NIMR

Erick Mboma

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti mbalimbali za afya, kama ishara ya kuthamini mchango wao katika maendeleo ya utafiti wa afya nchini.Kliniki zilizopokea mashuka hayo ni za utafiti wa kifua kikuu, VVU/UKIMWI pamoja na kisukari inayodhaminiwa na mradi wa PROTID. Mashuka hayo yalikabidhiwa tarehe 18 Aprili, 2026 kwa uongozi wa NIMR Mbeya kwa ajili ya kuwafikishia washiriki wanaohudumiwa kupitia kliniki hizo.Hatua hiyo inalenga kuonyesha kutambua na kuthamini ushiriki wa wananchi ambao wamekuwa nguzo muhimu katika kufanikisha tafiti za kisayansi zinazolenga kuboresha afya ya jamii.Akizungumza wakati wa kupokea zawadi hizo, Meneja wa Kituo cha NIMR Mbeya, Dkt. Bariki Mtafya, amesema mafanikio ya tafiti nyingi za afya hutegemea ushiriki wa wananchi, hivyo ni muhimu kuendelea kuthamini mchango wao.“Washiriki wa tafiti ni sehemu muhimu ya maendeleo ya sayansi ya afya. Hatua hii inaonesha kuthamini mchango wao na kuimarisha uhusiano kati ya watafiti na jamii,” amesema Dkt. Mtafya.Dkt. Mtafya pia amewapongeza wanawake wa NIMR Mbeya kwa moyo wa kujitolea, mshikamano na ushirikiano wao, akisema wameendelea kuwa chachu ya maendeleo ndani ya taasisi kupitia shughuli mbalimbali zinazounga mkono utafiti.Ameongeza kuwa wanawake wana nafasi muhimu katika kuendeleza sayansi na teknolojia, si tu kama watafiti bali pia kama viongozi na wabunifu wanaochangia mabadiliko chanya katika jamii.Aidha, amesema uongozi wa kituo utaendelea kuunga mkono juhudi za wanawake hao ili waendelee kutekeleza malengo yao ya kuimarisha shughuli za utafiti na ustawi wa jamii.Tukio hilo linaendelea kudhihirisha umuhimu wa ushirikiano kati ya watafiti na jamii katika kuhakikisha tafiti za afya zinafanikiwa na matokeo yake yanawanufaisha Watanzania wa sasa na vizazi vijavyo. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki Read More »

