Skip to content
Coat of arms of Tanzania

National Institute for Medical Research (NIMR)

Advancing Health Research, Enhancing Life

NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo, tarehe 8 Januari 2026, imeendesha mkutano wa majadiliano ya sera uliowakutanisha watafiti, watunga sera, watoa maamuzi wa sekta ya afya na wadau mbalimbali, kwa lengo la kuimarisha matumizi ya ushahidi wa kisayansi katika kuandaa na kutekeleza sera zinazohusu maandalizi, kinga na mwitikio wa taifa dhidi ya magonjwa yanayolipuka na kurejea mara kwa mara.
Akifungua mkutano huo, Mgeni Rasmi Dkt. Ahmad Mohamed Makuwani, Mkurugenzi wa Huduma ya Afya ya Uzazi, Magonjwa ya Wanawake na Watoto kutoka Wizara ya Afya, akimwakilisha Mganga Mkuu wa Serikali, amesema kuwa majadiliano hayo yanakuja katika kipindi muhimu kwa taifa, ambapo kumekuwa na kuendelea kushuhudiwa kwa milipuko ya magonjwa kama kipindupindu, dengue, COVID-19 na Marburg. Amesema hali hiyo inaweka shinikizo kubwa kwa mifumo ya afya na hivyo kuhitaji sera zinazojengwa juu ya ushahidi madhubuti wa kisayansi.
“Mkutano huu ni jukwaa muhimu la kutafakari mazingira ya milipuko ya magonjwa nchini na kuimarisha uwezo wa pamoja wa taifa katika kuzuia, kugundua mapema na kukabiliana na vitisho vya afya ya jamii vya sasa na vya baadaye,” amebainisha Dkt. Makuwani. Ameongeza kuwa majadiliano ya sera ni nyenzo muhimu ya kuunganisha tafiti na maamuzi ya kisera ili kufanikisha uamuzi unaozingatia ushahidi.
Aidha, Dkt. Makuwani amesisitiza umuhimu wa kuimarisha tafiti za ndani, ikiwemo utafiti wa tiba asili, akibainisha kuwa uzoefu wa mlipuko wa UVIKO-19 umeonesha mchango wa tiba asili katika kupunguza madhara kwa jamii. Akitoa wito, ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika tafiti za tiba asili na mifumo ya kitaifa ya utafiti.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Profesa Said Aboud, amesema kuwa mkutano huo umeandaliwa mahsusi kushughulikia masuala nyeti yanayohusiana na magonjwa yenye uwezekano wa kusababisha milipuko, huku ukilenga kuhakikisha matokeo ya tafiti yanatafsiriwa na kutumika moja kwa moja katika sera na mipango ya kitaifa.
Prof. Aboud ameeleza kuwa mkutano huo ni jukwaa la tafsiri ya maarifa, linalowaunganisha watafiti, watunga sera na watekelezaji ili kujadili ushahidi uliopo, kubadilishana uzoefu na kuandaa mapendekezo yatakayosaidia kuimarisha maandalizi, kinga na mwitikio wa taifa dhidi ya milipuko ya magonjwa.
“Tafiti zinaonesha kuwa maandalizi madhubuti dhidi ya milipuko yanategemea mifumo imara ya ufuatiliaji wa magonjwa, nguvu kazi ya afya iliyo imara na minyororo thabiti ya upatikanaji wa vifaa tiba,” ameongeza Prof. Aboud.
James Tumain Tengia, mwakilishi kutoka Wizara ya TAMISEMI, ameipongeza NIMR kwa kuandaa mkutano huo, akisema kuwa umefanikiwa kuwakutanisha watafiti, watunga sera na watoa maamuzi ili kuchakata matokeo ya tafiti mbalimbali na kuja na maoni yatakayosaidia kuboresha sera na miongozo ya utoaji wa huduma za afya.
Elizabeth Shayo, Mtafiti Mkuu kutoka NIMR, amesema kuwa mkutano huo umekuwa na manufaa makubwa kwa kuwa umetoa fursa ya kujadili namna bora ya kupambana na magonjwa ya mlipuko yanayoweza kutokea nchini.
Akitoa majumuisho ya mkutano huo, Dkt. Ernest Mazigo, mtafiti kutoka NIMR na mratibu wa mdahalo huo amesema kuwa wadau ambao ni watunga sera na watoa maamuzi wamepokea mapendekezo mbalimbali yaliyotolewa na wameanza kuangalia namna ya kuyaingiza katika mifumo na utekelezaji wa sera za afya.
Mdahalo huo wa siku moja uliofanyika katika Ukumbi wa CEEMI, ofisi ndogo za NIMR jijini Dar es Salaam, ulijikita katika kuangalia namna ushahidi wa kisayansi unavyoweza kuboresha sera na miongozo ya utoaji wa huduma za afya nchini, pamoja na kubaini vipaumbele vya tafiti na mapungufu ya utekelezaji. Mdahalo huo uliandaliwa kwa ushirikiano wa wataalamu kutoka Kurugenzi ya Kuratibu na Kukuza Utafiti ya NIMR akiwemo Mr. Emmanuel Makundi, Dkt. Stellah Kilima na Dkt. Elizabeth Shayo, huku Profesa Moshi Ntabaye aliyeendesha mjadala huo akishiriki kikamilifu katika kufanikisha mdahalo huo wa sera.

Section Title

NIMR kupitia PEN-Plus Yafikisha Huduma za Magonjwa Yasiyoambukiza Karibu na Wananchi

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kupitia mradi wa utafiti wa PENPLUS imeendelea kuboresha utoaji wa huduma za magonjwa yasiyoambukiza nchini kwa kuwezesha Hospitali za Kondoa...

NIMR CONTINUES TO STRENGTHEN ETHICAL AND REGULATORY FRAMEWORK FOR TRADITIONAL MEDICINE RESEARCH IN TANZANIA

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched stakeholders’ consultation on draft Traditional Medicine Research Guidelines aimed at strengthening ethical and regulatory...

ELEVATING CLINICAL TRIAL OVERSIGHT IN AFRICA: TRACE TRAINING IN PROGRESS IN MOROGORO

Reviewers from regulatory and research institutions are currently gathered at the EDEMA Conference Hall in Morogoro for the Clinical Trial Reviewers Training (17–19 June 2026) under the TRACE...

Strengthening Africa’s Clinical Research Systems: NIMR Leads TRACE Training to Enhance Trial Oversight.

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa mchango wake mkubwa katika kufanya tafiti na ubunifu unaoendelea kuboresha matibabu...

Waziri Mchengerwa Aipongeza NIMR kwa Tafiti Zinazoimarisha Huduma za Afya na Kuchochea Maendeleo ya Taifa

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa mchango wake mkubwa katika kufanya tafiti na ubunifu unaoendelea kuboresha matibabu...

Mchengerwa Aitaka NIMR Kuharakisha Ugeuzaji wa Tafiti Kuwa Uchumi Halisi

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa fedha kwa kuendesha zoezi la kuandaa hesabu za miezi tisa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua...

NIMR YAONGEZA KASI YA UWAJIBIKAJI KUPITIA UANDAAJI WA HESABU ZA MIEZI TISA KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuimarisha mfumo wa usimamizi wa fedha kwa kuendesha zoezi la kuandaa hesabu za miezi tisa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, hatua...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha...

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.

Dira 2050