Skip to content
Coat of arms of Tanzania

National Institute for Medical Research (NIMR)

Advancing Health Research, Enhancing Life

NIMR

Uncategorized

NIMR kupitia PEN-Plus Yafikisha Huduma za Magonjwa Yasiyoambukiza Karibu na Wananchi

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kupitia mradi wa utafiti wa PENPLUS imeendelea kuboresha utoaji wa huduma za magonjwa yasiyoambukiza nchini kwa kuwezesha Hospitali za Kondoa Mji na ya Kilutheri Karatu kutoa huduma za kibingwa ambazo awali zilipatikana katika hospitali za mikoa na rufaa pekee.Mafanikio hayo yamebainishwa wakati wa Kongamano la Tatu la Kimataifa la Kimkakati wa Kikanda la PEN-Plus la Kukabiliana na Magonjwa Yasiyoambukiza Barani Afrika (3rd ICPPA 2026) linaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Dar es Salaam, tarehe 23 hadi 25 Juni 2026.Akifungua Kongamano hilo, Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema mkakati wa PEN-Plus umeendelea kuwa suluhisho muhimu barani Afrika katika kuimarisha huduma za magonjwa yasiyoambukiza kwa kuyasogeza karibu na wananchi, hususan katika hospitali za wilaya na vituo vya afya vilivyochaguliwa.Amesema kupitia ushirikiano kati ya Serikali, Washirika wa Maendeleo na Mpango wa Samia Suluhu Hassan Outreach, huduma za PEN-Plus zinaendelea kupanuliwa nchini kote, hasa katika maeneo ya vijijini na yenye changamoto ya upatikanaji wa huduma za afya.Akitoa maelezo kwa Waziri wa Afya alipotembelea banda la NIMR, Mtafiti Kiongozi wa Mradi wa PEN-Plus nchini Tanzania, Dkt. Mary Mayige, alisema mradi huo wa utafiti umewezesha hospitali za Kondoa Mji na ya Kilutheri Karatu kutoa huduma za kibingwa za magonjwa yasiyoambukiza kwa kuwajengea uwezo wataalamu wa afya, kuboresha miundombinu ya vituo vya kutolea huduma, pamoja na kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya kisasa.Katika Kongamano hilo, NIMR inaendelea kutoa huduma za uchunguzi na ushauri wa afya kwa washiriki ikiwemo upimaji wa shinikizo la juu la damu, kisukari pamoja na vipimo vya urefu na uzito kwa lengo la kuhamasisha kinga na udhibiti wa magonjwa yasiyoambukiza.Aidha, timu ya mradi iliambatana na baadhi ya wanufaika wa kliniki za magonjwa yasiyoambukiza zinazotekelezwa kupitia PEN-Plus katika vituo mbalimbali vya afya nchini, ambapo walipata fursa ya kuelezea uzoefu wao kuhusu namna huduma hizo zilivyoboreshwa na kurahisisha upatikanaji wa matibabu katika maeneo yao.Ushiriki wa NIMR katika ICPPA 2026 unaonesha mchango wa taasisi katika kuimarisha huduma za magonjwa yasiyoambukiza kupitia tafiti, ushahidi wa kisayansi na utekelezaji wa mifumo bunifu ya utoaji huduma za afya inayolenga kuwafikia wananchi wengi zaidi, hususan walioko katika maeneo yenye uhitaji mkubwa. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR kupitia PEN-Plus Yafikisha Huduma za Magonjwa Yasiyoambukiza Karibu na Wananchi Read More »

