Skip to content
Coat of arms of Tanzania

National Institute for Medical Research (NIMR)

Advancing Health Research, Enhancing Life

NIMR

Erick Mboma

Baraza la NIMR Lawataka Watafiti Kutumia Fursa Kuongeza Machapisho na Ubunifu

Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) limewataka watafiti kutumia ipasavyo fursa zilizopo katika vituo vya Taasisi kuongeza machapisho na ubunifu wa utafiti, ili kuzalisha ushahidi unaochangia kuboresha afya ya Watanzania na sera za afya.Wito huo umetolewa tarehe 1 Septemba 2026, wakati Baraza lilipotembelea vituo vya NIMR Mabibo na Muhimbili jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujionea kwa vitendo shughuli na utendaji wa vituo hivyo, kutathmini matumizi ya miundombinu na vifaa vya utafiti, pamoja na kusikiliza maoni na changamoto za watumishi.Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Prof. Muhammad Bakari Kambi, aliyemwakilisha Mwenyekiti wa Baraza, Prof. James Mdoe, alisema NIMR ina rasilimali watu wenye uwezo na miundombinu ya utafiti inayotoa fursa kwa watafiti kuongeza uzalishaji wa maarifa na machapisho, huku akiwasisitiza kutumia fursa hizo kuongeza mchango wa NIMR kitaifa na kimataifa.Prof. Kambi pia alisisitiza umuhimu wa kuongeza ubunifu katika tafiti na uzalishaji wa bidhaa za tiba asili, sambamba na kuimarisha masoko ya bidhaa hizo ili kuongeza matumizi na kuchangia mapato ya Taasisi. Aidha, aliwataka watumishi kutunza na kutumia kwa ufanisi uwekezaji wa Serikali katika miundombinu na vifaa vya utafiti, ikiwemo maabara na kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za tiba asili chenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 2.4.Katika ziara hiyo, Baraza lilitembelea maeneo mbalimbali ya vituo hivyo na kuona shughuli za utafiti, miundombinu na vifaa vinavyotumika katika utekelezaji wa majukumu ya Taasisi. Miongoni mwa maeneo yaliyotembelewa ni maabara za kituo cha NIMR Mabibo, shughuli za utafiti wa Kifua Kikuu na UKIMWI katika katika kituo cha NIMR Muhimbili, maabara ya Kifua Kikuu iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili inayosimamiwa na NIMR kwa kushirikiana na Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma (NTLP) pamoja na Wizara ya Afya, na Maabara ya Vinasaba vya Malaria iliyopo katika Ofisi ndogo za NIMR Dar es Salaam.Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, alisema NIMR Mabibo ina maabara tatu zenye mashine zaidi ya 80 zinazotumika katika tafiti na ufuatiliaji wa ubora wa dawa za tiba asili. Alisema kituo hicho pia kina mitambo takribani 15 ya uzalishaji wa dawa, ambapo mitambo tisa tayari inafanya kazi na sita ikiwa katika hatua za usimikaji.Prof. Aboud alisema NIMR Mabibo imegundua bidhaa sita za tiba asili ambazo zipo katika hatua za awali, huku utafiti na majaribio yakiendelea. Kwa upande wa NIMR Muhimbili, alisema kituo hicho kimeendelea kutoa mchango katika kuboresha sera na miongozo mbalimbali ya afya nchini na kimataifa, ikiwemo katika maeneo ya VVU, Kifua Kikuu na magonjwa yanayohusiana nayo.Aliongeza kuwa NIMR Muhimbili inaendelea kuongeza machapisho kupitia ushirikiano na hospitali mbalimbali, matumizi ya kanzidata za tafiti za afya na tafiti za kimfumo zinazolenga kuunganisha ushahidi kutoka tafiti mbalimbali.Baraza pia lilipata fursa ya kukutana na watumishi wa vituo hivyo na kusikiliza maoni yao kuhusu utendaji wa kazi, changamoto wanazokabiliana nazo na maeneo yanayohitaji maboresho. Prof. Kambi aliwahakikishia watumishi kuwa changamoto zilizowasilishwa zitafanyiwa kazi, huku akiwapongeza kwa kazi wanayoifanya na kueleza kuridhishwa na maendeleo ya vituo hivyo.Ziara hiyo iliwezesha Baraza kupata uelewa wa moja kwa moja kuhusu shughuli, mafanikio, fursa na changamoto za vituo hivyo, pamoja na kutathmini maeneo yanayohitaji msukumo zaidi katika kuimarisha utendaji wa NIMR. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Baraza la NIMR Lawataka Watafiti Kutumia Fursa Kuongeza Machapisho na Ubunifu Read More »

