NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeanza rasmi utekelezaji wa utafiti wa majaribio ya tiba ya kuharakisha kutokomeza maambukizi ya ugonjwa wa matende na mabusha. Hayo yamebainishwa wakati wa kuendesha mafunzo ya siku mbili ya kutekeleza utafiti kwa watafiti na watoa huduma wa afya kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara.
Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, yalifunguliwa rasmi na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Mwinjuma M. Mkungu. Katika hotuba yake, aliipongeza NIMR kwa kuwa kinara wa tafiti za afya nchini na kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya katika kuandaa tafiti zenye lengo la kumaliza kabisa magonjwa yanayosumbua jamii, hususani yale yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (NTDs).
“NIMR ni nguzo muhimu katika sekta ya afya kwa kuwa inatoa ushahidi wa kisayansi unaosaidia kupanga na kutekeleza afua bora. Mafunzo haya ni sehemu ya juhudi hizo,” alisema Mhe. Mkungu.
Mafunzo hayo yamefuatiwa na kuanza kwa uchukuaji wa sampuli kwa washiriki wa utafiti katika kijiji cha Ruaha, kata ya Mnazi Mmoja, Wilaya ya Lindi. Utafiti huu wa kisayansi unalenga kulinganisha tiba tofauti za magonjwa ya matende na mabusha, hususani dawa ya “Doxycycline” na “Moxidectin + Albendazole”, dhidi ya Kingatiba iliyopo sasa ya “Ivermectin + Albendazole”.
Mtafiti Mkuu wa mradi wa utafiti kutoka NIMR, Dkt. Akili Kalinga, alisema kuwa tafiti hizi zinalenga kutafuta tiba mbadala na bora zaidi ambazo zitaweza kuharakisha kutokomeza ugonjwa huo nchini. “Tumekuwa kwenye mapambano dhidi ya matende na mabusha kwa miaka mingi. Tunategemea kuwa utafiti huu utasaidia kuondoa kabisa vikwazo vinavyosababisha maambukizi ya Ugonjwa huu kuendelea katika baadhi ya maeneo.” alisema Dkt. Kalinga.
Akizungumza wakati wa zoezi la uchukuaji wa sampuli, Mwenyekiti wa Kijiji cha Ruaha, Bi. Salima Kidamchong`we, alisema kuwa utafiti huo ni muhimu sana kwa jamii yao kwa sababu unawapa fursa ya kujua hali yao ya kiafya. “Tunatoa shukrani kwa NIMR na Wizara ya Afya kwa kutuletea utafiti huu. Ni jambo la maana na lenye manufaa kwa wananchi wetu,” alisema.
Naye mmoja wa washiriki wa utafiti kutoka kijiji cha Ruaha kata ya Mnazi Mmoja, Bw. Ali Bakari Natulama, aliipongeza NIMR kwa juhudi zake na kusema kwamba tafiti kama hizi zinasaidia sana katika kuelimisha jamii na kuwakinga na magonjwa hatari kama matende na mabusha.
Kwa sasa, ugonjwa wa matende na mabusha bado upo katika baadhi ya Halmashauri za wilaya nchini Tanzania ikiwemo Lindi Manispaa, Mtama, Mikindani, Kinondoni na Pangani. Licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa Halmashauri 114 kutokomeza maambukizi ya Ugonjwa na kusitisha ugawaji wa kingatiba uliofanyika kwa miaka mingi.
NIMR inatarajia kutumia matokeo ya utafiti huu kuboresha miongozo ya kitaifa na kidunia ya tiba na udhibiti wa magonjwa haya, kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya na wadau wengine.

Section Title

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

NIMR Director General Honored for Outstanding Contributions to Advancing Medical Science, Research and Capacity Building

The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof. Said S. Aboud, has been honoured with the African Excellence and Personality Award (AEPA 2026) in Medical Science...

NIMR Scientists Ranked Among Tanzania Top 50 by the AD Scientific Index 2026

The National Institute for Medical Research (NIMR) has once again demonstrated its leadership in scientific research with five of its distinguished scientists ranked among the Top 50 scientists in...

Decade-Long Research Led by NIMR Shapes Africa’s Push for Integrated HIV and NCD Care

New evidence from a decade of research led by Tanzania’s National Institute for Medical Research (NIMR) on integrated HIV and non-communicable disease (NCD) care is driving renewed efforts across...

Watumishi NIMR Wapatiwa Mafunzo ya Maadili ya Utumishi wa Umma, Rushwa Mahali pa Kazi na Afya ya Akili

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kujenga watumishi wenye weledi, uadilifu, uwajibikaji na afya njema kwa kuendesha mafunzo maalumu...

NIMR Researchers Shine with DZIF Early Career Scientists Grant

Researchers from the National Institute for Medical Research (NIMR), Mbeya Centre, have earned international recognition after five early career scientists were awarded the prestigious Deutsches...

NIMR Yasisitiza Tafiti Zinazotatua Changamoto za Afya Katika Maandalizi ya Bajeti ya 2026/2027

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said Aboud, ameitaka taasisi hiyo kuimarisha uwezo wake wa kifedha na kuwekeza katika tafiti zinazolenga kutatua...

Mkurugenzi Mkuu NIMR Aridhishwa na Maendeleo ya Utafiti na Huduma Kituo Kidogo cha Gonja.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said S. Aboud, ameridhishwa na maendeleo ya shughuli za utafiti na utoaji wa huduma za maabara yanayoendelea...