NIMR

Wananchi wanaendelea kunufaika na huduma za tiba asili kupitia tafiti, na uanzishwaji wa kiwanda cha kuzalisha dawa za tiba asili cha NIMR Mabibo kufuatia juhudi kubwa za Serikali kuhakikisha dawa salama na zenye ubora zinapatikana kwa wingi nchini.
Akizungumza tarehe 29 Agosti, 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Tiba Asili ya Mwafrika yaliyofanyika jijini Dodoma, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu, ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, aliipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa hatua kubwa zilizopigwa katika tafiti na uhamasishaji wa matumizi ya dawa za tiba asili.
Dkt. Kazungu alisema moja ya mafanikio makubwa ya NIMR ni uanzishwaji wa kiwanda cha Mabibo cha kuzalisha dawa za tiba asili ambacho kinatumia malighafi kutoka kwa wakulima wa miti dawa. “Kiwanda hiki hakijaishia tu kuzalisha dawa salama na zenye ufanisi na ubora, bali pia kimetoa fursa za ajira kwa wananchi na kuongeza kipato kwa wakulima wa malighafi hizo,” alisisitiza Dkt Kazungu.
Aidha, alitembelea banda la NIMR katika maonesho na kupongeza jitihada zilizofanywa huku akishauri kuimarisha tafiti zinazohusu tiba asili kwa magonjwa ya figo ambayo yanaongezeka kwa kasi katika siku za hivi karibuni.
Akitoa maelezo katika banda la NIMR Meneja wa kituo cha NIMR Mabibo Dkt. Emmanuel Peter alibainisha mchango wa NIMR katika kukuza tiba asili nchini kuwa ni pamoja na kufanya tafiti za tiba asili, kushiriki katika huduma jumuishi, kujenga kiwanda cha kuzalisha dawa za tiba asili, kuhamasisha tafiti, ugunduzi na matumizi ya dawa za tiba asili, kuimarisha ushirikiano na wadau wa tiba asili
Dkt. Peter alisema Kwa sasa, wananchi wanapata huduma jumuishi za tiba asili katika hospitali za rufaa za mikoa 14 ambapo mteja anaweza kuchagua tiba ya kisasa, tiba asili au kutumia zote kwa pamoja. “Huduma hii inamuwezesha mteja kufanyiwa vipimo vya kitaalamu na kupewa ushauri sahihi kuhusu tiba inayomfaa.
Maadhimisho hayo, yenye kaulimbiu “Tuimarishe Huduma za Tiba Asili Zenye Ushahidi wa Kisayansi,” yalianza tarehe 25 Agosti 2025 na yanatarajiwa kutamatika tarehe 31 Agosti 2025. Tukio hili limewakutanisha wataalamu wa tiba asili na tiba mbadala kutoka maeneo mbalimbali nchini, kwa lengo la kubadilishana uzoefu, na kuhamasisha matumizi ya dawa za tiba asili kwa manufaa ya jamii.

Section Title

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha...

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji...

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua...

MFANYAKAZI HODARI WA NIMR 2026

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

WAFANYAKAZI HODARI 2026 NGAZI YA TAASISI

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 30th April 2026, officially launched a new project aimed at strengthening Tanzania’s capacity to predict and respond to Mpox outbreak using...

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...