NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), tarehe 26 Februari 2026, kupitia mradi wa RAFT (Resilience Against Future Threats through Vector Control), imewasilisha matokeo ya utafiti kuhusu magonjwa ya mlipuko yanayoenezwa na mbu pamoja na usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu, hatua inayolenga kuimarisha ustahimilivu wa taifa katika kukabiliana na vitisho vya magonjwa hayo.
Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Mkurugenzi wa Kuratibu na Kukuza Tafiti, Dkt. Nyanda Elias Ntinginya, amesema Tanzania inahitaji kuimarisha mifumo yake ya ufuatiliaji na maandalizi ili kukabiliana kwa ufanisi na ongezeko la vitisho vya magonjwa yanayoenezwa na mbu.
Amesisitiza kuwa tafiti za kisayansi zinapaswa kuwa msingi wa maamuzi ya kisera, hasa katika kipindi hiki ambacho mabadiliko ya mazingira, ukuaji wa miji na ongezeko la mwingiliano wa watu vinaongeza hatari ya milipuko ya magonjwa kama dengue na magonjwa mengine ya virusi yanayoenezwa na mbu.
Kwa upande wake, Mtafiti Kiongozi wa Mradi wa RAFT, Dkt. Alphaxard Manjurano, amesema lengo la mkutano huo lilikuwa kuwasilisha matokeo muhimu kuhusu usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu na vitisho vya magonjwa ya mlipuko yanayoenezwa na mbu, pamoja na kuyajadili kwa kina na wadau wakuu wa udhibiti wa wadudu dhurifu nchini.
Akiwasilisha matokeo ya tathmini ya kitaifa ya utayari wa mfumo wa afya kukabiliana na vitisho vya mbu, Dkt. Manjurano alibainisha kuwa licha ya kuwepo kwa vituo 34 vya ufuatiliaji wa malaria (sentinel sites), bado kuna haja ya kuanzisha programu mahsusi ya kitaifa ya ufuatiliaji wa kawaida wa mbu wanaoeneza magonjwa.
“Kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2024, ufuatiliaji wa mbu wa kuanzia hatua za mabuu hadi mbu waliokomaa haujawahi kufanyika kwa mfumo wa kitaifa. Hii inaonesha umuhimu wa kuimarisha mfumo wa utambuzi wa mapema wa hatari za milipuko ya magonjwa ya yanayoenezwa na wadudu,” alisisitiza Dkt. Manjurano.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya kupitia Programu ya Taifa ya Udhibiti wa Malaria, Bw. Winfred Mwafongo, amesema matokeo hayo yatasaidia kuboresha sera na miongozo ya kukabiliana na malaria na magonjwa mengine yanayoenezwa na wadudu.
Naye Mwakilishi kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Jovin Kitau, ameipongeza NIMR kwa kufanya utafiti huo, akisema utachangia kuimarisha kinga ya jamii dhidi ya magonjwa yanayoenezwa na wadudu na kuongeza usalama wa afya ya umma.
Aidha, Mtafiti Mkuu kutoka NIMR, Dkt. William Kisinza, amesema katika majadiliano ya kikao hicho wadau wamependekeza kuimarishwa kwa programu maalumu inayosimamia masuala ya wadudu dhurifu ili kuongeza ufanisi wa udhibiti wa magonjwa yanayoenezwa na wadudu.
Kwa upande wake, Bi. Jackeline Martin, Mtafiti kutoka NIMR aliyefanya utafiti kuhusu ufanisi wa viuatilifu vilivyopo kwenye vyandarua, amesema matokeo yanaonesha ongezeko la usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu hivyo, jambo linaloonesha umuhimu wa kuendelea kuboresha mikakati ya udhibiti ili kuhakikisha vyandarua vinaendelea kuwa na ufanisi.
Mkutano huo uliofanyika katika Hoteli ya Protea, jijini Dar es Salaam, uliwakutanisha wadau mbalimbali wa udhibiti wa wadudu dhurifu kutoka Wizara ya Afya, NIMR, Shirika la Afya Duniani (WHO), Taasisi ya Afya ya Ifakara, pamoja na wadau wengine wa sekta ya afya.

Section Title

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha...

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji...

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua...

MFANYAKAZI HODARI WA NIMR 2026

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

WAFANYAKAZI HODARI 2026 NGAZI YA TAASISI

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 30th April 2026, officially launched a new project aimed at strengthening Tanzania’s capacity to predict and respond to Mpox outbreak using...

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.