NIMR

Imeelezwa kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuendeleza tafiti za tiba asili na kuwekeza zaidi katika viwanda vya kuzalisha dawa za tiba hizo nchini, ili kuongeza tija katika kuboresha huduma za afya kwa jamii. Kwa sasa, wananchi wengi wameonyesha mwamko mkubwa wa kutumia dawa za tiba asili.
Kauli hiyo imetolewa leo, Agosti 29, 2025 na Dkt. Ahmad Mohamed Makuwani Mkurugenzi wa Huduma ya Afya ya Uzazi, Magonjwa ya Wanawake na Watoto kutoka Wizara ya Afya, alipomuwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya katika Kongamano la Nne la Kisayansi la Tiba Asili lililoandaliwa na kuratibiwa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gaspar, jijini Dodoma.
Dkt. Makuani amewataka watafiti na wadau wa tiba asili kuwekeza nguvu katika kupata ushahidi wa kisayansi wa dawa hizo utakaosaidia kuimarisha sera za afya na kukuza ushirikiano kati ya wanasayansi na wataalamu wa tiba asili.
“Ili kuendeleza usawa wa afya, ni lazima dawa za tiba asili ambazo zimethibitishwa kuwa salama, zenye ufanisi na ubora ziingizwe rasmi kwenye mifumo ya utoaji huduma za afya. Tanzania tayari imeweka msingi imara kupitia Sheria ya Tiba Asili na Tiba Mbadala ya mwaka 2002 pamoja na Sheria ya NIMR ya mwaka 1980,” amesisitiza Dkt. Makuani.
Aidha, amependekeza kuundwa kwa mifumo ya ushirikiano na rufaa kati ya tiba asili na tiba za kisasa, kujumuisha tiba asili katika miongozo ya matibabu, na kujenga uaminifu kati ya wataalamu wa afya na waganga wa tiba asili.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amesema taasisi hiyo ina jukumu kubwa la kuhakikisha usalama, ufanisi na ubora wa dawa za tiba asili, ili kumlinda mwananchi dhidi ya madhara yanayoweza kusababishwa na dawa zisizo salama.
Prof. Aboud amewataka waganga na wataalamu wa tiba asili kupeleka dawa zao NIMR na katika taasisi zingine zenye mamlaka ili zipimwe na kuthibitishwa. “Hii itawezesha dawa hizo kuwa sehemu ya huduma jumuishi katika hospitali 14 za rufaa nchini,” amesisitiza Prof. Aboud.
Kongamano hilo la siku moja limewakutanisha wadau wa tiba asili kutoka ndani na nje ya nchi, ambapo walijadili matokeo ya tafiti mbalimbali. Kongamano hilo pia limeambatana na Maonesho ya Wiki ya Tiba Asili ya Mwafrika, yaliyofunguliwa

Section Title

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

NIMR Director General Honored for Outstanding Contributions to Advancing Medical Science, Research and Capacity Building

The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof. Said S. Aboud, has been honoured with the African Excellence and Personality Award (AEPA 2026) in Medical Science...

NIMR Scientists Ranked Among Tanzania Top 50 by the AD Scientific Index 2026

The National Institute for Medical Research (NIMR) has once again demonstrated its leadership in scientific research with five of its distinguished scientists ranked among the Top 50 scientists in...

Decade-Long Research Led by NIMR Shapes Africa’s Push for Integrated HIV and NCD Care

New evidence from a decade of research led by Tanzania’s National Institute for Medical Research (NIMR) on integrated HIV and non-communicable disease (NCD) care is driving renewed efforts across...

Watumishi NIMR Wapatiwa Mafunzo ya Maadili ya Utumishi wa Umma, Rushwa Mahali pa Kazi na Afya ya Akili

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kujenga watumishi wenye weledi, uadilifu, uwajibikaji na afya njema kwa kuendesha mafunzo maalumu...

NIMR Researchers Shine with DZIF Early Career Scientists Grant

Researchers from the National Institute for Medical Research (NIMR), Mbeya Centre, have earned international recognition after five early career scientists were awarded the prestigious Deutsches...

NIMR Yasisitiza Tafiti Zinazotatua Changamoto za Afya Katika Maandalizi ya Bajeti ya 2026/2027

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said Aboud, ameitaka taasisi hiyo kuimarisha uwezo wake wa kifedha na kuwekeza katika tafiti zinazolenga kutatua...