NIMR

Uncategorized

Waziri Mchengerwa Aipongeza NIMR kwa Tafiti Zinazoimarisha Huduma za Afya na Kuchochea Maendeleo ya Taifa

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa mchango wake mkubwa katika kufanya tafiti na ubunifu unaoendelea kuboresha matibabu, kupunguza gharama za huduma za afya na kuimarisha mifumo ya afya nchini.Akifungua rasmi Kongamano la Kisayansi la 33 la NIMR lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Mhe. Mchengerwa aliyemwakilishi Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alisema Serikali inatambua mchango wa taasisi hiyo katika kusaidia kutambua, kutathmini na kuimarisha afua mbalimbali za kupambana na magonjwa huku matokeo ya tafiti yakiendelea kuwa nyenzo muhimu katika kuboresha sera na huduma za afya kwa wananchi. Aidha, Mhe. Mchengerwa alisisitiza kuwa uwekezaji katika utafiti si anasa bali ni mkakati wa maendeleo ya taifa unaosaidia kujenga uwezo wa kutatua changamoto kwa ushahidi na ubunifu wa kisayansi, huku ukichochea maendeleo ya sekta mbalimbali na ukuaji wa uchumi.Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Modest Mkude, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, alisema kongamano hilo limefanyika wakati muafaka ambapo Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutekeleza sera ya Bima ya Afya kwa Wote, hatua inayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha..Naye Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Prof. James Mdoe, alisema kwa zaidi ya miaka 40 taasisi hiyo imeendelea kufanya tafiti zenye mchango mkubwa katika kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza, afya ya mama na mtoto, lishe, afya ya jamii na maeneo mengine ya kipaumbele.“Baraza la NIMR linaendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Afya katika kuhakikisha kuwa matokeo ya tafiti yanatumika kikamilifu katika kuboresha sera, mipango na utoaji wa huduma za afya nchini,” alisema Prof. Mdoe.Akitoa taarifa ya taasisi, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, alisema kongamano la mwaka huu limekusanya watafiti, wataalamu wa afya, watunga sera na washirika wa maendeleo kujadili nafasi ya ushahidi wa kisayansi katika kuimarisha mifumo ya afya na kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Prof. Aboud alisema NIMR imeendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta ya afya kupitia tafiti zilizosaidia maboresho ya sera, huduma za matibabu, kinga dhidi ya magonjwa na matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa tafiti za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Waziri Mchengerwa Aipongeza NIMR kwa Tafiti Zinazoimarisha Huduma za Afya na Kuchochea Maendeleo ya Taifa Read More »

Mchengerwa Aitaka NIMR Kuharakisha Ugeuzaji wa Tafiti Kuwa Uchumi Halisi

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa fedha kwa kuendesha zoezi la kuandaa hesabu za miezi tisa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua inayolenga kuhakikisha uwajibikaji, usahihi wa taarifa za kifedha na matumizi bora ya fedha za umma.Zoezi hilo linafanyika mjini Morogoro kuanzia tarehe 18 hadi 30 Mei 2026, likiwakutanisha wataalamu kutoka Idara ya Fedha na Uhasibu wa vituo vyote vya NIMR kwa ajili ya kupitia, kuhakiki na kuandaa taarifa za kifedha zitakazowezesha taasisi kuwa na mifumo madhubuti ya usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha.Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amewapongeza wahasibu na wataalamu wa fedha kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuhakikisha taasisi inaendelea kuwa mfano wa uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za umma.Amesisitiza umuhimu wa kuandaa taarifa za fedha kwa umakini, weledi, usahihi na kwa wakati ili kuimarisha uwazi wa kifedha pamoja na kuhakikisha hoja za wakaguzi zinapatiwa ufumbuzi mapema na kwa ufanisi.Prof. Aboud pia ametoa shukrani kwa wataalamu wa mifumo kutoka Wizara ya Fedha kwa kuendelea kutoa usimamizi shirikishi pamoja na mchango wao katika kuboresha Mfumo wa Uhasibu wa Serikali wa MUSE, hatua inayochochea ufanisi, kasi na ubora wa upatikanaji wa taarifa za fedha Serikalini.Wataalamu wa fedha na uhasibu wa NIMR wamesema maboresho ya Mfumo wa MUSE yatawezesha upatikanaji wa taarifa za fedha kwa haraka, kwa usahihi na kwa ufanisi zaidi, hatua itakayoimarisha usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma pamoja na kusaidia utekelezaji wenye tija wa shughuli za utafiti na huduma za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Mchengerwa Aitaka NIMR Kuharakisha Ugeuzaji wa Tafiti Kuwa Uchumi Halisi Read More »