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa na lengo la kujadili na kupitisha Mpango Mkakati wa Taasisi wa miaka mitano (2026–2031) pamoja na Mpango na Maoteo ya Bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027. Mpango Mkakati huo na bajeti hiyo vimeandaliwa kwa kuzingatia Mwongozo wa Maandalizi ya Bajeti, Mpango Mkakati wa NIMR, Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala ya mwaka 2025–2030, pamoja na miongozo mbalimbali iliyotolewa na Wizara ya Fedha, Sera za Kisekta na maelekezo ya Wizara ya Afya. Hatua hiyo inalenga kuimarisha uwazi na ushirikishwaji katika maamuzi ya taasisi ili kila mfanyakazi anapotekeleza majukumu yake afahamu kwa uwazi matarajio ya Mpango Mkakati. Aidha, inalenga kuhakikisha wafanyakazi wanashiriki kikamilifu katika maamuzi na utekelezaji wa malengo ya taasisi. Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Wafanyakazi ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amesema Baraza hilo ni jukwaa muhimu linalowaunganisha wafanyakazi na Menejimenti katika kujadili na kutoa ushauri kuhusu usimamizi wa kazi, rasilimali watu na mazingira bora ya kazi. Prof. Aboud amesema NIMR inaendelea na juhudi mbalimbali za kuongeza mapato ya taasisi ikiwemo mpango wa kuanzisha Kampuni Tanzu (Spin Off Company) itakayorahisisha mashirikiano na wadau na kuongeza mapato kwa taasisi na Serikali, kujenga jengo la ofisi Dodoma, kuboresha miundombinu ya kufanyia kazi, kutenga fedha za kufanya tafiti kwa ajili ya watafiti wachanga (Early Career Research Scientists) na kuboresha maslahi ya wafanyakazi. Aidha, amesema kupitia Kituo cha Mabibo, NIMR inaendelea kuzalisha dawa za tiba asili sambamba na kuendesha tafiti mbalimbali za kisayansi zinazolenga kuboresha afya za wananchi. Akitaja baadhi ya mafanikio ambayo Taasisi imeipata katika mwaka mmoja uliopita, Prof Aboud alisema Taasisi imeendelea kufanya tafiti ambazo zimetoa matokeo chanya katika kuboresha sera na huduma, kukarabati miundombinu ya vituo vyake, kununua vitendea kazi kwa ajili ya watumishi, kusimika mifumo ya TEHAMA ili kuongeza ufanisi na tija, kuhamishia Makao Makuu ya Taasisi Dodoma, kuwapatia ofisi kituo cha NIMR Muhimbili badala ya kuendelea kupanga ili kupunguza gharama za uendeshaji wa taasisi, kuzalisha dawa za tiba asili na kuchangia katika huduma jumuishi zinazotolewa katika Hospitali za Rufaa za Mkoa 14 na kuboresha maslahi ya wafanyakazi kupitia motisha. Katika hotuba yake, Prof. Aboud pia amewakumbusha wafanyakazi kuendelea kufanya kazi kwa bidii, kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, kutumia muda wa kazi ipasavyo na kutunza rasilimali za taasisi ili kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu. Mkutano Mkuu wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi umewakutanisha wajumbe kutoka vituo vyote vya NIMR pamoja na Makao Makuu, kwa lengo la kujadili kwa kina masuala mbalimbali yatakayosaidia kuimarisha utendaji wa taasisi. Mkutano huo pia ulihudhuriwa na viongozi kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Ufundi Stadi, Ushauri, Habari na Utafiti (RAAWU) akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa RAAWU Taifa, Bw. Simon Mbai pamoja na Katibu wa RAAWU Kanda ya Kati, Bi. Staile Kiko. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027 Read More »

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the challenges of Tuberculosis (TB) and diabetes mellitus (DM).This was highlighted by the Director General of NIMR in his opening remarks during the Preventive Treatment of Latent Tuberculosis Infection in People with DM (PROTID) Annual General Meeting, which brought together various local and international stakeholders.The meeting was attended by representatives from several institutions, including KCRI/KCMC through the Good Samaritan Foundation, Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS), Makerere University and Uganda Martyrs Hospital Lubaga (Uganda), Radboud University Medical Center (Netherlands), the University of Otago (New Zealand), St George’s Hospital Medical School, and King’s College London (United Kingdom) as well as NIMR.The Director General noted that the meeting was an important platform that demonstrates the strength of international collaboration in improving community health, emphasizing that the participation of stakeholders from diverse global institutions enhances the exchange of knowledge and experience.He further emphasized that the PROTID project has continued to act as a catalyst for building capacity in high-quality research as well as mentoring early-career researchers through multi-disciplinary approaches. He also noted that the research findings contribute to improving health policies and services particularly in settings where infectious diseases remain a major public health challenge.Researchers involved in the project discussed various study findings, achievements, challenges encountered, and opportunities to strengthen scientific collaboration in the fields of TB and diabetes.In addition, he encouraged institutions to further strengthen collaboration, actively engage in discussions and develop sustainable solutions to public health challenges.He also expressed appreciation to the PROTID project leadership, the organizers of the meeting, and all partners for their contribution to the success of this important event.The three-day meeting was held from 12th to 14th April 2026 at the Ummy Mwalimu Hall at the National Hospital of Muhimbili in Dar es Salaam. It brought together different groups including researchers, medical doctors, partners, and early-career researchers, with the aim of strengthening international collaboration and advancing research in TB and DM. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting Read More »

