NIMR

Baraza jipya la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) limepatiwa mafunzo ya uongozi na utawala bora siku tatu kuanzia tarehe 6 hadi 8 Oktoba 2025 na Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute). Mafunzo hayo yameandaliwa kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina na kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 6 hadi 8 Oktoba 2025.
Mafunzo haya yamelenga kuwaongezea wajumbe wa Baraza la Taasisi uelewa kuhusu majukumu yao katika kusimamia taasisi za umma kwa ufanisi, uwajibikaji na kwa kuzingatia misingi ya utawala bora na matumizi sahihi ya rasilimali za umma. Maeneo muhimu ambayo
washiriki pia walijifunza ni pamoja na mbinu za Kuimarisha ufanisi wa Baraza, utawala bora na utekelezaji wa majukumu ya Baraza ambapo walipata uelewa kuhusu dhana ya uongozi wenye matokeo na uhusiano kati ya Baraza na menejimenti.
Aidha wamejifunza kuhusu mikakati madhubuti ya kudhibiti vihatarishi ndani ya taasisi, uelewa wa mambo ya rasilimali fedha, ukaguzi, manunuzi ya umma na usimamizi wa rasilimali za umma na kuweka msisitizo katika matumizi bora ya kimkakati na yenye tija kwa manufaa ya wananchi.
Kupitia ushiriki wa NIMR, mafunzo haya yanatarajiwa kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Baraza likiwa na kazi muhimu ya kusimamia utekelezaji wa majukumu ya taasisi ili kuhakikisha matokeo ya tafiti yanachangia katika kuboresha sera, huduma za afya na ustawi wa jamii.

Section Title

NIMR Strengthens International Collaboration in Tuberculosis and Diabetes Mellitus Research at PROTID Annual General Meeting

The National Institute for Medical Research (NIMR) has continued to emphasize the importance of international collaboration in advancing research, training, and innovation aimed at addressing the...

NIMR Director General Honored for Outstanding Contributions to Advancing Medical Science, Research and Capacity Building

The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof. Said S. Aboud, has been honoured with the African Excellence and Personality Award (AEPA 2026) in Medical Science...

NIMR Scientists Ranked Among Tanzania Top 50 by the AD Scientific Index 2026

The National Institute for Medical Research (NIMR) has once again demonstrated its leadership in scientific research with five of its distinguished scientists ranked among the Top 50 scientists in...

Decade-Long Research Led by NIMR Shapes Africa’s Push for Integrated HIV and NCD Care

New evidence from a decade of research led by Tanzania’s National Institute for Medical Research (NIMR) on integrated HIV and non-communicable disease (NCD) care is driving renewed efforts across...

Watumishi NIMR Wapatiwa Mafunzo ya Maadili ya Utumishi wa Umma, Rushwa Mahali pa Kazi na Afya ya Akili

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kujenga watumishi wenye weledi, uadilifu, uwajibikaji na afya njema kwa kuendesha mafunzo maalumu...

NIMR Researchers Shine with DZIF Early Career Scientists Grant

Researchers from the National Institute for Medical Research (NIMR), Mbeya Centre, have earned international recognition after five early career scientists were awarded the prestigious Deutsches...

NIMR Yasisitiza Tafiti Zinazotatua Changamoto za Afya Katika Maandalizi ya Bajeti ya 2026/2027

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said Aboud, ameitaka taasisi hiyo kuimarisha uwezo wake wa kifedha na kuwekeza katika tafiti zinazolenga kutatua...

Mkurugenzi Mkuu NIMR Aridhishwa na Maendeleo ya Utafiti na Huduma Kituo Kidogo cha Gonja.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said S. Aboud, ameridhishwa na maendeleo ya shughuli za utafiti na utoaji wa huduma za maabara yanayoendelea...

Wanawake wa NIMR Mbeya Waadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake kwa Matendo ya Huruma na Elimu ya Uwiano wa Majukumu ya Kazi na Familia.

Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, tarehe 08 Machi, wanawake wa Taasisi ya Taifa ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Kituo cha Mbeya walionyesha mshikamano na kujitolea kwa jamii...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.