NIMR YAONGEZA KASI YA UWAJIBIKAJI KUPITIA UANDAAJI WA HESABU ZA MIEZI TISA KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa fedha kwa kuendesha zoezi la kuandaa hesabu za miezi tisa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua inayolenga kuhakikisha uwajibikaji, usahihi wa taarifa za kifedha na matumizi bora ya fedha za umma.Zoezi hilo linafanyika mjini Morogoro kuanzia tarehe 18 hadi 30 Mei 2026, likiwakutanisha wataalamu kutoka Idara ya Fedha na Uhasibu wa vituo vyote vya NIMR kwa ajili ya kupitia, kuhakiki na kuandaa taarifa za kifedha zitakazowezesha taasisi kuwa na mifumo madhubuti ya usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha.Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amewapongeza wahasibu na wataalamu wa fedha kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuhakikisha taasisi inaendelea kuwa mfano wa uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za umma.Amesisitiza umuhimu wa kuandaa taarifa za fedha kwa umakini, weledi, usahihi na kwa wakati ili kuimarisha uwazi wa kifedha pamoja na kuhakikisha hoja za wakaguzi zinapatiwa ufumbuzi mapema na kwa ufanisi.Prof. Aboud pia ametoa shukrani kwa wataalamu wa mifumo kutoka Wizara ya Fedha kwa kuendelea kutoa usimamizi shirikishi pamoja na mchango wao katika kuboresha Mfumo wa Uhasibu wa Serikali wa MUSE, hatua inayochochea ufanisi, kasi na ubora wa upatikanaji wa taarifa za fedha Serikalini.Wataalamu wa fedha na uhasibu wa NIMR wamesema maboresho ya Mfumo wa MUSE yatawezesha upatikanaji wa taarifa za fedha kwa haraka, kwa usahihi na kwa ufanisi zaidi, hatua itakayoimarisha usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma pamoja na kusaidia utekelezaji wenye tija wa shughuli za utafiti na huduma za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR YAONGEZA KASI YA UWAJIBIKAJI KUPITIA UANDAAJI WA HESABU ZA MIEZI TISA KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. Read More »

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha Makatibu Muhtasi na Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA), uliofanyika katika Ukumbi wa Ngurdoto, mkoani Arusha, kuanzia tarehe 18 hadi 23 Mei, 2026.Mkutano huo uliwakutanisha makatibu muhtasi na waandishi waendesha ofisi kutoka taasisi mbalimbali nchini kwa lengo la kujadili mabadiliko ya kiteknolojia, maendeleo ya kitaaluma pamoja na kuimarisha maadili, uwajibikaji na ufanisi katika utendaji kazi.Katika mkutano huo, NIMR iliwakilishwa na makatibu muhtasi wanane kutoka Makao Makuu na katika vituo vyake nchini ambao ni Rukia Mbwana (Makao Makuu Dodoma), Dalin Chimbonaga (Mabibo), Charity Msangi (Tanga), Sikuzani Masaka (Tabora), Jacquline Mtambi (Makao Makuu Dodoma), Asia Mwanaupanga (Mbeya), Tabitha Temhanga (Dodoma) na Laika Tibishubwamu (Mwanza).Ushiriki wa watumishi hao unaakisi dhamira ya dhati ya ya taasisi katika kuwajengea uwezo watumishi wake ili kuongeza tija, weledi na ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi.Mgeni rasmi kwenye mkutano huo alikuwa Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye alisisitiza umuhimu wa ubunifu, uwajibikaji, uadilifu na ufanisi kama msingi wa maendeleo endelevu katika maeneo ya kazi.Kaulimbiu ya mkutano huo ni: “Ubunifu, Uwajibikaji, Uadilifu na Ufanisi ni Mojawapo ya Misingi Imara ya Maendeleo Endelevu Kwenye Utendaji Kazi.”Kupitia ushiriki huo, watumishi wa NIMR wanapata fursa ya kujifunza mbinu mpya za utendaji kazi, kubadilishana uzoefu wa kitaaluma pamoja na kujengewa uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya kiteknolojia katika mazingira ya kisasa ya kazi.Ushiriki wa NIMR katika mkutano huo unaendelea kudhihirisha maono ya taasisi ya kuimarisha utendaji kazi kwa kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu, weledi na utoaji wa huduma bora kwa jamii. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma Read More »