Serikali Yataka Tiba Asili Zenye Ushahidi wa Kisayansi Kujumuishwa Katika Mfumo Rasmi wa Afya

Serikali imetoa wito kwa watafiti na wadau wa tiba asili kuongeza kasi ya tafiti, uthibitishaji wa kisayansi na uwekezaji katika uzalishaji wa dawa za tiba asili, ili zenye ushahidi wa usalama, ubora na ufanisi ziweze kujumuishwa katika mfumo rasmi wa afya nchini.Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya, katika Kongamano la Tano la Kisayansi la Tiba Asili lililofanyika leo, tarehe 28 Agosti 2026, katika Ukumbi wa Eden Highlands Hotel, Jijini Mbeya, ambapo alimwakilisha Naibu Katibu Mkuu – Dawa na Vifaa Tiba wa Wizara ya Afya, Mhe. Emanuel Tayari, aliyekuwa Mgeni Rasmi.Balozi Dkt. Ulisubisya amesema Tanzania ina utajiri mkubwa wa maliasili na maarifa ya tiba asili ambayo yanaweza kuwa sehemu ya suluhisho la changamoto mbalimbali za afya, iwapo yatafanyiwa tafiti za kutosha na kuthibitishwa kisayansi.Amesema Serikali inahitaji kuona ongezeko la tafiti za tiba asili, uwekezaji katika maendeleo ya dawa hizo pamoja na kuimarika kwa uzalishaji katika viwanda vya ndani.Aidha, ametoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya wanasayansi, wataalamu wa tiba asili, wataalamu wa afya, taasisi za udhibiti, vyuo vikuu, watunga sera na sekta nyingine, ili kujenga mfumo unaowezesha tiba asili zenye ushahidi kutumika kwa usalama ndani ya huduma rasmi za afya.Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Prof. James E. Mdoe, amesema maendeleo ya tiba asili yanahitaji kujenga daraja kati ya sayansi ya kisasa na maarifa ya jadi yaliyorithishwa na jamii kwa vizazi.Prof. Mdoe amesema Kongamano hilo ni fursa kwa watafiti, wataalamu wa tiba asili, watunga sera, watoa huduma za afya na wadau wengine kujadili ushahidi uliopo, changamoto na fursa za kuendeleza tiba asili nchini.Akizungumza katika Kongamano hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amesema Taasisi hiyo kupitia Kituo cha Utafiti wa Tiba Asili Mabibo imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya maabara kwa ajili ya kuimarisha msingi wa kisayansi wa dawa za tiba asili.Prof. Aboud amesema maabara hizo tayari zinatumika kufuatilia ubora wa dawa 45 zinazopatikana kupitia mpango wa huduma jumuishi, ambapo dawa hizo zimewafikia zaidi ya wagonjwa 2,000 katika hospitali 14 za rufaa za mikoa.Prof. Aboud pia amesema NIMR inakamilisha taratibu za kuhakikisha Kiwanda cha Dawa za Tiba Asili Mabibo kinafunguliwa rasmi katika mwaka wa fedha 2026/27.Kongamano hilo, lenye kaulimbiu “Kuongeza Kasi ya Ujumuishaji wa Tiba Asili Zenye Ushahidi wa Kisayansi Katika Mifumo Rasmi ya Afya: Jukumu la Ushirikiano wa Sekta Mbalimbali,” limewakutanisha wataalamu wa tiba asili na tiba mbadala, watafiti, watoa huduma za afya, watunga sera, taasisi za udhibiti, vyuo vikuu na washirika wa maendeleo. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Serikali Yataka Tiba Asili Zenye Ushahidi wa Kisayansi Kujumuishwa Katika Mfumo Rasmi wa Afya Read More »

