NIMR

Mwenyekiti mpya wa Baraza la Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James Mdoe, amefurahishwa na kazi inayofanywa na Kituo cha Utafiti wa Dawa za Tiba Asili cha NIMR Mabibo katika kuendeleza tafiti za tiba mbadala kwa afya ya Watanzania.
Pongezi hizo alizitoa tarehe 24 Juni, 2025 alipofanya ziara ya kikazi kituoni hapo. Prof. Mdoe alitembelea kituo hicho kwa ajili ya kujitambulisha na kuona maendeleo ya tafiti, ugunduzi na uzalishaji wa tiba asili.
Akimkaribisha katika kituo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud alimpongeza Prof. James Mdoe kwa kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi na kumuahidi kumpa ushirikiano ili kufanikisha malengo ya Taasisi. Aliwasilisha taarifa ya kituo iliyoeleza mafanikio mbalimbali katika maeneo ya rasilimali watu, vitendea kazi, miundombinu ya majengo na maabara pamoja na maendeleo ya uzalishaji ya dawa za tiba asili. Akizungumza na watumishi wa kituo hicho, Mwenyekiti wa Baraza alielekeza Taasisi kuandaa mpango mkakati wa kutofautisha huduma na biashara, watafiti kuongeza machapisho ya tafiti, kusajili haki miliki, kuongeza ushirikiano na taasisi nyingine za tiba asili kama ITM na watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufanikisha malengo ya Taasisi.
Prof. Mdoe alisisitiza kuwa tiba asili ni hazina muhimu inayoweza kutoa suluhisho la changamoto nyingi za kiafya na akahimiza juhudi zaidi katika kukuza ubunifu na utafiti katika eneo hilo. Pia alishukuru kwa mapokezi mazuri na kuahidi kuendelea kushirikiana na Taasisi katika kuhakikisha kituo kinapiga hatua zaidi.

Section Title

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

NIMR Director General Honored for Outstanding Contributions to Advancing Medical Science, Research and Capacity Building

The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof. Said S. Aboud, has been honoured with the African Excellence and Personality Award (AEPA 2026) in Medical Science...

NIMR Scientists Ranked Among Tanzania Top 50 by the AD Scientific Index 2026

The National Institute for Medical Research (NIMR) has once again demonstrated its leadership in scientific research with five of its distinguished scientists ranked among the Top 50 scientists in...

Decade-Long Research Led by NIMR Shapes Africa’s Push for Integrated HIV and NCD Care

New evidence from a decade of research led by Tanzania’s National Institute for Medical Research (NIMR) on integrated HIV and non-communicable disease (NCD) care is driving renewed efforts across...

Watumishi NIMR Wapatiwa Mafunzo ya Maadili ya Utumishi wa Umma, Rushwa Mahali pa Kazi na Afya ya Akili

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kujenga watumishi wenye weledi, uadilifu, uwajibikaji na afya njema kwa kuendesha mafunzo maalumu...

NIMR Researchers Shine with DZIF Early Career Scientists Grant

Researchers from the National Institute for Medical Research (NIMR), Mbeya Centre, have earned international recognition after five early career scientists were awarded the prestigious Deutsches...

NIMR Yasisitiza Tafiti Zinazotatua Changamoto za Afya Katika Maandalizi ya Bajeti ya 2026/2027

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said Aboud, ameitaka taasisi hiyo kuimarisha uwezo wake wa kifedha na kuwekeza katika tafiti zinazolenga kutatua...

Mkurugenzi Mkuu NIMR Aridhishwa na Maendeleo ya Utafiti na Huduma Kituo Kidogo cha Gonja.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said S. Aboud, ameridhishwa na maendeleo ya shughuli za utafiti na utoaji wa huduma za maabara yanayoendelea...

Wanawake wa NIMR Mbeya Waadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake kwa Matendo ya Huruma na Elimu ya Uwiano wa Majukumu ya Kazi na Familia.

Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, tarehe 08 Machi, wanawake wa Taasisi ya Taifa ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Kituo cha Mbeya walionyesha mshikamano na kujitolea kwa jamii...