NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe (MNMH) leo tarehe 13/02/2026 zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) inayolenga kuimarisha mashirikiano katika tafiti, mafunzo na matumizi ya teknolojia za kisasa katika utoaji wa huduma bora za afya ya akili nchini.
Kupitia ushirikiano huu, taasisi hizo zitaongeza uwezo wa wataalamu wa afya ya akili kupitia mafunzo na tafiti shirikishi zitakazotoa ushahidi wa kisayansi kwa lengo la kuboresha sera, miongozo na utoaji wa huduma kwa kutumia teknolojia za kisasa ili kuongeza ufanisi na ubora kwa wananchi. Ushirikiano huo pia utahusisha utekelezaji wa pamoja wa miradi ya utafiti, kuandika machapisho ya kitaaluma, kuandaa vijarida sera na ushawishi katika kuboresha huduma kwa wananchi.
Makubaliano haya yanakusudia kupanua wigo wa tafiti katika eneo la afya ya akili, kuunganisha utaalamu, matumizi ya rasilimali watu wenye ubobezi na uzoefu wa taasisi hizo, na kuhakikisha matokeo ya tafiti yanawafikia wananchi na kuleta mabadiliko chanya katika maisha yao.
Hafla ya utiaji saini imefanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya NIMR jijini Dodoma na kuongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, akiwa na Meneja wa Kituo cha NIMR Dodoma, Dk. Basiliana Emidi. Kwa upande wa MNMH, ujumbe uliongozwa na Dk. Innocent R. Mwombeki aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji, akiongozana na Veronica Haule na Anewa Saweni.

Section Title

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

NIMR Director General Honored for Outstanding Contributions to Advancing Medical Science, Research and Capacity Building

The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof. Said S. Aboud, has been honoured with the African Excellence and Personality Award (AEPA 2026) in Medical Science...

NIMR Scientists Ranked Among Tanzania Top 50 by the AD Scientific Index 2026

The National Institute for Medical Research (NIMR) has once again demonstrated its leadership in scientific research with five of its distinguished scientists ranked among the Top 50 scientists in...

Decade-Long Research Led by NIMR Shapes Africa’s Push for Integrated HIV and NCD Care

New evidence from a decade of research led by Tanzania’s National Institute for Medical Research (NIMR) on integrated HIV and non-communicable disease (NCD) care is driving renewed efforts across...

Watumishi NIMR Wapatiwa Mafunzo ya Maadili ya Utumishi wa Umma, Rushwa Mahali pa Kazi na Afya ya Akili

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kujenga watumishi wenye weledi, uadilifu, uwajibikaji na afya njema kwa kuendesha mafunzo maalumu...

NIMR Researchers Shine with DZIF Early Career Scientists Grant

Researchers from the National Institute for Medical Research (NIMR), Mbeya Centre, have earned international recognition after five early career scientists were awarded the prestigious Deutsches...

NIMR Yasisitiza Tafiti Zinazotatua Changamoto za Afya Katika Maandalizi ya Bajeti ya 2026/2027

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said Aboud, ameitaka taasisi hiyo kuimarisha uwezo wake wa kifedha na kuwekeza katika tafiti zinazolenga kutatua...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.