NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa STEPPS (Strengthening Health System Capacity for Access and Delivery of Paediatric Praziquantel for Schistosomiasis in Tanzania) tarehe 18 Februari 2026 imezindua rasmi Utafiti wa utoaji wa dawa ya kichocho aina ya paediatric praziquantel kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, hatua inayopanua wigo wa matibabu kwa kundi ambalo kwa muda mrefu halikujumuishwa katika kampeni za utoaji dawa kwa pamoja. Uzinduzi huo umefanyika jijini Mwanza wakati wa Warsha ya Wadau ya kuanza kwa utoaji wa dawa hiyo chini ya Mradi wa STEPPS.
Akizindua rasmi utafti huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, amesema hatua hiyo ni ya kihistoria kwa Tanzania, hasa baada ya nchi kuwa ya kwanza katika ukanda huu na huenda duniani kusajili dawa ya paediatric praziquantel. Ameongeza kuwa matokeo ya mwisho ya utekelezaji wa mradi huo yataisaidia Serikali kuiingiza dawa hiyo katika mwongozo rasmi wa utoaji wa huduma za afya nchini. Ameeleza kuwa ushahidi wa kisayansi uliokusanywa kwa zaidi ya muongo mmoja umeonesha kuwa watoto chini ya miaka mitano wanaoishi katika maeneo yenye maambukizi makubwa ya kichocho wanaweza pia kuambukizwa, hali iliyosukuma juhudi za kutafuta mfumo maalumu wa dawa kwa kundi hilo la watoto chini ya miaka mitano. Aidha, amesema Serikali inaendelea kufanya jitihada za kupambana na ugonjwa huo kupitia utoaji wa elimu kwa jamii, utekelezaji wa afua za kinga na tiba pamoja na kuboresha usimamizi wa maji katika maeneo yenye maambukizi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amesema uzinduzi huo ni matokeo ya safari ndefu ya utafiti, ubunifu na ushirikiano wa kimataifa ulioanza mwaka 2020 kupitia Mradi wa STEPPS. Amefafanua kuwa katika hatua ya utekelezaji, mifumo miwili jumuishi ya utoaji dawa—Test and Treat na Mass Drug Administration (MDA)—ilijaribiwa ili kubaini njia bora yenye ufanisi, gharama nafuu na inayokubalika zaidi kwa jamii kabla ya upanuzi wa kitaifa.
Naye Mtafiti Kiongozi wa mradi huo, Dkt. Paul Erasto Kazyoba, amesema tafiti zimeonesha kuwa watoto chini ya umri wa miaka mitano pia wana maambukizi ya kichocho, ilhali awali afua za dawa zililenga zaidi watoto wa umri wa kwenda shule kuanzia miaka sita. Ameongeza kuwa dawa hiyo imefanyiwa majaribio na imeonesha usalama na ufanisi kwa watoto wadogo, ikiwa na maboresho makubwa ikilinganishwa na dawa ya awali, ikiwemo kupunguza usumbufu uliokuwa ukijitokeza kwa baadhi ya watumiaji. Amesisitiza kuwa mradi huo umejengwa juu ya ushirikiano kati ya NIMR, Wizara ya Afya na washirika wa maendeleo wakiwemo UNDP, WHO/TDR na PATH, kwa ufadhili wa GHIT Fund ya Japan pamoja na END FUND.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa UNDP na Naibu Mwakilishi Mkazi wa Tanzania, Bw. John Rutere, amesema taasisi hiyo imeona umuhimu wa kushirikiana na NIMR, Serikali na wadau wengine katika kuhakikisha watoto chini ya miaka mitano wanapata dawa stahiki ya kutibu kichocho, akibainisha kuwa ushirikiano huo utaendelea si tu katika kudhibiti kichocho bali pia katika kushughulikia changamoto nyingine za afya ya jamii. Naye Bi. Grace Bahati, mkazi wa Kijiji cha Ishayahisho, Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, ameishukuru NIMR kwa mradi huo wa utafiti akisema utasaidia kubaini maambukizi ya kichocho mapema na kuwapatia watoto dawa, hatua itakayochangia kulinda afya ya jamii.
Warsha hiyo imewakutanisha wadau kutoka ndani na nje ya nchi kujadili mikakati ya kuongeza upatikanaji wa dawa hiyo nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki, sambamba na kuimarisha mifumo ya afya kwa ajili ya kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ifikapo mwaka 2030. Warsha hiyo ilitanguliwa na ziara ya kutembelea maeneo ambayo utafiti unafanyika, ikiwamo Hospitali ya Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, ambapo wadau walijionea zoezi la utambuzi wa ugonjwa na ugawaji wa dawa likiendelea.

Section Title

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha...

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji...

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua...

MFANYAKAZI HODARI WA NIMR 2026

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

WAFANYAKAZI HODARI 2026 NGAZI YA TAASISI

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 30th April 2026, officially launched a new project aimed at strengthening Tanzania’s capacity to predict and respond to Mpox outbreak using...

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.