NIMR

Katika kusheherekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, wanawake wa Kituo cha Utafiti cha NIMR Tanga wameadhimisha siku hiyo kwa kutembelea Kituo cha Watoto Yatima cha FURAHA, kilichopo Raskazone, jijini Tanga, na kutoa msaada wa mahitaji muhimu kama unga, mchele, mafuta, sabuni za kufulia na za kuogea. Baada ya kukabidhi vitu hivyo, watoto hao walionyesha furaha na shukurani zao kupitia nyimbo na michezo mbalimbali.
Maadhimisho haya hufanyika kila tarehe 08 Machi. Mwaka huu, yalikuwa na kaulimbiu isemayo: “Haki ya Mwanamke na Wasichana, Msingi wa Maendeleo Jumuishi Kufikia Dira 2050.”
Akizungumza kwenye tukio hilo kwa niaba ya wanawake wa NIMR Tanga, Dr. Veneranda Bwana alisema ni desturi ya wanawake wa NIMR kushiriki katika masuala ya jamii, na akasisitiza kwamba kila siku ni fursa ya kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya wengine. “Siku ya Wanawake Duniani ni fursa ya kusherehekea wanawake, lakini pia ni wakati wa kuonyesha mshikamano na wale walioko kwenye hali ngumu,” alisisitiza Dr. Bwana.
Msimamizi wa kituo hicho aliwashukuru wanawake wa NIMR Tanga kwa msaada huo na akakaribisha wadau mbalimbali kuendeleza jitihada za kutoa misaada, akibainisha kwamba watoto hao wanahitaji msaada ili kuendeleza maisha yao.

Section Title

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha...

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji...

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua...

MFANYAKAZI HODARI WA NIMR 2026

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

WAFANYAKAZI HODARI 2026 NGAZI YA TAASISI

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 30th April 2026, officially launched a new project aimed at strengthening Tanzania’s capacity to predict and respond to Mpox outbreak using...

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.