Skip to content
Coat of arms of Tanzania

National Institute for Medical Research (NIMR)

Advancing Health Research, Enhancing Life

NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo cha Muhimbili, imewajengea uwezo watumishi wa afya 18 wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana (Amana RRH) katika uandishi wa maandiko ya utafiti (Proposal Development), hatua inayolenga kuboresha huduma za afya kwa jamii kupitia tafiti zenye ubora na ushahidi wa kisayansi.

Mafunzo hayo ya siku nne yalifanyika kuanzia tarehe 26 hadi 29 Januari 2026 katika hospitali hiyo yakilenga kuwawezesha watoa huduma wa afya kubuni, kuandaa na kuwasilisha mapendekezo bora ya tafiti za kisayansi zinazoweza kupata ufadhili na kuleta matokeo chanya katika sekta ya afya.

Kupitia mafunzo hayo ya vitendo, washiriki walipata ujuzi wa kuandaa maandiko ya kisayansi yenye viwango, kuimarisha uwezo wa uandishi wa kitaaluma, kuelewa na kuzingatia maadili ya utafiti pamoja na kutumia takwimu sahihi katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili wananchi.

Akifungua mafunzo hayo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dkt. Bryceson Loti Kiweru, alisema utafiti ni nyenzo muhimu isiyoweza kuepukika katika sekta ya afya.

“Swala zima la utafiti haliepukiki katika sekta ya afya na inahitajika ushirikiano na taasisi zinazofanya utafiti ili kuboresha huduma za afya nchini,” alisema Dkt. Kiweru.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Idara ya Tafiti kutoka kituo cha NIMR Muhimbili, Dkt. Ester Mbutolwe, alisisitiza umuhimu wa matumizi sahihi ya takwimu katika kuibua suluhisho la changamoto za afya.

“Kila mtu akijengewa uwezo vizuri anaweza kutoa mchango wake katika kuboresha afya za wananchi. Takwimu sahihi ni msingi wa utafiti wenye matokeo ya kuaminika. Ushirikiano kati ya NIMR na hospitali za rufaa za mkoa ni muhimu,” alisisitiza Dkt. Mbutolwe.

Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za NIMR za kuimarisha tafiti za afya nchini kwa kuwajengea uwezo wataalamu walioko kwenye vituo vya kutolea huduma, ili tafiti zinazofanyika ziweze kutoa majibu ya changamoto halisi za jamii na kuboresha ubora wa huduma za afya nchini.

Section Title

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Henry M. Jackson Foundation (HJF) ya Marekani zimejadili namna ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, ikiwa ni pamoja na kufanya...

NIMR to Lead Ethical Oversight in a Multicountry Trial Exploring New Approaches to Prevent Childhood Diarrhoeal Diseases.

The National Institute for Medical Research (NIMR) is leading ethical oversight in a new multicountry clinical trial investigating whether probiotics can enhance the protection provided by rotavirus...

NIMR TABORA RESEARCH CENTRE A CENTURY OF SCIENCE: A NEW ERA OF PUBLIC HEALTH IMPACT

From a Sleeping Sickness Unit to a Modern Public Health Research Hub For more than a century, NIMR Tabora has connected scientific discovery with practical public health action. Established in Tabora...

NIMR na HJF Kuimarisha Ushirikiano wa Tafiti za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Henry M. Jackson Foundation (HJF) ya Marekani zimejadili namna ya kuendeleza ushirikiano katika tafiti za afya, ikiwa ni pamoja na kufanya...

NIMR and HJF Strengthen Health Research Collaboration

The National Institute for Medical Research (NIMR) and the U.S.-based Henry M. Jackson Foundation (HJF) have discussed strategies to strengthen the existing collaboration in health research including...

NIMR and Museen Stade Strengthen Strategic Partnership to Advance Research, Heritage and Tourism at Amani Hill

The National Institute for Medical Research (NIMR) and Museen Stade of Germany have formalized their partnership through the signing of a collaboration agreement under the WAYS – Towards Fair and...

NIMR Mbeya Yawafikia Wakulima, Kuimarisha Ushirikishwaji wa Jamii katika Utafiti wa Afya.

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Kituo cha Mbeya, imetumia Maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nanenane) Kanda ya Kusini kuwafikia wananchi moja kwa moja, hususan wakulima...

Today is your last opportunity to submit your abstract for the 5th Traditional Medicine Scientific Conference.

Today is your last opportunity to submit your abstract for the 5th Traditional Medicine Scientific Conference.Share your research, engage with experts, and contribute to advancing evidence-based...

NIMR, Partners Advance Efforts to Strengthen Tanzania’s Clinical Trial Oversight Framework

The National Institute for Medical Research (NIMR) in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), other local and international partners, on 28th July, 2026...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Dira 2050