NIMR CONTINUES TO STRENGTHEN ETHICAL AND REGULATORY FRAMEWORK FOR TRADITIONAL MEDICINE RESEARCH IN TANZANIA

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched stakeholders’ consultation on draft Traditional Medicine Research Guidelines aimed at strengthening ethical and regulatory oversight of traditional medicine research in Tanzania.The consultation held in Morogoro on 22nd June 2026, is being implemented under the Trial Regulation and Clinical Ethics Optimization (TRACE PROJECT) and brings together government institutions, regulators, universities, researchers, healthcare providers, traditional medicine practitioners, and development partners.Opening the meeting, NIMR Director General Prof. Said Aboud said the guidelines are intended to reinforce ethical conduct, scientific rigor, and participant protection while supporting the development of evidence-based traditional medicine products.He said traditional medicine remains a key source of healthcare for many Tanzanians adding that stronger research is needed to generate reliable evidence on safety, efficacy, and quality.“These guidelines go beyond regulation. They provide a foundation for a robust research ecosystem that promotes scientific excellence, ethical conduct, protection of participants, and responsible product development,” he said.Head of Research Regulation at NIMR and Tanzania TRACE Project Coordinator, Dr. Obadia Bishoge said the consultation is intended to refine the draft guidelines through stakeholder input and strengthen ethical standards in traditional medicine research.He said the framework is expected to address challenges in ethical review processes within Research Ethics Committees, while improving coordination among researchers, traditional medicine practitioners, and regulators. He added that it will also support preservation of indigenous knowledge and alignment of research with scientific and legal standards.The meeting included technical presentations and discussions that will inform finalization of the guidelines and strengthen the governance of traditional medicine research in Tanzania.NIMR reiterated its commitment to continue working with stakeholders under the TRACE Project to strengthen ethical and regulatory systems for health research, to improve public health outcomes and support national development.#MinistryofHealth#NIMR #TRACEProject #TraditionalMedicine #AdvancingHealthResearchEnhancingLife Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR CONTINUES TO STRENGTHEN ETHICAL AND REGULATORY FRAMEWORK FOR TRADITIONAL MEDICINE RESEARCH IN TANZANIA Read More »

ELEVATING CLINICAL TRIAL OVERSIGHT IN AFRICA: TRACE TRAINING IN PROGRESS IN MOROGORO

Reviewers from regulatory and research institutions are currently gathered at the EDEMA Conference Hall in Morogoro for the Clinical Trial Reviewers Training (17–19 June 2026) under the TRACE Project.Today’s session features presentations on the training objectives, delivered by Dr. Obadia Bishoge, Head of Health Research Regulation Section at NIMR and TRACE Project Coordinator. The session focuses on strengthening ethical and regulatory review processes for clinical trial protocols in Tanzania.The training focuses on strengthening ethical review in clinical research, improving risk mitigation and benefit-sharing, and addressing issues of research misconduct.Implemented by the National Institute for Medical Research (NIMR) in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), the TRACE Project continues to strengthen research integrity and regulatory systems, supporting Africa’s goal to increase participation in global clinical trials from below 2% to 10% by 2030. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

ELEVATING CLINICAL TRIAL OVERSIGHT IN AFRICA: TRACE TRAINING IN PROGRESS IN MOROGORO Read More »

Strengthening Africa’s Clinical Research Systems: NIMR Leads TRACE Training to Enhance Trial Oversight.

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa mchango wake mkubwa katika kufanya tafiti na ubunifu unaoendelea kuboresha matibabu, kupunguza gharama za huduma za afya na kuimarisha mifumo ya afya nchini.Akifungua rasmi Kongamano la Kisayansi la 33 la NIMR lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Mhe. Mchengerwa aliyemwakilishi Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alisema Serikali inatambua mchango wa taasisi hiyo katika kusaidia kutambua, kutathmini na kuimarisha afua mbalimbali za kupambana na magonjwa huku matokeo ya tafiti yakiendelea kuwa nyenzo muhimu katika kuboresha sera na huduma za afya kwa wananchi. Aidha, Mhe. Mchengerwa alisisitiza kuwa uwekezaji katika utafiti si anasa bali ni mkakati wa maendeleo ya taifa unaosaidia kujenga uwezo wa kutatua changamoto kwa ushahidi na ubunifu wa kisayansi, huku ukichochea maendeleo ya sekta mbalimbali na ukuaji wa uchumi.Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Modest Mkude, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, alisema kongamano hilo limefanyika wakati muafaka ambapo Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutekeleza sera ya Bima ya Afya kwa Wote, hatua inayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha..Naye Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Prof. James Mdoe, alisema kwa zaidi ya miaka 40 taasisi hiyo imeendelea kufanya tafiti zenye mchango mkubwa katika kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza, afya ya mama na mtoto, lishe, afya ya jamii na maeneo mengine ya kipaumbele.“Baraza la NIMR linaendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Afya katika kuhakikisha kuwa matokeo ya tafiti yanatumika kikamilifu katika kuboresha sera, mipango na utoaji wa huduma za afya nchini,” alisema Prof. Mdoe.Akitoa taarifa ya taasisi, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, alisema kongamano la mwaka huu limekusanya watafiti, wataalamu wa afya, watunga sera na washirika wa maendeleo kujadili nafasi ya ushahidi wa kisayansi katika kuimarisha mifumo ya afya na kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Prof. Aboud alisema NIMR imeendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta ya afya kupitia tafiti zilizosaidia maboresho ya sera, huduma za matibabu, kinga dhidi ya magonjwa na matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa tafiti za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Strengthening Africa’s Clinical Research Systems: NIMR Leads TRACE Training to Enhance Trial Oversight. Read More »

