NIMR

June 9, 2026

Waziri Mchengerwa Aipongeza NIMR kwa Tafiti Zinazoimarisha Huduma za Afya na Kuchochea Maendeleo ya Taifa

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa mchango wake mkubwa katika kufanya tafiti na ubunifu unaoendelea kuboresha matibabu, kupunguza gharama za huduma za afya na kuimarisha mifumo ya afya nchini.Akifungua rasmi Kongamano la Kisayansi la 33 la NIMR lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Mhe. Mchengerwa aliyemwakilishi Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alisema Serikali inatambua mchango wa taasisi hiyo katika kusaidia kutambua, kutathmini na kuimarisha afua mbalimbali za kupambana na magonjwa huku matokeo ya tafiti yakiendelea kuwa nyenzo muhimu katika kuboresha sera na huduma za afya kwa wananchi. Aidha, Mhe. Mchengerwa alisisitiza kuwa uwekezaji katika utafiti si anasa bali ni mkakati wa maendeleo ya taifa unaosaidia kujenga uwezo wa kutatua changamoto kwa ushahidi na ubunifu wa kisayansi, huku ukichochea maendeleo ya sekta mbalimbali na ukuaji wa uchumi.Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Modest Mkude, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, alisema kongamano hilo limefanyika wakati muafaka ambapo Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutekeleza sera ya Bima ya Afya kwa Wote, hatua inayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha..Naye Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Prof. James Mdoe, alisema kwa zaidi ya miaka 40 taasisi hiyo imeendelea kufanya tafiti zenye mchango mkubwa katika kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza, afya ya mama na mtoto, lishe, afya ya jamii na maeneo mengine ya kipaumbele.“Baraza la NIMR linaendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Afya katika kuhakikisha kuwa matokeo ya tafiti yanatumika kikamilifu katika kuboresha sera, mipango na utoaji wa huduma za afya nchini,” alisema Prof. Mdoe.Akitoa taarifa ya taasisi, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, alisema kongamano la mwaka huu limekusanya watafiti, wataalamu wa afya, watunga sera na washirika wa maendeleo kujadili nafasi ya ushahidi wa kisayansi katika kuimarisha mifumo ya afya na kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Prof. Aboud alisema NIMR imeendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta ya afya kupitia tafiti zilizosaidia maboresho ya sera, huduma za matibabu, kinga dhidi ya magonjwa na matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa tafiti za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Waziri Mchengerwa Aipongeza NIMR kwa Tafiti Zinazoimarisha Huduma za Afya na Kuchochea Maendeleo ya Taifa Read More »

Mchengerwa Aitaka NIMR Kuharakisha Ugeuzaji wa Tafiti Kuwa Uchumi Halisi

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa fedha kwa kuendesha zoezi la kuandaa hesabu za miezi tisa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua inayolenga kuhakikisha uwajibikaji, usahihi wa taarifa za kifedha na matumizi bora ya fedha za umma.Zoezi hilo linafanyika mjini Morogoro kuanzia tarehe 18 hadi 30 Mei 2026, likiwakutanisha wataalamu kutoka Idara ya Fedha na Uhasibu wa vituo vyote vya NIMR kwa ajili ya kupitia, kuhakiki na kuandaa taarifa za kifedha zitakazowezesha taasisi kuwa na mifumo madhubuti ya usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha.Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amewapongeza wahasibu na wataalamu wa fedha kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuhakikisha taasisi inaendelea kuwa mfano wa uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za umma.Amesisitiza umuhimu wa kuandaa taarifa za fedha kwa umakini, weledi, usahihi na kwa wakati ili kuimarisha uwazi wa kifedha pamoja na kuhakikisha hoja za wakaguzi zinapatiwa ufumbuzi mapema na kwa ufanisi.Prof. Aboud pia ametoa shukrani kwa wataalamu wa mifumo kutoka Wizara ya Fedha kwa kuendelea kutoa usimamizi shirikishi pamoja na mchango wao katika kuboresha Mfumo wa Uhasibu wa Serikali wa MUSE, hatua inayochochea ufanisi, kasi na ubora wa upatikanaji wa taarifa za fedha Serikalini.Wataalamu wa fedha na uhasibu wa NIMR wamesema maboresho ya Mfumo wa MUSE yatawezesha upatikanaji wa taarifa za fedha kwa haraka, kwa usahihi na kwa ufanisi zaidi, hatua itakayoimarisha usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma pamoja na kusaidia utekelezaji wenye tija wa shughuli za utafiti na huduma za afya nchini. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Mchengerwa Aitaka NIMR Kuharakisha Ugeuzaji wa Tafiti Kuwa Uchumi Halisi Read More »