NIMR Director General Honored for Outstanding Contributions to Advancing Medical Science, Research and Capacity Building

The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof. Said S. Aboud, has been honoured with the African Excellence and Personality Award (AEPA 2026) in Medical Science, Research and Capacity Building by the African Corporate Excellence and Personality Awards (ACEPA) Events Secretariat on 10th April 2026 in Accra, Ghana. The award was in recognition of his outstanding leadership and remarkable contributions to advancing medical research, public health, and scientific innovation across Africa.The citation of the award recognizes Prof. Aboud for his exceptional leadership and unwavering dedication to strengthening medical research systems and improving public health outcomes. Through his extensive work in infection biology and clinical research, he has established himself as a globally respected authority in the field of health research.With more than two decades of experience, Prof. Aboud has led and contributed to groundbreaking research addressing major public health challenges, including HIV, malaria, tuberculosis and antimicrobial resistance. His work has significantly influenced health policy development, advancing diagnostics and strengthened research capacity both in Tanzania and internationally.In addition to his academic and scientific contributions, Prof. Aboud has demonstrated strong leadership in both national and international health institutions. His active involvement in global health initiatives including pandemic preparedness and response efforts has contributed to improving healthcare delivery systems and advancing scientific innovation across the African continent.Speaking during the award event, Prof. Aboud thanked the organizers for the recognition and urged countries to increase investment in health research, enhance uptake of impactful research findings and to inculcate a culture of research and innovation in young population that can lead to product development in diagnostics, vaccines and therapeutics in Africa. This recognition not only celebrates Prof. Aboud individual achievements but also highlights the critical role played by Tanzanian researchers in advancing science and improving public health. It further reinforces the growing reputation of NIMR as a leading institution in health research in Africa. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Director General Honored for Outstanding Contributions to Advancing Medical Science, Research and Capacity Building Read More »

NIMR Scientists Ranked Among Tanzania Top 50 by the AD Scientific Index 2026

The National Institute for Medical Research (NIMR) has once again demonstrated its leadership in scientific research with five of its distinguished scientists ranked among the Top 50 scientists in Tanzania by the AD Scientific Index 2026.This recognition highlights NIMR growing influence in advancing health research and generating evidence that informs policy and strengthens healthcare systems to reduce morbidity and mortality both nationally and globally. This also reflects the institute continued commitment to excellence, innovation and impactful research scientists.The research scientists recognized in this ranking are Prof. Sayoki Mfinanga (4th), Prof. Said Aboud (10th), Dr. Susan Rumisha (12th), Dr. William Kisinza (30th) and Dr. Bruno Mmbando (41st). The inclusion of these scientists reflects years of commitment, dedication, conduct of impactful research and significant contributions to the public health and scientific knowledge nationally and globally.Through the research work, NIMR address key health challenges in Tanzania and beyond including HIV/AIDS, tuberculosis, malaria, health data systems, zoonoses, NCDs, vector-borne diseases and others. The research conducted continues to inform policy, influence decision-making, and strengthen responses to both infectious and non-communicable diseases.The presence of five NIMR scientists in the Top 50 is not only an individual achievement but also a strong reflection of the institution role as a centre of scientific excellence and a trusted partner in global health research.NIMR congratulates the five scientists for their outstanding performance and continued commitment to enhancing lives through advancing health research. The institute also congratulates all other NIMR researchers who have appeared in the ranking of AD Scientific Index 2026. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Scientists Ranked Among Tanzania Top 50 by the AD Scientific Index 2026 Read More »

Decade-Long Research Led by NIMR Shapes Africa’s Push for Integrated HIV and NCD Care