Prof. Mdoe Asisitiza Kukamilishwa kwa Ukarabati wa Kituo cha NIMR Tukuyu

Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James E. Mdoe, amesema ataendelea kushirikiana na Menejimenti ya NIMR katika kuhakikisha maeneo yaliyobaki ya ukarabati wa Kituo Kidogo cha Utafiti cha NIMR Tukuyu yanakamilishwa.Prof. Mdoe ametoa kauli hiyo Agosti 27, 2026, wakati wa ziara ya siku moja katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Mbeya na Kituo Kidogo cha Utafiti cha NIMR Tukuyu, ikiwa ni sehemu ya kujionea shughuli za utafiti zinazoendelea katika vituo hivyo pamoja na hali ya miundombinu na mazingira ya kazi.Akiwa Tukuyu, Prof. Mdoe alielezwa na uongozi wa Kituo cha Utafiti cha NIMR Mbeya kuwa ukarabati wa kituo kidogo hicho unaendelea kwa kutumia vyanzo vya ndani vya mapato vya Taasisi. Prof. Mdoe alisisitiza umuhimu wa kukamilisha maeneo yaliyosalia ya ukarabati.Ziara hiyo pia ilimpa Prof. Mdoe fursa ya kujionea shughuli mbalimbali za utafiti zinazofanyika katika vituo hivyo, ikiwemo tafiti za Kifua Kikuu na Virusi vya UKIMWI katika Kituo cha NIMR Mbeya, pamoja na tafiti za ugonjwa wa Usubi zinazofanyika katika Kituo Kidogo cha Utafiti cha NIMR Tukuyu.Katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Mbeya, Prof. Mdoe alitembelea maabara za utafiti na kujionea matumizi ya mitambo ya kisasa kwa ajili ya shughuli za utafiti, pamoja na miundombinu ya kuhifadhi sampuli na majengo yanayotumika katika shughuli za kituo.Akizungumza na watumishi wa NIMR Mbeya na Tukuyu, Prof. Mdoe aliwatia moyo kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa bidii na weledi. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuboresha miundombinu na mazingira ya kazi ili kuwawezesha watumishi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.Prof. Mdoe pia amewataka wananchi kushiriki katika tafiti zinazofanywa na NIMR, akieleza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kuwezesha tafiti kuzalisha ushahidi wa kisayansi unaoweza kusaidia kutatua changamoto mbalimbali za afya zinazowakabili wananchi.Kwa upande wake, Mkuu wa Kituo cha Utafiti cha NIMR Mbeya, Dkt. Bariki Mtafya, amemshukuru Prof. Mdoe kwa kutembelea vituo hivyo na kupata fursa ya kujionea shughuli za utafiti pamoja na changamoto zinazowakabili watafiti.Dkt. Mtafya amesema uongozi wa kituo utaendelea kushirikiana na Menejimenti ya NIMR katika kushughulikia changamoto mbalimbali na kuhakikisha shughuli za utafiti zinaendelea kwa ufanisi. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Prof. Mdoe Asisitiza Kukamilishwa kwa Ukarabati wa Kituo cha NIMR Tukuyu Read More »

