NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa (Sokoine) ili kuzindu awamu ya pili ya utekelezaji wa mradi.
Mkutano huo umetoa fursa ya kujadili mbinu bora za kutekeleza mradi unaolenga kupambana na vikwazo vya kupambana na ugonjwa wa mabusha na matende katika mkoa wa Lindi na mikoa mingine yenye tatizo hili.
Aidha mkutano huo umejikita katika kufanya mapitio ya utekelezaji wa awamu ya kwanza na kuweka mikakati thabiti kwa awamu ya pili ya kuendelea kupunguza maambukizi katika maeneo machache yaliyosalia na pia namana ya kuwahudumia wenye madhara ya mabusha na matende.
Akifungua mkutano huo, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Dkt. Enock S. Chilumba, aliishukuru NIMR kwa kuichagua Lindi kuwa eneo la utekelezaji wa mradi huo muhimu. Amesema kuwa mradi wa TAKeOFF awamu ya kwanza umesaidia kuibua wagonjwa wa maradhi ya mabusha na matende zaidi ya 4,000 na kwamba wagonjwa 3,571 walipatiwa matibabu kupitia Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele (NTDCP) kwa kushirikiana na wadau wengine wa afya.
“Kuwepo kwa NIMR Lindi ni fursa kubwa wanatusaidia kuwajengea uwezo watumishi wetu katika nyanja za utafiti na kuhakikisha tafiti zinakamilika kwa wakati na kuleta majibu yatakayoboresha huduma za afya,” alisema Dkt. Chilumba.
Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi – Sokoine, Dkt. Alexander Makalla, alisema kuwa majadiliano hayo yatasaidia kuzalisha nyaraka muhimu zitakazotumika kama mwongozo katika utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa mabusha na matende.
“Sisi kama Hospitali na wadau wengine tuko tayari na tumejipanga, msisite kutushirikisha pale mnapohitaji mchango wetu ili mradi huu uzalishe matokeo chanya,” alisisitiza Dkt. Makalla.
Akizungumza katika mkutano huo, Mtafiti Mkuu wa Mradi wa TAKeOFF, Dkt. Akili Kalinga, alisema kuwa lengo la kikao ni kushirikisha wadau muhimu katika hatua za mwanzo za mradi ili kuhakikisha kila upande una uelewa na ushiriki wa pamoja. Ameeleza kuwa Lindi ni miongoni mwa mikoa yenye maambukizi makubwa, hivyo ni muhimu kuimarisha jitihada katika awamu hii ya pili.
Katika mkutano huo, jumla ya tafiti tano ziliwasilishwa, ambazo zinatekelezwa chini ya mradi kuanzia mwaka 2024 hadi mwaka 2027, ambazo ni utafiti unaohusu Kulinganisha ubora wa mifumo ya kupima na kutibu kwa dawa ya ‘Doxycycline’ au ‘Moxidectin+Albendazole’ kwa kufananisha na Kingadawa ya ‘Ivermectin+Albendazole’ inayogawiwa kwa jamii kusaidia kutokomeza ugonjwa wa Matende na Mabusha nchini Ghana na Tanzania – Hatua ya 3 ya majaribio ya dawa katika mikoa ya Mtwara Lindi na Tanga, utafiti unaohusu Tathmini ya Maambukizi na changamoto kuelekea kutokomeza ugonjwa wa Usubi Tanzania: uzoefu wa eneo la maambukizi la Ruvuma baada ya zaidi ya miongo miwili ya ugawaji wa Kingatiba kwa jamii.
Tafiti zingine zilizowasilishwa ni Ufuatiliaji wa maradhi ya Matende na Mabusha na jinsi ya kuyatolea taarifa kwa kuwatumia watoa huduma za afya wa jamii ili wagonjwa waweze kupata huduma za kupunguza madhara na kuzuia ulemavu katika vituo vya kutolea huduma za afya, Utafiti wa kuangalia Uhusiano kati ya magonjwa yasioambukiza (NCDs) na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (NTDs) na utafiti wa Utambuzi wa vimelea vinavyosababisha homa za mitoki (ADL) kwa wagonjwa wa matende yanayosababishwa na minyoo ya Filaria.
Mkutano huo wa siku moja uliofanyika Lindi umewakutanisha wadau wa afya ikiwamo kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa( Sokoine), Watafiti na watumishi wa NIMR.

Section Title

NIMR Yatoa Matokeo ya Utafiti Kuonyesha Mwelekeo Mpya wa Kujenga Ustahimilivu Dhidi ya Magonjwa ya Mlipuko Yanayosababishwa na Wadudu Dhurifu

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), tarehe 26 Februari 2026, kupitia mradi wa RAFT (Resilience Against Future Threats through Vector Control), imewasilisha matokeo ya utafiti...

NIMR Director General Strengthens Research Direction at Tanga Centre to Address National Health Priorities

The Tanga Medical Research Centre had the honor of hosting Professor Said Aboud, the Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), on 24th February 2026, during an official...

NIMR and EAHRC Launch Landmark National Workshop on Evidence-Based Healthcare

The National Institute for Medical Research (NIMR) in collaboration with the East African Health Research Commission (EAHRC), have launched the 1st National Workshops on Ethics and Clinical Research...

NIMR Yazindua Utafiti wa Utoaji wa Dawa ya Kichocho kwa Watoto Chini ya Miaka Mitano Kupitia Mradi wa STEPPES

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa STEPPS (Strengthening Health System Capacity for Access and Delivery of Paediatric Praziquantel for Schistosomiasis in...

NIMR na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe Zasaini Hati ya Makubaliano Kushirikiana Katika Tafiti Nchini

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe (MNMH) leo tarehe 13/02/2026 zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) inayolenga kuimarisha...

NIMR Yawanoa Watumishi wa Afya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Kuandika Maandiko ya Utafiti Kuboresha Huduma za Afya

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo cha Muhimbili, imewajengea uwezo watumishi wa afya 18 wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana (Amana RRH) katika uandishi wa...

WRAIR Delegation Visits NIMR–Mbeya Centre to Advance HIV Research Collaboration

The National Institute for Medical Research – Mbeya Medical Research Centre (NIMR-MMRC) on 10th February 2026 hosted a high-level delegation from Walter Reed Army Institute of Research (WRAIR) in a...

Matokeo ya utafiti wa EPInA yaonesha kupungua kwa usubi na kifafa Mahenge

Kiwango cha ugonjwa wa usubi kwa watu wenye kifafa katika eneo la Mahenge, Wilaya ya Ulanga, Mkoa wa Morogoro, kimepungua hadi asilimia 22, huku maambukizi kwa ujumla yakipungua kwa takribani asilimia...

NIMR Emerges as a Global and Regional Leader in EDCTP-Supported Health Research

The National Institute for Medical Research (NIMR) in Tanzania, has been recognized as a leading contributor to internationally competitive health research following its strong performance in...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.