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji wa shughuli za utafiti unafanyika kwa tija.Kikao kazi cha maandalizi ya mpango huo kilianza tarehe 18 Mei 2026 kikihusisha wataalamu wa manunuzi, wateknolojia wa maabara, wahasibu, watafiti na wataalamu wa mipango, ufuatiliaji na tathmini wakiwakilisha vituo, vitengo na kurugenzi tatu za taasisii kwa lengo la kuandaa mpango wenye uhalisia unaoendana na bajeti na mahitaji katika utekelezaji wa kazi za utafiti.Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya kikao hicho, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amesisitiza umuhimu wa kuandaa mpango wa manunuzi kwa umakini mkubwa na kuzingatia uwezo halisi wa kifedha ili kuepusha changamoto za mpango kutotekelezeka kwa kiwango kilichokusudiwa.Ameelekeza maafisa manunuzi na ugavi kujiridhisha na mpango na bajeti za kila kitengo kabla ya kuingiza taarifa kwenye mfumo wa NeST, hatua ambayo amesema itasaidia kuongeza uwiano kati ya mpango na rasilimali fedha zilizopo.Mpango huo unatarajiwa kuwezesha upatikanaji wa bidhaa na huduma muhimu kwa wakati, huku ukizingatia sheria, taratibu, kanuni na mahitaji halisi ya utekelezaji wa shughuli za taasisi hiyo katika mwaka wa fedha 2026/27.Wizara ya Afya Tanzania imeendelea kusimamia na kuhimiza matumizi bora ya rasilimali za umma katika taasisi zake kwa lengo la kuboresha huduma za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija Read More »

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua iliyowezesha wengi kutambua hali zao za kiafya na kupata elimu ya kujikinga na magonjwa.Maadhimisho ya kitaifa ya Mei Mosi mwaka 2026 yamefanyika mkoani Njombe yakiongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sanjari na maadhimisho hayo, vituo vya NIMR nchini vilishiriki kwa kutekeleza shughuli za kijamii, hususan utoaji wa huduma za afya bure kwa wananchi.Huduma zilizotolewa ni pamoja na vipimo vya malaria kwa kutumia mRDT, sukari kwenye damu, shinikizo la damu, pamoja na vipimo vya uzito na urefu. Wananchi pia walipatiwa elimu ya afya kuhusu magonjwa mbalimbali, hasa malaria, ili kuwajengea uwezo wa kujikinga na kutambua dalili mapema.Katika vituo mbalimbali ikiwemo Tanga, Amani, Mwanza na Mbeya, wananchi walijitokeza kwa wingi kupatiwa huduma hizo. Katika viwanja vya Mkwakwani mkoani Tanga, baadhi ya wananchi walieleza kufurahishwa na huduma hizo, wakisema zimewasaidia kufahamu hali zao za kiafya na kuchukua hatua mapema.“Huduma hizi zimetusaidia sana. Wengi wetu hatupati nafasi ya kupima afya mara kwa mara, lakini leo tumepata fursa ya kujua hali zetu,” alisema mmoja wa wananchi aliyepata huduma hizo.Sanjari na utoaji wa huduma, watafiti kutoka vituo vya NIMR walitoa elimu na kuonesha shughuli mbalimbali za utafiti zinazotekelezwa na taasisi hiyo, ikiwemo tafiti kuhusu mbu na ugonjwa wa malaria. Lengo likiwa ni kuongeza uelewa wa jamii kuhusu mchango wa tafiti katika kuboresha afya na kudhibiti magonjwa.Aidha, wafanyakazi hodari wa NIMR kwa mwaka 2026 walitambuliwa katika maadhimisho ya kitaifa kwa kupatiwa vyeti na zawadi, ikiwa ni kuthamini mchango wao katika maendeleo ya taasisi na sekta ya afya nchini.Maadhimisho ya Mei Mosi mwaka huu yamebeba kaulimbiu isemayo: “Kazi Zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu Katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.” Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo Read More »