New evidence from a decade of research led by Tanzania’s National Institute for Medical Research (NIMR) on integrated HIV and non-communicable disease (NCD) care is driving renewed efforts across Africa to reform health systems, as leaders prepare for the launch of the SPARK-NCD initiative to strengthen data and service integration.Speaking at the high-level dissemination of integrated HIV and NCD evidence, Zanzibar Second Vice President, Suleiman Hemed Abdulla, representing Dr Hussein Ali Mwinyi, President of the Zanzibar Revolutionary Government and Chairman of the Revolutionary Council, called for stronger collaboration among health experts to improve healthcare outcomes across Africa.He noted that people living with HIV are increasingly affected by non-communicable diseases such as cardiovascular conditions, diabetes, cancer and mental health disorders, underscoring the need for more coordinated care, while emphasizing the importance of research in guiding effective service delivery.He also commended the efforts of both the Government of the United Republic of Tanzania and the Zanzibar Revolutionary Government in tackling HIV and non-communicable diseases.Evidence from studies led by NIMR, including the INTE-COMM trial in Tanzania and Uganda, shows that integrated, community-based care can expand access to treatment while maintaining outcomes comparable to facility-based services.The findings further show that bringing services closer to communities reduces transport costs, waiting times and stigma, while easing pressure on health facilities and informing policy discussions across Africa on integrated HIV and NCD services.Representing the Chief Medical Officer from the Ministry of Health Tanzania, NIMR Director General Prof. Said Aboud said the initiative aims to ensure research findings translate into tangible benefits for communities.“Integrated service delivery allows patients with multiple conditions to receive care more efficiently, reducing hospital visits and healthcare costs, while also contributing to reduced deaths and the growing burden of HIV and non-communicable diseases, particularly among vulnerable populations,” he said.The SPARK-NCD initiative, led by Africa CDC, seeks to strengthen disease surveillance and support data-driven decision-making across African countries. Discussions also emphasized the need to improve NCD surveillance, integrate services, and strengthen Africa-led, data-driven health solutions.The two-day continental meeting, held from March 27–28, 2026, at the Golden Tulip Hotel in Zanzibar brought together Ministers of Health, policymakers, researchers and development partners from across Africa.With growing political commitment and locally generated evidence from institutions such as NIMR, experts say that integrating HIV and NCD services could transform healthcare systems across Africa, improving access, reducing costs and saving lives. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Decade-Long Research Led by NIMR Shapes Africa’s Push for Integrated HIV and NCD Care Read More »

Watumishi NIMR Wapatiwa Mafunzo ya Maadili ya Utumishi wa Umma, Rushwa Mahali pa Kazi na Afya ya Akili

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kujenga watumishi wenye weledi, uadilifu, uwajibikaji na afya njema kwa kuendesha mafunzo maalumu yanayolenga kuimarisha maadili ya utumishi wa umma, mapambano dhidi ya rushwa mahali pa kazi na kuhamasisha umuhimu wa afya ya akili.Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 18 Machi 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma, yakiendeshwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Taasisi ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe.Akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR Prof. Said Aboud amesema kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati ya Serikali ya kuimarisha utawala bora kupitia watumishi wa umma wanaozingatia maadili, sheria, kanuni na taratibu za kazi. Alisisitiza kuwa maadili ya utumishi wa umma ni msingi muhimu katika kujenga taasisi imara, yenye kuaminika na inayotoa huduma bora kwa wananchi.Prof. Aboud ameeleza kuwa NIMR inaongozwa na misingi mikuu mitano ya uendeshaji ambayo ni uadilifu, ujumuishwaji, ubora, uwajibikaji na uwazi, na kwamba mafunzo hayo yanalengs kuimarisha utekelezaji wa misingi hiyo katika kazi za kila siku za watumishi.Prof. Aboud amesema mafunzo hayo pia yataweka misingi ya maadili kwa watumishi wa umma na kujenga uzalendo kama njia mojawapo ya kuondoa vitendo vya rushwa mahali pa kazi.Sambamba na hilo, mtaalamu kutoka Taasisi ya Mirembe ametoa elimu kuhusu afya ya akili, akisisitiza kuwa ustawi wa akili ni nyenzo muhimu katika kuongeza tija na ufanisi kazini. Alieleza kuwa mtumishi mwenye afya njema ya akili huwa na uwezo mkubwa wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuhimili changamoto za kikazi.Aidha, menejimenti ya NIMR imeisitiza kuwa itaendelea kujenga mazingira ya kazi yanayozingatia maadili, yasiyovumilia vitendo vya rushwa na yanayojali ustawi wa watumishi wote. Mafunzo hayo ya siku moja yaliyohudhuriwa na Menejimenti na watumishi wa NIMR kutoka makao makuu Dodoma na vituo vya utafiti yanatarajiwa kuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa NIMR na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa jamii, sambamba na kuchangia juhudi za Serikali za kujenga utumishi wa umma wenye maadili na uwajibikaji. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Watumishi NIMR Wapatiwa Mafunzo ya Maadili ya Utumishi wa Umma, Rushwa Mahali pa Kazi na Afya ya Akili Read More »

