wa Baraza, wajumbe wapya, Menejimenti ya NIMR pamoja na mwakilishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina. Hatua hizi inachagiza umuhimu wa kuendelea kufanya mageuzi ya Taasisi iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Bunge Na. 23 ya mwaka 1979.

Section Title

Prof. Mdoe Asisitiza Kukamilishwa kwa Ukarabati wa Kituo cha NIMR Tukuyu

Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James E. Mdoe, amesema ataendelea kushirikiana na Menejimenti ya NIMR katika kuhakikisha maeneo yaliyobaki ya...

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Henry M. Jackson Foundation (HJF) ya Marekani zimejadili namna ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, ikiwa ni pamoja na kufanya...

NIMR to Lead Ethical Oversight in a Multicountry Trial Exploring New Approaches to Prevent Childhood Diarrhoeal Diseases.

The National Institute for Medical Research (NIMR) is leading ethical oversight in a new multicountry clinical trial investigating whether probiotics can enhance the protection provided by rotavirus...

NIMR TABORA RESEARCH CENTRE A CENTURY OF SCIENCE: A NEW ERA OF PUBLIC HEALTH IMPACT

From a Sleeping Sickness Unit to a Modern Public Health Research Hub For more than a century, NIMR Tabora has connected scientific discovery with practical public health action. Established in Tabora...

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Henry M. Jackson Foundation (HJF) ya Marekani zimejadili namna ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, ikiwa ni pamoja na kufanya...

NIMR and HJF Strengthen Health Research Collaboration

The National Institute for Medical Research (NIMR) and the U.S.-based Henry M. Jackson Foundation (HJF) have discussed strategies to strengthen the existing collaboration in health research including...

NIMR and Museen Stade Strengthen Strategic Partnership to Advance Research, Heritage and Tourism at Amani Hill

The National Institute for Medical Research (NIMR) and Museen Stade of Germany have formalized their partnership through the signing of a collaboration agreement under the WAYS – Towards Fair and...

NIMR Mbeya Yawafikia Wakulima, Kuimarisha Ushirikishwaji wa Jamii katika Utafiti wa Afya.

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Kituo cha Mbeya, imetumia Maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nanenane) Kanda ya Kusini kuwafikia wananchi moja kwa moja, hususan wakulima...

Today is your last opportunity to submit your abstract for the 5th Traditional Medicine Scientific Conference.

Today is your last opportunity to submit your abstract for the 5th Traditional Medicine Scientific Conference.Share your research, engage with experts, and contribute to advancing evidence-based...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Dira 2050