NIMR

Kiwango cha ugonjwa wa usubi kwa watu wenye kifafa katika eneo la Mahenge, Wilaya ya Ulanga, Mkoa wa Morogoro, kimepungua hadi asilimia 22, huku maambukizi kwa ujumla yakipungua kwa takribani asilimia 40, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wa “Ubunifu wa Njia za Huduma za Kifafa Barani Afrika (EPInA)”.

Matokeo hayo yamewasilishwa katika mkutano wa siku mbili unaoendelea katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam, ukiwakutanisha wadau kutoka Wizara ya Afya, Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Taasisi mbalimbali za Serikali, pamoja na washirika wa maendeleo kutoka Uingereza, Kenya na Ghana. Lengo la mkutano huo ilikuwa ni kujadili matokeo ya utafiti uliofanyika Mahenge, mkoani Morogoro, na kuweka mikakati ya kuendeleza mapambano dhidi ya usubi na kifafa.

Akifungua mkutano huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekhalaghe, aliyemwakilisha Waziri wa Afya, Mhe. Mohammed Mchengerwa, amesema mafanikio hayo yanaonesha matokeo chanya ya ushirikiano kati ya Serikali, watafiti na jamii.

“Haya ni mafanikio makubwa ya jitihada za pamoja. Kupungua kwa kiwango cha maambukizi kwa asilimia 40 ni ishara kuwa tuko kwenye mwelekeo sahihi,” ameeleza Dkt. Shekhalaghe.

Aliongeza kuwa ili kutokomeza kabisa tatizo hilo, ni muhimu kuendelea na uimarishaji wa utoaji wa dawa hasa aina ya Ivermectin pamoja na kuongeza elimu kwa jamii.

“Niwaombe wananchi waendelee kushiriki kikamilifu katika matumizi ya dawa na kuamini wataalamu wa afya. Kifafa na usubi ni magonjwa yanayozuilika na kutibika,” alisisitiza.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Dkt. George PrayGod, Meneja wa Kituo cha Utafiti cha NIMR Muhimbili amesema utafiti huo umetoa takwimu muhimu zitakazosaidia kuboresha sera na miongozo ya utoaji wa huduma za afya.

“Takwimu hizi ni msingi muhimu wa maboresho ya sera na mikakati ya afya ya umma, hususan katika maeneo yenye maambukizi ya usubi na kifafa,” alisema.

Kwa upande wake, Mtafiti Kiongozi wa EPInA, Dkt. Bruno Mmbando, alisema tafiti zinaonesha uhusiano wa karibu kati ya usubi na kifafa, ambapo maeneo yenye maambukizi makubwa ya usubi pia huwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa kifafa.

“Mahenge bado ina changamoto kutokana na mazingira yake ya kijiografia yenye misitu inayochangia mazalia ya vimelea. Hata hivyo, tumeshuhudia mafanikio makubwa ukilinganisha na miaka ya nyuma,” alisema Dkt. Mmbando.

Alibainisha kuwa maeneo ya Tukuyu (Mbeya) na Amani (Tanga) tayari yameonesha mafanikio makubwa zaidi, jambo linalotoa matumaini kuwa tatizo hilo linaweza kudhibitiwa kikamilifu.

Naye mshirika wa mradi wa EPInA kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, Uingereza, Profesa Charles Newton, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kimataifa katika mapambano hayo.

“Kama tulivyoweza kupiga hatua kubwa katika kudhibiti malaria, tunaweza pia kupunguza kwa kiwango kikubwa kifafa kinachohusishwa na usubi endapo tutaendelea kushirikiana kisayansi na kimkakati,” alisema Profesa Newton.

Utafiti wa EPInA ulitekelezwa Mahenge kwa lengo la kuimarisha huduma za kifafa kupitia maboresho ya kinga, uchunguzi wa mapema, matibabu na kuongeza uelewa wa jamii, ikiwa ni sehemu ya jitihada za muda mrefu za kupunguza na hatimaye kutokomeza usubi na kifafa nchini. 

Section Title

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Kupitia Mafunzo ya Kitaaluma

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa kushiriki Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Chama cha...

NIMR Yaandaa Mpango wa Manunuzi 202627 kwa Lengo la Kuimarisha Ufanisi na Tija

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeandaa Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika manunuzi ya umma na kuhakikisha utekelezaji...

NIMR Yatoa Huduma za Afya Bure kwa Mamia, Yaadhimisha Mei Mosi 2026 kwa Vitendo

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa vitendo kwa kutoa huduma za afya bure kwa wananchi katika vituo mbalimbali nchini, hatua...

MFANYAKAZI HODARI WA NIMR 2026

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

WAFANYAKAZI HODARI 2026 NGAZI YA TAASISI

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo...

NIMR Launches Project to Strengthen Mpox Outbreak Prediction in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 30th April 2026, officially launched a new project aimed at strengthening Tanzania’s capacity to predict and respond to Mpox outbreak using...

Wanawake wa NIMR Mbeya Watoa Zawadi kwa Kliniki za Utafiti wa Afya Kusaidia Washiriki

Wanawake wa Kituo cha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Mbeya wametoa zawadi za mashuka kwa kliniki za utafiti zinazotumiwa na kituo hicho ili kusaidia washiriki wa tafiti...

NIMR Yafanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Yajadili Mpango Mkakati wa 2026–2031 na Bajeti ya 2026/2027

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 21 Aprili 2026, imefanya Mkutano wa 17 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma, ukiwa...

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.