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Henry M. Jackson Foundation (HJF) ya Marekani zimejadili namna ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, ikiwa ni pamoja na kufanya tafiti za pamoja, kuimarisha uwezo wa watafiti na kutumia miundombinu iliyopo kupanua wigo wa tafiti nchini.Majadiliano hayo yalifanyika tarehe 13 Agosti 2026 katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Mbeya, wakati Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa HJF, Meja Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Marekani, Dkt. Joseph Caravalho, pamoja na ujumbe wake walipotembelea kituo hicho.Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, alisema kusainiwa kwa Hati ya Makubaliano (MoU) kati ya Serikali ya Tanzania na Marekani kunatoa fursa ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, hasa wakati ambapo mazingira ya ufadhili wa tafiti za afya duniani yanaendelea kubadilika.Prof. Aboud alisema NIMR imewekeza katika miundombinu ya utafiti katika Kituo cha Mbeya na vituo vyake vingine, ikiwemo maabara na vifaa vinavyowezesha tafiti mbalimbali za afya.Katika majadiliano hayo, pande hizo pia zilizungumzia mabadiliko katika ufadhili wa utafiti kutoka Marekani. Prof. Aboud alitoa shukrani kwa Serikali ya Marekani kwa mchango wake kupitia Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR), ambao umeunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya VVU na changamoto nyingine za afya ya umma.NIMR na HJF pia zilijadili maeneo ya ushirikiano wa baadaye, yakiwemo kuendeleza tafiti za pamoja, kujenga uwezo wa watafiti na kutafuta maeneo mapya ya ushirikiano wa kisayansi.Baada ya majadiliano, ujumbe wa HJF ulitembelea Maabara ya Usalama na Kinga ya Mwili (Safety and Immunology) ya Kituo cha NIMR Mbeya, ambapo ulijionea shughuli za utafiti zinazotekelezwa katika kituo hicho. Ujumbe huo pia ulielezwa kuhusu uwekezaji uliofanywa na Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo HJF, katika kuimarisha miundombinu ya kituo.Ziara hiyo ilihitimishwa kwa pande zote mbili kueleza utayari wa kuendeleza ushirikiano uliopo na kutumia miundombinu na uwezo wa watafiti kupanua tafiti za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya Read More »

NIMR to Lead Ethical Oversight in a Multicountry Trial Exploring New Approaches to Prevent Childhood Diarrhoeal Diseases.

The National Institute for Medical Research (NIMR) is leading ethical oversight in a new multicountry clinical trial investigating whether probiotics can enhance the protection provided by rotavirus vaccination and reduce diarrhoeal disease among children. This approach could also help reduce antibiotic exposure and contribute to efforts to address antimicrobial resistance (AMR).The PRoRota Clinical Trial was launched in Dar es Salaam on 18th August 2026 by Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS), in collaboration with NIMR and partners from Tanzania, Malawi, Côte d’Ivoire and Norway. The two-day kick-off meeting, held at White Sands Hotel, brought together researchers and partners from microbiology, infectious diseases, epidemiology, health economics, social sciences and public health.Speaking at the meeting, the Guest of Honour, Prof. Tumaini Nagu, Deputy Permanent Secretary in the Prime Minister’s Office responsible for Health, said childhood diarrhoeal diseases remain an important and preventable cause of illness and death among children. She highlighted the importance of research such as PRoRota in generating evidence on whether probiotics can strengthen the effectiveness of rotavirus vaccination, reduce diarrhoeal disease and potentially reduce antibiotic exposure and AMR. NIMR plays a key role in the consortium, including leading the Ethics Work Package to support ethical conduct and protection of infants that will participate in the trial across the three African countries. NIMR will also coordinate the project’s independent ethics oversight and Data Safety Monitoring Board. In addition, NIMR will co-lead the formative, acceptability and feasibility research, which will generate evidence on caregivers’, healthcare providers’ and other stakeholders’ perspectives and experiences to inform trial implementation and the potential future integration of probiotics into routine childhood immunization programmes.During opening remarks, the Director General Prof. Said Aboud reaffirmed NIMR commitment to ensuring that the trial is conducted in accordance with high ethical and scientific standards. He said the Institute will work closely with consortium partners to generate evidence that can contribute to improved prevention of childhood diarrhoeal diseases and inform future health decisions. The research will help establish not only whether the intervention works, but also how it may be received by caregivers and healthcare providers and if it can be implemented within participating healthcare systems.Childhood diarrhoeal diseases remain an important public health concern, while antibiotic use in managing infections adds to the broader challenge of AMR. By examining whether probiotics can strengthen the protection provided by rotavirus vaccination and potentially reduce antibiotic exposure, PRoRota seeks to generate evidence that could inform future approaches to childhood disease prevention and vaccination across the participating countries. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR to Lead Ethical Oversight in a Multicountry Trial Exploring New Approaches to Prevent Childhood Diarrhoeal Diseases. Read More »

