NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo cha Muhimbili, imewajengea uwezo watumishi wa afya 18 wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana (Amana RRH) katika uandishi wa maandiko ya utafiti (Proposal Development), hatua inayolenga kuboresha huduma za afya kwa jamii kupitia tafiti zenye ubora na ushahidi wa kisayansi.

Mafunzo hayo ya siku nne yalifanyika kuanzia tarehe 26 hadi 29 Januari 2026 katika hospitali hiyo yakilenga kuwawezesha watoa huduma wa afya kubuni, kuandaa na kuwasilisha mapendekezo bora ya tafiti za kisayansi zinazoweza kupata ufadhili na kuleta matokeo chanya katika sekta ya afya.

Kupitia mafunzo hayo ya vitendo, washiriki walipata ujuzi wa kuandaa maandiko ya kisayansi yenye viwango, kuimarisha uwezo wa uandishi wa kitaaluma, kuelewa na kuzingatia maadili ya utafiti pamoja na kutumia takwimu sahihi katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili wananchi.

Akifungua mafunzo hayo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dkt. Bryceson Loti Kiweru, alisema utafiti ni nyenzo muhimu isiyoweza kuepukika katika sekta ya afya.

“Swala zima la utafiti haliepukiki katika sekta ya afya na inahitajika ushirikiano na taasisi zinazofanya utafiti ili kuboresha huduma za afya nchini,” alisema Dkt. Kiweru.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Idara ya Tafiti kutoka kituo cha NIMR Muhimbili, Dkt. Ester Mbutolwe, alisisitiza umuhimu wa matumizi sahihi ya takwimu katika kuibua suluhisho la changamoto za afya.

“Kila mtu akijengewa uwezo vizuri anaweza kutoa mchango wake katika kuboresha afya za wananchi. Takwimu sahihi ni msingi wa utafiti wenye matokeo ya kuaminika. Ushirikiano kati ya NIMR na hospitali za rufaa za mkoa ni muhimu,” alisisitiza Dkt. Mbutolwe.

Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za NIMR za kuimarisha tafiti za afya nchini kwa kuwajengea uwezo wataalamu walioko kwenye vituo vya kutolea huduma, ili tafiti zinazofanyika ziweze kutoa majibu ya changamoto halisi za jamii na kuboresha ubora wa huduma za afya nchini.

Section Title

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha...

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji...

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua...

MFANYAKAZI HODARI WA NIMR 2026

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

WAFANYAKAZI HODARI 2026 NGAZI YA TAASISI

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 30th April 2026, officially launched a new project aimed at strengthening Tanzania’s capacity to predict and respond to Mpox outbreak using...

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.