Waziri Mchengerwa Aipongeza NIMR kwa Tafiti Zinazoimarisha Huduma za Afya na Kuchochea Maendeleo ya Taifa

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa mchango wake mkubwa katika kufanya tafiti na ubunifu unaoendelea kuboresha matibabu, kupunguza gharama za huduma za afya na kuimarisha mifumo ya afya nchini.Akifungua rasmi Kongamano la Kisayansi la 33 la NIMR lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Mhe. Mchengerwa aliyemwakilishi Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alisema Serikali inatambua mchango wa taasisi hiyo katika kusaidia kutambua, kutathmini na kuimarisha afua mbalimbali za kupambana na magonjwa huku matokeo ya tafiti yakiendelea kuwa nyenzo muhimu katika kuboresha sera na huduma za afya kwa wananchi. Aidha, Mhe. Mchengerwa alisisitiza kuwa uwekezaji katika utafiti si anasa bali ni mkakati wa maendeleo ya taifa unaosaidia kujenga uwezo wa kutatua changamoto kwa ushahidi na ubunifu wa kisayansi, huku ukichochea maendeleo ya sekta mbalimbali na ukuaji wa uchumi.Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Modest Mkude, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, alisema kongamano hilo limefanyika wakati muafaka ambapo Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutekeleza sera ya Bima ya Afya kwa Wote, hatua inayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha..Naye Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Prof. James Mdoe, alisema kwa zaidi ya miaka 40 taasisi hiyo imeendelea kufanya tafiti zenye mchango mkubwa katika kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza, afya ya mama na mtoto, lishe, afya ya jamii na maeneo mengine ya kipaumbele.“Baraza la NIMR linaendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Afya katika kuhakikisha kuwa matokeo ya tafiti yanatumika kikamilifu katika kuboresha sera, mipango na utoaji wa huduma za afya nchini,” alisema Prof. Mdoe.Akitoa taarifa ya taasisi, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, alisema kongamano la mwaka huu limekusanya watafiti, wataalamu wa afya, watunga sera na washirika wa maendeleo kujadili nafasi ya ushahidi wa kisayansi katika kuimarisha mifumo ya afya na kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Prof. Aboud alisema NIMR imeendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta ya afya kupitia tafiti zilizosaidia maboresho ya sera, huduma za matibabu, kinga dhidi ya magonjwa na matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa tafiti za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Waziri Mchengerwa Aipongeza NIMR kwa Tafiti Zinazoimarisha Huduma za Afya na Kuchochea Maendeleo ya Taifa Read More »

Mchengerwa Aitaka NIMR Kuharakisha Ugeuzaji wa Tafiti Kuwa Uchumi Halisi

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa fedha kwa kuendesha zoezi la kuandaa hesabu za miezi tisa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua inayolenga kuhakikisha uwajibikaji, usahihi wa taarifa za kifedha na matumizi bora ya fedha za umma.Zoezi hilo linafanyika mjini Morogoro kuanzia tarehe 18 hadi 30 Mei 2026, likiwakutanisha wataalamu kutoka Idara ya Fedha na Uhasibu wa vituo vyote vya NIMR kwa ajili ya kupitia, kuhakiki na kuandaa taarifa za kifedha zitakazowezesha taasisi kuwa na mifumo madhubuti ya usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha.Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amewapongeza wahasibu na wataalamu wa fedha kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuhakikisha taasisi inaendelea kuwa mfano wa uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za umma.Amesisitiza umuhimu wa kuandaa taarifa za fedha kwa umakini, weledi, usahihi na kwa wakati ili kuimarisha uwazi wa kifedha pamoja na kuhakikisha hoja za wakaguzi zinapatiwa ufumbuzi mapema na kwa ufanisi.Prof. Aboud pia ametoa shukrani kwa wataalamu wa mifumo kutoka Wizara ya Fedha kwa kuendelea kutoa usimamizi shirikishi pamoja na mchango wao katika kuboresha Mfumo wa Uhasibu wa Serikali wa MUSE, hatua inayochochea ufanisi, kasi na ubora wa upatikanaji wa taarifa za fedha Serikalini.Wataalamu wa fedha na uhasibu wa NIMR wamesema maboresho ya Mfumo wa MUSE yatawezesha upatikanaji wa taarifa za fedha kwa haraka, kwa usahihi na kwa ufanisi zaidi, hatua itakayoimarisha usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma pamoja na kusaidia utekelezaji wenye tija wa shughuli za utafiti na huduma za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Mchengerwa Aitaka NIMR Kuharakisha Ugeuzaji wa Tafiti Kuwa Uchumi Halisi Read More »