NIMR Researchers Shine with DZIF Early Career Scientists Grant

Researchers from the National Institute for Medical Research (NIMR), Mbeya Centre, have earned international recognition after five early career scientists were awarded the prestigious Deutsches Zentrum für Infektionsforschung (DZiF) Early Career Scientists Grant 2026 The grant is awarded annually by the DZIF Academy through its Short-term Training Program, which aims to strengthen scientific skills, support career development, and promote collaboration between Tanzanian researchers and their German counterparts within the DZIF network.The program is co-led by Dr. Nyanda Ntinginya and Dr. Bariki Mtafya, and is designed to equip early career scientists with essential research skills through mentorship, targeted training, and opportunities for scientific collaboration.The five NIMR researchers selected for the 2026 grant are Dr Lucy Elauteri Mrema, Dr Julieth Lalashowi, Dr Daniel Mapamba, Jacklina Mhidze, and Willyhelmina Olomi. Their research addresses critical health priorities, including the intersection of non-communicable and infectious diseases, tuberculosis-related complications, HIV/TB immunology, and infectious disease modelling.Through this support, the selected researchers will benefit from enhanced training and exposure, particularly in the field of infectious diseases, contributing to the strengthening of Africa’s research capacity and nurturing the next generation of scientific leaders.This achievement marks an important milestone in reinforcing the long-standing collaboration between Tanzania and Germany in health research, while highlighting NIMR’s commitment to advancing scientific excellence and innovation. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Researchers Shine with DZIF Early Career Scientists Grant Read More »

NIMR Yasisitiza Tafiti Zinazotatua Changamoto za Afya Katika Maandalizi ya Bajeti ya 2026/2027

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said Aboud, ameitaka taasisi hiyo kuimarisha uwezo wake wa kifedha na kuwekeza katika tafiti zinazolenga kutatua changamoto za afya nchini, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi.Akizungumza wakati wa kufunga kikao kazi cha maandalizi ya mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 kilichofanyika kuanzia tarehe 2 hadi 11 Machi 2026 katika Hoteli ya Edema mjini Morogoro, Profesa Aboud alipongeza ushiriki mkubwa wa wataalamu wa bajeti kutoka kurugenzi, vitengo na vituo mbalimbali vya taasisi.“Kikao kazi hiki kimeonesha kwa vitendo dhana ya ushirikishwaji wa wadau muhimu katika mchakato wa maandalizi ya bajeti, huku kikizingatia miongozo ya serikali katika upangaji wa mipango na matumizi ya rasilimali za taasisi,” alisema.Aliwataka washiriki kuhakikisha kuwa katika kupanga bajeti wanatanguliza vipaumbele vya taasisi kwa kutenga rasilimali za kutosha katika maeneo muhimu yatakayochangia kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi.Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuiwezesha taasisi kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi. Alieleza kuwa ni wakati muafaka kwa taasisi kuangalia namna ya kufanya tafiti zinazolenga kutatua changamoto za afya nchini kupitia vyanzo vyake vya mapato ya ndani na kupunguza utegemezi.Alielekeza timu inayohusika na mipango na bajeti kuangalia uwezekano wa kutenga fedha za awali za tafiti (research seed fund) ili kuwasaidia hasa watafiti wachanga kuanzisha tafiti zitakazochangia maendeleo ya sekta ya afya nchini. Ametoa wito pia kwa taasisi kuanzisha mfuko wa fedha wa kuwezesha kufanya tafiti za afya (Research endowment fund).Vilevile, alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuboresha ustawi wa watumishi, akiiagiza timu hiyo kuangalia uwezekano wa kutekeleza kipengele cha posho ya chakula kwa watumishi kwa mujibu wa mpango wa motisha ambapo kwa sasa hulipwa nauli pekee wakati wa shughuli rasmi za kikazi.Kikao kazi hicho kiliwakutanisha maafisa bajeti kutoka vituo, kurugenzi na vitengo mbalimbali vya NIMR kwa lengo la kuandaa mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali na taasisi. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Yasisitiza Tafiti Zinazotatua Changamoto za Afya Katika Maandalizi ya Bajeti ya 2026/2027 Read More »