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 30th April 2026, officially launched a new project aimed at strengthening Tanzania’s capacity to predict and respond to Mpox outbreak using evidence-based scientific approaches.Speaking during the inception meeting, the Director of Emergency Preparedness and Response at the Ministry of Health, Dr. Erasto Sylvanus, said the project comes at a critical time as the country continues to enhance its preparedness for public health emergencies. He emphasized that the initiative will support a shift from reactive response to proactive planning through the use of epidemic modelling and risk mapping.He further noted that the project outputs will guide decision making, improve resource allocation, and strengthen the overall effectiveness of outbreak response.The project’s Principal Investigator from NIMR, Dr. Angelina M. Lutambi, highlighted that the initiative will also focus on building local capacity in epidemic modelling and geospatial analysis, enabling Tanzanian experts to independently manage future public health threats.Adding to these efforts, the Programme Lead for Thanzi at ECSA-HC, Mr. Edward Kataika, emphasized the importance of modelling in strengthening health systems. He noted that ECSA Health Community promotes the use of modelling as a key approach to generating evidence for decision-making. According to him, modelling will complement other tools and approaches such as economic evaluation to inform better allocation of limited resources within health systems.A key highlight of the meeting was a presentation by Mr. Emmanuel Mnjowe, a software developer representing ECSA-HC, on the Thanzi Model, a newly developed predictive tool designed to support outbreak forecasting and response planning. The model is expected to play a significant role in strengthening data-driven decision-making in managing Mpox and other public health threats.Implemented in collaboration with key partners including the Ministry of Health, the Prime Minister’s Office – Regional Administration and Local Government (PO-RALG), the East, Central and Southern Africa Health Community (ECSA-HC), the Centers for Disease Control and Prevention (CDC), and the National Bureau of Statistics (NBS), the project is expected to generate critical insights that will enhance timely and effective interventions.The launch of this project marks a significant step forward in strengthening Tanzania’s preparedness and response to emerging and re-emerging infectious diseases.

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania Read More »

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti mbalimbali za afya, kama ishara ya kuthamini mchango wao katika maendeleo ya utafiti wa afya nchini.Kliniki zilizopokea mashuka hayo ni za utafiti wa kifua kikuu, VVU/UKIMWI pamoja na kisukari inayodhaminiwa na mradi wa PROTID. Mashuka hayo yalikabidhiwa tarehe 18 Aprili, 2026 kwa uongozi wa NIMR Mbeya kwa ajili ya kuwafikishia washiriki wanaohudumiwa kupitia kliniki hizo.Hatua hiyo inalenga kuonyesha kutambua na kuthamini ushiriki wa wananchi ambao wamekuwa nguzo muhimu katika kufanikisha tafiti za kisayansi zinazolenga kuboresha afya ya jamii.Akizungumza wakati wa kupokea zawadi hizo, Meneja wa Kituo cha NIMR Mbeya, Dkt. Bariki Mtafya, amesema mafanikio ya tafiti nyingi za afya hutegemea ushiriki wa wananchi, hivyo ni muhimu kuendelea kuthamini mchango wao.“Washiriki wa tafiti ni sehemu muhimu ya maendeleo ya sayansi ya afya. Hatua hii inaonesha kuthamini mchango wao na kuimarisha uhusiano kati ya watafiti na jamii,” amesema Dkt. Mtafya.Dkt. Mtafya pia amewapongeza wanawake wa NIMR Mbeya kwa moyo wa kujitolea, mshikamano na ushirikiano wao, akisema wameendelea kuwa chachu ya maendeleo ndani ya taasisi kupitia shughuli mbalimbali zinazounga mkono utafiti.Ameongeza kuwa wanawake wana nafasi muhimu katika kuendeleza sayansi na teknolojia, si tu kama watafiti bali pia kama viongozi na wabunifu wanaochangia mabadiliko chanya katika jamii.Aidha, amesema uongozi wa kituo utaendelea kuunga mkono juhudi za wanawake hao ili waendelee kutekeleza malengo yao ya kuimarisha shughuli za utafiti na ustawi wa jamii.Tukio hilo linaendelea kudhihirisha umuhimu wa ushirikiano kati ya watafiti na jamii katika kuhakikisha tafiti za afya zinafanikiwa na matokeo yake yanawanufaisha Watanzania wa sasa na vizazi vijavyo. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki Read More »