NIMR

Mwenyekiti mpya wa Baraza la Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James Mdoe, amefurahishwa na kazi inayofanywa na Kituo cha Utafiti wa Dawa za Tiba Asili cha NIMR Mabibo katika kuendeleza tafiti za tiba mbadala kwa afya ya Watanzania.
Pongezi hizo alizitoa tarehe 24 Juni, 2025 alipofanya ziara ya kikazi kituoni hapo. Prof. Mdoe alitembelea kituo hicho kwa ajili ya kujitambulisha na kuona maendeleo ya tafiti, ugunduzi na uzalishaji wa tiba asili.
Akimkaribisha katika kituo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud alimpongeza Prof. James Mdoe kwa kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi na kumuahidi kumpa ushirikiano ili kufanikisha malengo ya Taasisi. Aliwasilisha taarifa ya kituo iliyoeleza mafanikio mbalimbali katika maeneo ya rasilimali watu, vitendea kazi, miundombinu ya majengo na maabara pamoja na maendeleo ya uzalishaji ya dawa za tiba asili. Akizungumza na watumishi wa kituo hicho, Mwenyekiti wa Baraza alielekeza Taasisi kuandaa mpango mkakati wa kutofautisha huduma na biashara, watafiti kuongeza machapisho ya tafiti, kusajili haki miliki, kuongeza ushirikiano na taasisi nyingine za tiba asili kama ITM na watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufanikisha malengo ya Taasisi.
Prof. Mdoe alisisitiza kuwa tiba asili ni hazina muhimu inayoweza kutoa suluhisho la changamoto nyingi za kiafya na akahimiza juhudi zaidi katika kukuza ubunifu na utafiti katika eneo hilo. Pia alishukuru kwa mapokezi mazuri na kuahidi kuendelea kushirikiana na Taasisi katika kuhakikisha kituo kinapiga hatua zaidi.

Section Title

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha...

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji...

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua...

MFANYAKAZI HODARI WA NIMR 2026

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

WAFANYAKAZI HODARI 2026 NGAZI YA TAASISI

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 30th April 2026, officially launched a new project aimed at strengthening Tanzania’s capacity to predict and respond to Mpox outbreak using...

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...