Skip to content
Coat of arms of Tanzania

National Institute for Medical Research (NIMR)

Advancing Health Research, Enhancing Life

NIMR

Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James Mdoe, leo tarehe 25 Julai 2025 amefanya ziara ya kikazi katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Muhimbili, akiambatana na Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud.
Katika ziara hiyo, Prof. Mdoe ametembelea Maabara Kuu ya Kifua Kikuu, ambayo inaendeshwa kwa ushirikiano kati ya Kituo cha NIMR Muhimbili na Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma wa Wizara ya Afya. Maabara hiyo ni miongoni mwa nguzo muhimu katika mapambano dhidi ya kifua kikuu nchini na kanda ya Afrika. Alisisitiza kuwa mwelekeo wa uongozi wake ni kuona NIMR inazidi kung’ara kitaifa na kimataifa kupitia tafiti za afya zenye athari chanya kwa jamii.
Baada ya kutembelea maabara, Prof. Mdoe alipata nafasi ya kuzungumza na watumishi wa kituo hicho ambapo aliwatia moyo kuongeza tija na ubunifu katika kazi zao za utafiti, akisisitiza umuhimu wa kufikia malengo ambayo Taasisi imejiwekea. Aliahidi kushirikiana kwa karibu na menejimenti ya Taasisi katika kuhakikisha changamoto zilizopo zinatatuliwa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR Prof. Said Aboud alimpongeza Prof. Mdoe kwa kuteuliwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Baraza la NIMR.
Aidha aliwapongeza watumishi wa Kituo cha NIMR Muhimbili kwa mchango wao mkubwa katika kushiriki kutengeneza sera na miongozi ya tiba ya kifua kikuu na UKIMWI kitaifa na kimataifa kutokana na matokeo ya tafiti. Hata hivyo, aliwasihi kuongeza juhudi katika kuchapisha matokeo ya tafiti na kuandaa vijarida sera ili kuongeza ushahidi wa kisayansi kutoka katika kazi za utafiti wanazofanya. “Katika mwaka wa fedha 2024/25, tumefanikiwa kuchapisha machapisho 46 ya tafiti za afya katika majarida ya kitaifa, kikanda na kimataifa na vijarida sera 12 kutoka katika kituo cha NIMR Muhimbili. Hili ni jambo la kujivunia lakini bado tuna nafasi ya kufanya vizuri zaidi,” alisema Prof. Aboud.
Ziara hiyo imeonesha dhamira ya dhati ya uongozi wa juu wa NIMR katika kuimarisha usimamizi, kuongeza uwajibikaji na kuendeleza utafiti wa afya unaolenga kuboresha maisha ya Watanzania.

Section Title

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Henry M. Jackson Foundation (HJF) ya Marekani zimejadili namna ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, ikiwa ni pamoja na kufanya...

NIMR to Lead Ethical Oversight in a Multicountry Trial Exploring New Approaches to Prevent Childhood Diarrhoeal Diseases.

The National Institute for Medical Research (NIMR) is leading ethical oversight in a new multicountry clinical trial investigating whether probiotics can enhance the protection provided by rotavirus...

NIMR TABORA RESEARCH CENTRE A CENTURY OF SCIENCE: A NEW ERA OF PUBLIC HEALTH IMPACT

From a Sleeping Sickness Unit to a Modern Public Health Research Hub For more than a century, NIMR Tabora has connected scientific discovery with practical public health action. Established in Tabora...

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Henry M. Jackson Foundation (HJF) ya Marekani zimejadili namna ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, ikiwa ni pamoja na kufanya...

NIMR and HJF Strengthen Health Research Collaboration

The National Institute for Medical Research (NIMR) and the U.S.-based Henry M. Jackson Foundation (HJF) have discussed strategies to strengthen the existing collaboration in health research including...

NIMR and Museen Stade Strengthen Strategic Partnership to Advance Research, Heritage and Tourism at Amani Hill

The National Institute for Medical Research (NIMR) and Museen Stade of Germany have formalized their partnership through the signing of a collaboration agreement under the WAYS – Towards Fair and...

NIMR Mbeya Yawafikia Wakulima, Kuimarisha Ushirikishwaji wa Jamii katika Utafiti wa Afya.

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Kituo cha Mbeya, imetumia Maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nanenane) Kanda ya Kusini kuwafikia wananchi moja kwa moja, hususan wakulima...

Today is your last opportunity to submit your abstract for the 5th Traditional Medicine Scientific Conference.

Today is your last opportunity to submit your abstract for the 5th Traditional Medicine Scientific Conference.Share your research, engage with experts, and contribute to advancing evidence-based...

NIMR, Partners Advance Efforts to Strengthen Tanzania’s Clinical Trial Oversight Framework

The National Institute for Medical Research (NIMR) in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), other local and international partners, on 28th July, 2026...
Dira 2050