NIMR TABORA RESEARCH CENTRE A CENTURY OF SCIENCE: A NEW ERA OF PUBLIC HEALTH IMPACT

From a Sleeping Sickness Unit to a Modern Public Health Research Hub For more than a century, NIMR Tabora has connected scientific discovery with practical public health action. Established in Tabora in 1922 to support regional control of sleeping sickness, the unit has evolved into one of Tanzania’s oldest public health research platforms and a strategic scientific presence in the western zone. Since it was taken by the National Institute for Medical Research (NIMR) in 1979, the Centre has maintained its excellence and focal point for sleeping sickness research and monitoring in the country. Because of changing dynamics of public health threats, its mandate has expanded from a single disease to a multidisciplinary portfolio covering infectious and non-infectious diseases, antimicrobial resistance, climate and health, outbreak preparedness, clinical research, genomics, data science and health systems. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR TABORA RESEARCH CENTRE A CENTURY OF SCIENCE: A NEW ERA OF PUBLIC HEALTH IMPACT Read More »

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Henry M. Jackson Foundation (HJF) ya Marekani zimejadili namna ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, ikiwa ni pamoja na kufanya tafiti za pamoja, kuimarisha uwezo wa watafiti na kutumia miundombinu iliyopo kupanua wigo wa tafiti nchini.Majadiliano hayo yalifanyika tarehe 13 Agosti 2026 katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Mbeya, wakati Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa HJF, Meja Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Marekani, Dkt. Joseph Caravalho, pamoja na ujumbe wake walipotembelea kituo hicho.Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, alisema kusainiwa kwa Hati ya Makubaliano (MoU) kati ya Serikali ya Tanzania na Marekani kunatoa fursa ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, hasa wakati ambapo mazingira ya ufadhili wa tafiti za afya duniani yanaendelea kubadilika.Prof. Aboud alisema NIMR imewekeza katika miundombinu ya utafiti katika Kituo cha Mbeya na vituo vyake vingine, ikiwemo maabara na vifaa vinavyowezesha tafiti mbalimbali za afya.Katika majadiliano hayo, pande hizo pia zilizungumzia mabadiliko katika ufadhili wa utafiti kutoka Marekani. Prof. Aboud alitoa shukrani kwa Serikali ya Marekani kwa mchango wake kupitia Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR), ambao umeunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya VVU na changamoto nyingine za afya ya umma.NIMR na HJF pia zilijadili maeneo ya ushirikiano wa baadaye, yakiwemo kuendeleza tafiti za pamoja, kujenga uwezo wa watafiti na kutafuta maeneo mapya ya ushirikiano wa kisayansi.Baada ya majadiliano, ujumbe wa HJF ulitembelea Maabara ya Usalama na Kinga ya Mwili (Safety and Immunology) ya Kituo cha NIMR Mbeya, ambapo ulijionea shughuli za utafiti zinazotekelezwa katika kituo hicho. Ujumbe huo pia ulielezwa kuhusu uwekezaji uliofanywa na Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo HJF, katika kuimarisha miundombinu ya kituo.Ziara hiyo ilihitimishwa kwa pande zote mbili kueleza utayari wa kuendeleza ushirikiano uliopo na kutumia miundombinu na uwezo wa watafiti kupanua tafiti za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya Read More »

