NIMR

Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James Mdoe, leo tarehe 25 Julai 2025 amefanya ziara ya kikazi katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Muhimbili, akiambatana na Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud.
Katika ziara hiyo, Prof. Mdoe ametembelea Maabara Kuu ya Kifua Kikuu, ambayo inaendeshwa kwa ushirikiano kati ya Kituo cha NIMR Muhimbili na Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma wa Wizara ya Afya. Maabara hiyo ni miongoni mwa nguzo muhimu katika mapambano dhidi ya kifua kikuu nchini na kanda ya Afrika. Alisisitiza kuwa mwelekeo wa uongozi wake ni kuona NIMR inazidi kung’ara kitaifa na kimataifa kupitia tafiti za afya zenye athari chanya kwa jamii.
Baada ya kutembelea maabara, Prof. Mdoe alipata nafasi ya kuzungumza na watumishi wa kituo hicho ambapo aliwatia moyo kuongeza tija na ubunifu katika kazi zao za utafiti, akisisitiza umuhimu wa kufikia malengo ambayo Taasisi imejiwekea. Aliahidi kushirikiana kwa karibu na menejimenti ya Taasisi katika kuhakikisha changamoto zilizopo zinatatuliwa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR Prof. Said Aboud alimpongeza Prof. Mdoe kwa kuteuliwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Baraza la NIMR.
Aidha aliwapongeza watumishi wa Kituo cha NIMR Muhimbili kwa mchango wao mkubwa katika kushiriki kutengeneza sera na miongozi ya tiba ya kifua kikuu na UKIMWI kitaifa na kimataifa kutokana na matokeo ya tafiti. Hata hivyo, aliwasihi kuongeza juhudi katika kuchapisha matokeo ya tafiti na kuandaa vijarida sera ili kuongeza ushahidi wa kisayansi kutoka katika kazi za utafiti wanazofanya. “Katika mwaka wa fedha 2024/25, tumefanikiwa kuchapisha machapisho 46 ya tafiti za afya katika majarida ya kitaifa, kikanda na kimataifa na vijarida sera 12 kutoka katika kituo cha NIMR Muhimbili. Hili ni jambo la kujivunia lakini bado tuna nafasi ya kufanya vizuri zaidi,” alisema Prof. Aboud.
Ziara hiyo imeonesha dhamira ya dhati ya uongozi wa juu wa NIMR katika kuimarisha usimamizi, kuongeza uwajibikaji na kuendeleza utafiti wa afya unaolenga kuboresha maisha ya Watanzania.

Section Title

NIMR Yatoa Matokeo ya Utafiti Kuonyesha Mwelekeo Mpya wa Kujenga Ustahimilivu Dhidi ya Magonjwa ya Mlipuko Yanayosababishwa na Wadudu Dhurifu

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), tarehe 26 Februari 2026, kupitia mradi wa RAFT (Resilience Against Future Threats through Vector Control), imewasilisha matokeo ya utafiti...

NIMR Director General Strengthens Research Direction at Tanga Centre to Address National Health Priorities

The Tanga Medical Research Centre had the honor of hosting Professor Said Aboud, the Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), on 24th February 2026, during an official...

NIMR and EAHRC Launch Landmark National Workshop on Evidence-Based Healthcare

The National Institute for Medical Research (NIMR) in collaboration with the East African Health Research Commission (EAHRC), have launched the 1st National Workshops on Ethics and Clinical Research...

NIMR Yazindua Utafiti wa Utoaji wa Dawa ya Kichocho kwa Watoto Chini ya Miaka Mitano Kupitia Mradi wa STEPPES

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa STEPPS (Strengthening Health System Capacity for Access and Delivery of Paediatric Praziquantel for Schistosomiasis in...

NIMR na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe Zasaini Hati ya Makubaliano Kushirikiana Katika Tafiti Nchini

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe (MNMH) leo tarehe 13/02/2026 zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) inayolenga kuimarisha...

NIMR Yawanoa Watumishi wa Afya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Kuandika Maandiko ya Utafiti Kuboresha Huduma za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo cha Muhimbili, imewajengea uwezo watumishi wa afya 18 wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana (Amana RRH) katika uandishi wa...

WRAIR Delegation Visits NIMR–Mbeya Centre to Advance HIV Research Collaboration

The National Institute for Medical Research – Mbeya Medical Research Centre (NIMR-MMRC) on 10th February 2026 hosted a high-level delegation from Walter Reed Army Institute of Research (WRAIR) in a...

Matokeo ya utafiti wa EPInA yaonesha kupungua kwa usubi na kifafa Mahenge

Kiwango cha ugonjwa wa usubi kwa watu wenye kifafa katika eneo la Mahenge, Wilaya ya Ulanga, Mkoa wa Morogoro, kimepungua hadi asilimia 22, huku maambukizi kwa ujumla yakipungua kwa takribani asilimia...

NIMR Emerges as a Global and Regional Leader in EDCTP-Supported Health Research

The National Institute for Medical Research (NIMR) in Tanzania, has been recognized as a leading contributor to internationally competitive health research following its strong performance in...