NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke. Mafunzo hayo ya siku tatu, yaliyofanyika kuanzia tarehe 26 hadi 28 Novemba 2025, yalilenga kuwajengea uwezo washiriki katika kubuni, kuandaa na kuwasilisha mapendekezo bora ya tafiti za kisayansi.
Katika mafunzo hayo, washiriki walipata fursa ya kufanya mazoezi kwa vitendo kuhusu hatua muhimu za uandishi wa andiko la utafiti, ikiwemo kuandaa mapendekezo yenye ubora, kuimarisha uwezo wa uandishi wa kisayansi, kuelewa na kutekeleza maadili ya utafiti, pamoja na kubadilisha mawazo ya kitaalamu na kuwa tafiti zenye matokeo chanya na zinazoweza kupata ufadhili.
Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mkurugenzi wa Kukuza na Kuratibu Tafiti NIMR (DRCP) Dkt. Nyanda E. Ntinginya, ameushukuru uongozi wa Hospitali ya Temeke kwa kuthamini umuhimu wa mafunzo hayo na kuhakikisha ushiriki mpana wa watumishi wake. Amesisitiza kuwa ujuzi walioupata washiriki unapaswa kutumika kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa kuanzisha, kuendesha na kuchapisha tafiti zenye manufaa kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
Dkt. Nyanda pia alibainisha kuwa NIMR itaendelea kuimarisha ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Temeke katika kukuza uwezo wa watumishi, kuendeleza tafiti za pamoja na kuhamasisha matumizi ya ushahidi wa kisayansi katika kuboresha huduma za afya nchini.
Mafunzo hayo yanaibua matumaini mapya kwa watumishi wa afya Temeke, huku yakitarajiwa kuongeza ubunifu, ushindani na tija katika uandaaji wa tafiti zenye mchango mkubwa katika mfumo wa afya wa Tanzania.

Section Title

Waziri Mchengerwa Aipongeza NIMR kwa Tafiti Zinazoimarisha Huduma za Afya na Kuchochea Maendeleo ya Taifa

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa mchango wake mkubwa katika kufanya tafiti na ubunifu unaoendelea kuboresha matibabu...

Mchengerwa Aitaka NIMR Kuharakisha Ugeuzaji wa Tafiti Kuwa Uchumi Halisi

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa fedha kwa kuendesha zoezi la kuandaa hesabu za miezi tisa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua...

NIMR YAONGEZA KASI YA UWAJIBIKAJI KUPITIA UANDAAJI WA HESABU ZA MIEZI TISA KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa fedha kwa kuendesha zoezi la kuandaa hesabu za miezi tisa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha...

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji...

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua...

MFANYAKAZI HODARI WA NIMR 2026

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

WAFANYAKAZI HODARI 2026 NGAZI YA TAASISI

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 30th April 2026, officially launched a new project aimed at strengthening Tanzania’s capacity to predict and respond to Mpox outbreak using...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.