NIMR and HJF Strengthen Health Research Collaboration

The National Institute for Medical Research (NIMR) and the U.S.-based Henry M. Jackson Foundation (HJF) have discussed strategies to strengthen the existing collaboration in health research including joint research, capacity building for researchers, and making better use of existing infrastructure to expand the scope of health research in Tanzania.The discussions took place on 13th August 2026 at the NIMR Mbeya Research Centre, during a visit by HJF President and Chief Executive Officer, retired U.S. Army Major General Dr. Joseph Caravalho, and his delegation.Speaking during the visit, NIMR Director General Prof. Said Aboud said the signing of the Memorandum of Understanding (MoU) between the Governments of Tanzania and the United States provides an opportunity to further strengthen bilateral cooperation in health research, particularly at a time when the global health research funding landscape is changing.Prof. Aboud noted that NIMR has invested in research infrastructure at the Mbeya Research Centre and its other centres, including laboratories and equipment that support a range of health research activities.The discussions also covered changes in U.S. research funding. Prof. Aboud expressed appreciation to the U.S. Government for its support through the President’s Emergency Plan for AIDS Relief (PEPFAR), which has contributed to Tanzania’s efforts to address HIV and other public health challenges.NIMR and HJF also discussed areas for future collaboration, including joint research, researcher capacity building and identifying new areas of scientific cooperation.Following the discussions, the HJF delegation visited the Safety and Immunology Laboratory at the NIMR Mbeya Research Centre, where they observed ongoing research activities. The delegation was also briefed on investments made by the Government in collaboration with various partners, including HJF, to strengthen the Centre’s research infrastructure.The visit concluded with both sides expressing their commitment to continuing the existing partnership and making use of available infrastructure and research capacity to expand health research in Tanzania. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR and HJF Strengthen Health Research Collaboration Read More »

NIMR and Museen Stade Strengthen Strategic Partnership to Advance Research, Heritage and Tourism at Amani Hill

The National Institute for Medical Research (NIMR) and Museen Stade of Germany have formalized their partnership through the signing of a collaboration agreement under the WAYS – Towards Fair and Sustainable International Partnerships Programme. The agreement was signed on 13th August 2026 at the NIMR Headquarters sub-Office in Dar es Salaam.The collaboration agreement follows the approval of funding by the German Federal Cultural Foundation under the four-year WAYS Programme, which is being jointly implemented by NIMR, Tanzania, and Museen Stade, Germany. The partnership seeks to promote sustainable and mutually beneficial cooperation in research, heritage preservation, education, and knowledge exchange.The four-year programme will be implemented at the NIMR Amani Centre, with a particular focus on strengthening the historical, scientific, educational, and tourism value of the Amani Hill Research Station. Key areas of implementation will include the establishment of a Museum of Medical History at the Amani Hill Station, promotion of research tourism, enhancement of the Botanical Garden, preservation and development of medicinal and herbal plantations for research purposes and the production of traditional medicines.As part of the partnership, NIMR and Museen Stade will jointly implement a touring exhibition programme in Tanzania, complemented by an educational programme designed to enhance public awareness and knowledge of the historical and scientific significance of the Amani Hill Station. The exhibition is expected to be presented at four locations corresponding to the field research sites associated with the project entitled “The Karl Braun Collection and the Role of the Amani Institute during the German Colonial Period in Tanzania” (Amani Stade Project). The research project is being jointly undertaken by NIMR and Museen Stade.Speaking following the signing of the agreement, Dr. Sebastian Möllers, Director of Museen Stade, Germany, reaffirmed his institution’s commitment to broadening and deepening its collaboration with NIMR. He emphasised the importance of expanding the partnership to include research institutions and institutions of higher learning based in Germany. He further expressed interest in establishing opportunities for student exchange programmes and other academic initiatives once a fully operational Training Centre has been established at NIMR Amani Hill. The proposed Centre is expected to provide specialized training and capacity-building programmes.Speaking during the signing ceremony, NIMR Director General, Professor Said Aboud reaffirmed NIMR commitment to strengthening and sustaining its partnership with Museen Stade. He underscored the strategic importance of the collaboration in advancing research, education, heritage conservation, and knowledge exchange.Professor Aboud further noted that the current partnership provides an important foundation and springboard for establishing additional collaborative research initiatives with other national and international institutions. He emphasised that NIMR remains committed to developing strategic partnerships that contribute to scientific advancement, institutional capacity development, preservation of Tanzania’s medical and scientific heritage, and the promotion of research-based tourism.The signing of the agreement marks an important milestone in the longstanding collaboration between NIMR and Museen Stade and provides a framework for further cooperation in research, education, cultural heritage preservation, institutional development, and international knowledge exchange. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR and Museen Stade Strengthen Strategic Partnership to Advance Research, Heritage and Tourism at Amani Hill Read More »

