Katika kusheherekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, wanawake wa Kituo cha Utafiti cha NIMR Tanga wameadhimisha siku hiyo kwa kutembelea Kituo cha Watoto Yatima cha FURAHA, kilichopo Raskazone, jijini Tanga, na kutoa msaada wa mahitaji muhimu kama unga, mchele, mafuta, sabuni za kufulia na za kuogea. Baada ya kukabidhi vitu hivyo, watoto hao walionyesha furaha na shukurani zao kupitia nyimbo na michezo mbalimbali.
Maadhimisho haya hufanyika kila tarehe 08 Machi. Mwaka huu, yalikuwa na kaulimbiu isemayo: “Haki ya Mwanamke na Wasichana, Msingi wa Maendeleo Jumuishi Kufikia Dira 2050.”
Akizungumza kwenye tukio hilo kwa niaba ya wanawake wa NIMR Tanga, Dr. Veneranda Bwana alisema ni desturi ya wanawake wa NIMR kushiriki katika masuala ya jamii, na akasisitiza kwamba kila siku ni fursa ya kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya wengine. “Siku ya Wanawake Duniani ni fursa ya kusherehekea wanawake, lakini pia ni wakati wa kuonyesha mshikamano na wale walioko kwenye hali ngumu,” alisisitiza Dr. Bwana.
Msimamizi wa kituo hicho aliwashukuru wanawake wa NIMR Tanga kwa msaada huo na akakaribisha wadau mbalimbali kuendeleza jitihada za kutoa misaada, akibainisha kwamba watoto hao wanahitaji msaada ili kuendeleza maisha yao.
Section Title
Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.