NIMR YAONGEZA KASI YA UWAJIBIKAJI KUPITIA UANDAAJI WA HESABU ZA MIEZI TISA KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa fedha kwa kuendesha zoezi la kuandaa hesabu za miezi tisa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua inayolenga kuhakikisha uwajibikaji, usahihi wa taarifa za kifedha na matumizi bora ya fedha za umma.Zoezi hilo linafanyika mjini Morogoro kuanzia tarehe 18 hadi 30 Mei 2026, likiwakutanisha wataalamu kutoka Idara ya Fedha na Uhasibu wa vituo vyote vya NIMR kwa ajili ya kupitia, kuhakiki na kuandaa taarifa za kifedha zitakazowezesha taasisi kuwa na mifumo madhubuti ya usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha.Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amewapongeza wahasibu na wataalamu wa fedha kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuhakikisha taasisi inaendelea kuwa mfano wa uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za umma.Amesisitiza umuhimu wa kuandaa taarifa za fedha kwa umakini, weledi, usahihi na kwa wakati ili kuimarisha uwazi wa kifedha pamoja na kuhakikisha hoja za wakaguzi zinapatiwa ufumbuzi mapema na kwa ufanisi.Prof. Aboud pia ametoa shukrani kwa wataalamu wa mifumo kutoka Wizara ya Fedha kwa kuendelea kutoa usimamizi shirikishi pamoja na mchango wao katika kuboresha Mfumo wa Uhasibu wa Serikali wa MUSE, hatua inayochochea ufanisi, kasi na ubora wa upatikanaji wa taarifa za fedha Serikalini.Wataalamu wa fedha na uhasibu wa NIMR wamesema maboresho ya Mfumo wa MUSE yatawezesha upatikanaji wa taarifa za fedha kwa haraka, kwa usahihi na kwa ufanisi zaidi, hatua itakayoimarisha usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma pamoja na kusaidia utekelezaji wenye tija wa shughuli za utafiti na huduma za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR YAONGEZA KASI YA UWAJIBIKAJI KUPITIA UANDAAJI WA HESABU ZA MIEZI TISA KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026. Read More »

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha Makatibu Muhtasi na Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA), uliofanyika katika Ukumbi wa Ngurdoto, mkoani Arusha, kuanzia tarehe 18 hadi 23 Mei, 2026.Mkutano huo uliwakutanisha makatibu muhtasi na waandishi waendesha ofisi kutoka taasisi mbalimbali nchini kwa lengo la kujadili mabadiliko ya kiteknolojia, maendeleo ya kitaaluma pamoja na kuimarisha maadili, uwajibikaji na ufanisi katika utendaji kazi.Katika mkutano huo, NIMR iliwakilishwa na makatibu muhtasi wanane kutoka Makao Makuu na katika vituo vyake nchini ambao ni Rukia Mbwana (Makao Makuu Dodoma), Dalin Chimbonaga (Mabibo), Charity Msangi (Tanga), Sikuzani Masaka (Tabora), Jacquline Mtambi (Makao Makuu Dodoma), Asia Mwanaupanga (Mbeya), Tabitha Temhanga (Dodoma) na Laika Tibishubwamu (Mwanza).Ushiriki wa watumishi hao unaakisi dhamira ya dhati ya ya taasisi katika kuwajengea uwezo watumishi wake ili kuongeza tija, weledi na ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi.Mgeni rasmi kwenye mkutano huo alikuwa Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye alisisitiza umuhimu wa ubunifu, uwajibikaji, uadilifu na ufanisi kama msingi wa maendeleo endelevu katika maeneo ya kazi.Kaulimbiu ya mkutano huo ni: “Ubunifu, Uwajibikaji, Uadilifu na Ufanisi ni Mojawapo ya Misingi Imara ya Maendeleo Endelevu Kwenye Utendaji Kazi.”Kupitia ushiriki huo, watumishi wa NIMR wanapata fursa ya kujifunza mbinu mpya za utendaji kazi, kubadilishana uzoefu wa kitaaluma pamoja na kujengewa uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya kiteknolojia katika mazingira ya kisasa ya kazi.Ushiriki wa NIMR katika mkutano huo unaendelea kudhihirisha maono ya taasisi ya kuimarisha utendaji kazi kwa kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu, weledi na utoaji wa huduma bora kwa jamii. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma Read More »

