NIMR, Wizara ya Afya Watoa Mafunzo kwa Wataalamu wa Afya Kutumia Teknolojia ya Uchambuzi na Ufuatiliaji wa Vinasaba vya Magonjwa ya Mlipuko
Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa Kushirikiana na Wizara ya Afya, tarehe 18/08/2025 imeanza mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa maabara na watafiti kutoka taasisi mbalimbali za afya, lengo likiwa ni kuimarisha uwezo wa Wizara ya Afya na taasisi zake katika kuchambua (Bioinformatics) takwimu za mpangilio wa vinasaba (NGS data) za magonjwa ya mlipuko zinazozalishwa nchini Tanzania, ili kutambua aina na kufuatilia mabadiliko ya vimelea hivyo vya maradhi.Akifungua mafunzo hayo ya siku tano yanayofanyika mjini Morogoro, Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Epidemiolojia na Udhibiti wa Magonjwa kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Vida Mmbaga, amesema mafunzo hayo ni hatua muhimu katika kuimarisha uwezo wa wataalamu wa maabara kutumia teknolojia ya kisasa katika mapambano dhidi ya magonjwa ya mlipuko. “Kuchakata takwimu hizi kutasaidia kutoa usaidizi kwa nguzo zingine za udhibiti ambazo zinafanya kazi kwa pamoja na maabara, kwani kazi ya utabibu inategemea utambuzi kutoka maabara. Hivyo, wataalamu hawa wakiboresha uchambuzi wa kina, utaalamu wao utasaidia zaidi katika kudhibiti magonjwa,” amesema Dkt. Mmbaga. Ameongeza kuwa Serikali inalenga kuboresha uchakataji wa takwimu za vimelea vya maradhi kwa usahihi ili kusaidia kudhibiti magonjwa kwa ufanisi na uhakika.Naye Dkt. Clara Lubinza Mtafiti kutoka NIMR na Mratibu Msaidizi wa Mradi wa Global Heath Security ambao NIMR inatekeleza kwa kushirikiana na Wizara ya Afya amesema mafunzo hayo yatawasaidia wataalamu wa afya na maabara kuweza kuvisoma vinasaba vya vimelea vya magonjwa, kuvielewa ni vimelea vya aina gani na kuvitambua vinapokua vinabadilika. Aidha Dkt. Clara ameeleza kuwa matarajio baada ya mafunzo hayo ni kuhakikisha wataalamu wa afya wanapata uwezo wa kuchambua na kutambua vimelea vinavyosababisha magonjwa mbalimbali, kubaini tabia, aina na maeneo vinaposambaa, na kutambua mapema iwapo vitabadilika. “Hatua hii itawawezesha watalaamu wetu kutoa taarifa kwa Wizara ya Afya kwa wakati, ili kuchukua hatua za haraka za kudhibiti na kuzuia usambazaji zaidi wa vimelea hivyo.” Alieleza Dkt. Clara. Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na NIMR kwa kushirikiana na Wizara ya Afya yamewakutanisha pamoja wataalamu kutoa NIMR, Wizara ya Afya, Maabara Kuu ya Taifa ya Afya ya Jamii, Hospital ya Magonjwa ya Mlipuko Kibong`oto, na Maabara ya Afya ya Jamii ya Zanzibar. Section Title NIMR, Wizara ya Afya Watoa Mafunzo kwa Wataalamu wa Afya Kutumia Teknolojia ya Uchambuzi na Ufuatiliaji wa Vinasaba vya Magonjwa ya Mlipuko ByErick Mboma August 20, 2025 Uncategorized Section Title Heri ya Siku ya Wakulima “Nanenane” ByErick Mboma August 8, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR), in partnership with the University of Oslo… Read More Heri ya Siku ya Wakulima “Nanenane” ByErick Mboma August 8, 2025 Uncategorized Section Title Heri ya Siku ya Wakulima “Nanenane” ByErick Mboma August 8, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR), in partnership with the University of Oslo… Read More NIMR Hosts Pandemic Ethics Project General Assembly, Welcomes Experts from Six Countries ByErick Mboma July 30, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR), in partnership with the University of Oslo, hosted a high-level Pandemic Ethics General Assembly today 30th July 2025, at its Sub Office in Dar es… Read More NIMR Management Trained on Corporate Entrepreneurship ByErick Mboma July 30, 2025 Uncategorized In a strategic move to enhance institutional sustainability and increase revenue collections, the National Institute for Medical Research (NIMR) has conducted a high-level training on corporate… Read More NIMR Highlights Digital Health Solutions for HIV-Exposed Infants at National Child Health Congress ByErick Mboma July 27, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR) played a pivotal role in the 2nd Tanzania Child Health and Welfare Congress, held from 23rd – 25th July 2025 in Arusha, by spotlighting cutting-edge… Read More Mwenyekiti Mpya wa Baraza la NIMR Aonyesha Dhamira ya Kuimarisha Utafiti wa Afya ByErick Mboma July 26, 2025 Uncategorized Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James Mdoe, leo tarehe 25 Julai 2025 amefanya ziara ya kikazi katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Muhimbili… Read More Mwenyekiti Mpya wa Baraza la NIMR Apongeza Kituo cha Utafiti wa Dawa za Tiba Asili Mabibo ByErick Mboma July 25, 2025 Uncategorized Mwenyekiti mpya wa Baraza la Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James Mdoe, amefurahishwa na kazi inayofanywa na Kituo cha Utafiti wa Dawa za Tiba Asili cha NIMR Mabibo katika… Read More NIMR Yaanza Utekelezaji wa Utafiti wa Majaribio ya Dawa Kutokomeza Maambukizi ya Ugonjwa wa Matende na Mabusha Lindi na Mtwara ByErick Mboma July 16, 2025 Uncategorized Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeanza rasmi utekelezaji wa utafiti wa majaribio ya tiba ya kuharakisha kutokomeza maambukizi ya ugonjwa wa matende na mabusha. Hayo… Read More NIMR Yawanoa Watafiti Vijana Kuandika Maandiko ya Tafiti za Afya Yanayoweza Kushindana Kimataifa ByErick Mboma July 1, 2025 Uncategorized aasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendesha mafunzo maalumu kwa watafiti vijana 13 kuhusu namna ya kuandaa maandiko ya tafiti za afya kwa madhumuni ya kuvutia washirika wa… Read More