NIMR Mbeya Yawafikia Wakulima, Kuimarisha Ushirikishwaji wa Jamii katika Utafiti wa Afya.

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Kituo cha Mbeya, imetumia Maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nanenane) Kanda ya Kusini kuwafikia wananchi moja kwa moja, hususan wakulima ambao ni sehemu kubwa ya washiriki katika tafiti zake, kwa kutoa elimu ya afya, huduma za uchunguzi na elimu kuhusu tafiti za afya zinazofanyika katika Kanda ya Kusini.Maonesho hayo, yaliyofikia kilele tarehe 8 Agosti 2026, yalitoa fursa kwa Taasisi kuimarisha uhusiano na jamii na wadau mbalimbali, huku likiwafikia kundi muhimu la wananchi wanaoshiriki katika tafiti zake. Takriban asilimia 90 ya washiriki katika tafiti zinazofanywa katika kituo hicho ni wakulima, hivyo Nanenane imekuwa jukwaa muhimu la kuwafikia moja kwa moja na kuwaeleza umuhimu wa ushiriki katika tafiti zinazolenga kuboresha afya na ustawi wa jamii.Kupitia banda la NIMR, wananchi walipata huduma za uchunguzi wa afya bila malipo, zikiwemo upimaji wa Kifua Kikuu (TB), UKIMWI na Homa ya Ini, pamoja na ushauri wa afya kutoka kwa wataalamu. Huduma hizo zilienda sambamba na elimu kuhusu kinga, udhibiti wa magonjwa na umuhimu wa kupima afya mapema.Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, Afisa wa Jamii anayehusika na masuala ya Ushirikishwaji wa Jamii, Bw. Simeon Mwanyonga, alisisitiza umuhimu wa kuwafikishia wananchi elimu sahihi kuhusu magonjwa na kuwahamasisha kupima afya zao mara kwa mara.“Ni muhimu kuhakikisha wananchi wanapata elimu sahihi kuhusu magonjwa mbalimbali na umuhimu wa kupima afya zao mapema, ili kubaini hali zao na kuchukua hatua zinazostahili,” alisema Mwanyonga.Utekelezaji wa shughuli hizo ulifanyika kwa ushirikiano kati ya Kitengo cha Ushirikishwaji wa Jamii, Bodi ya Ushauri ya Jamii (CAB), Mwitikio wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma (MKUTA) pamoja na wataalamu wa Kifua Kikuu.Kwa ujumla, ushiriki huo umeendelea kuimarisha ushirikishwaji wa jamii katika utafiti kwa kuwafikia wananchi katika mazingira yao, kuwaongezea uelewa kuhusu tafiti zinazofanyika na umuhimu wa ushiriki wao. Kupitia majukwaa kama Nanenane, utafiti unasogezwa karibu zaidi na jamii, huku wananchi wakipata fursa ya kuelewa na kushiriki katika tafiti zinazolenga kujibu changamoto za afya nchini.Ushiriki huo ulienda sambamba na kaulimbiu ya Nanenane 2026 isemayo, “Tambua Soko, Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050,” ambapo maadhimisho ya kitaifa yalifanyika jijini Dodoma. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

NIMR Mbeya Yawafikia Wakulima, Kuimarisha Ushirikishwaji wa Jamii katika Utafiti wa Afya. Read More »

Dira 2050