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji wa shughuli za utafiti unafanyika kwa tija.Kikao kazi cha maandalizi ya mpango huo kilianza tarehe 18 Mei 2026 kikihusisha wataalamu wa manunuzi, wateknolojia wa maabara, wahasibu, watafiti na wataalamu wa mipango, ufuatiliaji na tathmini wakiwakilisha vituo, vitengo na kurugenzi tatu za taasisii kwa lengo la kuandaa mpango wenye uhalisia unaoendana na bajeti na mahitaji katika utekelezaji wa kazi za utafiti.Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya kikao hicho, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amesisitiza umuhimu wa kuandaa mpango wa manunuzi kwa umakini mkubwa na kuzingatia uwezo halisi wa kifedha ili kuepusha changamoto za mpango kutotekelezeka kwa kiwango kilichokusudiwa.Ameelekeza maafisa manunuzi na ugavi kujiridhisha na mpango na bajeti za kila kitengo kabla ya kuingiza taarifa kwenye mfumo wa NeST, hatua ambayo amesema itasaidia kuongeza uwiano kati ya mpango na rasilimali fedha zilizopo.Mpango huo unatarajiwa kuwezesha upatikanaji wa bidhaa na huduma muhimu kwa wakati, huku ukizingatia sheria, taratibu, kanuni na mahitaji halisi ya utekelezaji wa shughuli za taasisi hiyo katika mwaka wa fedha 2026/27.Wizara ya Afya Tanzania imeendelea kusimamia na kuhimiza matumizi bora ya rasilimali za umma katika taasisi zake kwa lengo la kuboresha huduma za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija Read More »

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua iliyowezesha wengi kutambua hali zao za kiafya na kupata elimu ya kujikinga na magonjwa.Maadhimisho ya kitaifa ya Mei Mosi mwaka 2026 yamefanyika mkoani Njombe yakiongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sanjari na maadhimisho hayo, vituo vya NIMR nchini vilishiriki kwa kutekeleza shughuli za kijamii, hususan utoaji wa huduma za afya bure kwa wananchi.Huduma zilizotolewa ni pamoja na vipimo vya malaria kwa kutumia mRDT, sukari kwenye damu, shinikizo la damu, pamoja na vipimo vya uzito na urefu. Wananchi pia walipatiwa elimu ya afya kuhusu magonjwa mbalimbali, hasa malaria, ili kuwajengea uwezo wa kujikinga na kutambua dalili mapema.Katika vituo mbalimbali ikiwemo Tanga, Amani, Mwanza na Mbeya, wananchi walijitokeza kwa wingi kupatiwa huduma hizo. Katika viwanja vya Mkwakwani mkoani Tanga, baadhi ya wananchi walieleza kufurahishwa na huduma hizo, wakisema zimewasaidia kufahamu hali zao za kiafya na kuchukua hatua mapema.“Huduma hizi zimetusaidia sana. Wengi wetu hatupati nafasi ya kupima afya mara kwa mara, lakini leo tumepata fursa ya kujua hali zetu,” alisema mmoja wa wananchi aliyepata huduma hizo.Sanjari na utoaji wa huduma, watafiti kutoka vituo vya NIMR walitoa elimu na kuonesha shughuli mbalimbali za utafiti zinazotekelezwa na taasisi hiyo, ikiwemo tafiti kuhusu mbu na ugonjwa wa malaria. Lengo likiwa ni kuongeza uelewa wa jamii kuhusu mchango wa tafiti katika kuboresha afya na kudhibiti magonjwa.Aidha, wafanyakazi hodari wa NIMR kwa mwaka 2026 walitambuliwa katika maadhimisho ya kitaifa kwa kupatiwa vyeti na zawadi, ikiwa ni kuthamini mchango wao katika maendeleo ya taasisi na sekta ya afya nchini.Maadhimisho ya Mei Mosi mwaka huu yamebeba kaulimbiu isemayo: “Kazi Zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu Katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.” Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo Read More »

Dira 2050