Mkurugenzi Mkuu NIMR Aridhishwa na Maendeleo ya Utafiti na Huduma Kituo Kidogo cha Gonja.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said S. Aboud, ameridhishwa na maendeleo ya shughuli za utafiti na utoaji wa huduma za maabara yanayoendelea katika Kituo kidogo cha NIMR Gonja kufuatia ziara yake ya kikazi iliyofanyika tarehe 25 Februari 2026.Ziara hiyo ni sehemu ya utaratibu wa kawaida wa uongozi wa Taasisi kutembelea vituo vyake nchini kwa lengo la kufuatilia utendaji kazi, maendeleo ya miundombinu pamoja na mchango wa tafiti katika kuboresha huduma za afya kwa jamii.Akiwa kituoni hapo, Prof. Aboud alikagua ukarabati wa majengo uliofanyika, maendeleo ya kitengo cha upimaji wa magonjwa mbalimbali kinachotumika katika tafiti pamoja na mifumo ya utunzaji na usimamizi wa takwimu zinazozalishwa katika maabara. Alielezwa kuwa maboresho hayo yamelenga kuongeza ubora wa huduma za uchunguzi wa magonjwa na kuimarisha mazingira ya kufanyia tafiti.Akimkaribisha Mkurugenzi Mkuu kuzungumza na watumishi, Mkuu wa Kituo cha NIMR Gonja, Ndugu Said Frank Magogo, alimshukuru Prof. Aboud kwa kuendelea kukipa kituo hicho ushauri wa kitaalamu, kuwapatia rasilimali watu, mashine za hematolojia na chemia hai pamoja na vitendanishi zilizochangia kuimarika kwa utekelezaji wa majukumu ya msingi ya kituo katika kufanya tafiti na kutoa huduma kwa wananchi.Akizungumza na wafanyakazi, Prof. Aboud aliwapongeza kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma katika utekelezaji wa majukumu yao, akieleza kuridhishwa kwake na maendeleo yaliyofikiwa hususan katika utoaji wa huduma za maabara kwa jamii pamoja na matumizi ya takwimu za tafiti katika kubaini maeneo mapya ya utafiti yanayolenga kutatua changamoto za afya nchini.Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha matumizi sahihi ya takwimu zinazozalishwa kupitia tafiti ili kuongeza ushahidi wa kisayansi utakaosaidia kupanga na kuboresha afua za afya kwa Watanzania.Ziara ya Mkurugenzi Mkuu katika Kituo cha NIMR Gonja ni sehemu ya juhudi za Taasisi za kuhakikisha vituo vyake vyote vinaendelea kuimarisha ubora wa tafiti, kuongeza ufanisi wa huduma za uchunguzi wa magonjwa na kutoa mchango endelevu katika maendeleo ya sekta ya afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Mkurugenzi Mkuu NIMR Aridhishwa na Maendeleo ya Utafiti na Huduma Kituo Kidogo cha Gonja. Read More »