NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke. Mafunzo hayo ya siku tatu, yaliyofanyika kuanzia tarehe 26 hadi 28 Novemba 2025, yalilenga kuwajengea uwezo washiriki katika kubuni, kuandaa na kuwasilisha mapendekezo bora ya tafiti za kisayansi.
Katika mafunzo hayo, washiriki walipata fursa ya kufanya mazoezi kwa vitendo kuhusu hatua muhimu za uandishi wa andiko la utafiti, ikiwemo kuandaa mapendekezo yenye ubora, kuimarisha uwezo wa uandishi wa kisayansi, kuelewa na kutekeleza maadili ya utafiti, pamoja na kubadilisha mawazo ya kitaalamu na kuwa tafiti zenye matokeo chanya na zinazoweza kupata ufadhili.
Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mkurugenzi wa Kukuza na Kuratibu Tafiti NIMR (DRCP) Dkt. Nyanda E. Ntinginya, ameushukuru uongozi wa Hospitali ya Temeke kwa kuthamini umuhimu wa mafunzo hayo na kuhakikisha ushiriki mpana wa watumishi wake. Amesisitiza kuwa ujuzi walioupata washiriki unapaswa kutumika kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa kuanzisha, kuendesha na kuchapisha tafiti zenye manufaa kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
Dkt. Nyanda pia alibainisha kuwa NIMR itaendelea kuimarisha ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Temeke katika kukuza uwezo wa watumishi, kuendeleza tafiti za pamoja na kuhamasisha matumizi ya ushahidi wa kisayansi katika kuboresha huduma za afya nchini.
Mafunzo hayo yanaibua matumaini mapya kwa watumishi wa afya Temeke, huku yakitarajiwa kuongeza ubunifu, ushindani na tija katika uandaaji wa tafiti zenye mchango mkubwa katika mfumo wa afya wa Tanzania.

Section Title

NIMR Emerges as a Global and Regional Leader in EDCTP-Supported Health Research

The National Institute for Medical Research (NIMR) in Tanzania, has been recognized as a leading contributor to internationally competitive health research following its strong performance in...

NIMR Yaongoza Mdahalo wa Sera Kuhakikisha Ushahidi wa Kisayansi Unatumika Kukabili Milipuko ya Magonjwa

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo, tarehe 8 Januari 2026, imeendesha mkutano wa majadiliano ya sera uliowakutanisha watafiti, watunga sera, watoa maamuzi wa sekta ya afya...

NIMR Unveils Genomic Evidence Showing Predominance of Bacterial Pathogens in Acute Respiratory Infections in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR) disseminated on 22nd December 2025 research findings from the project titled Genomic characterization of Acute Respiratory Infections (ARI) Pathogens...

Beyond Clinical Surveillance: Wastewater and Environmental Monitoring Reveal Hotspots of Antimicrobial-Resistant “Superbugs”

A recent study presented at the 7th Africa Continental World Antimicrobial Awareness Week (WAAW) event has unveiled the “environmental resistome” in Tanzania. Using advanced genomic tools to analyse...

NIMR Disseminates Impactful Research Findings at the 7th Africa Continental World AMR Awareness Week

In a milestone event for the continent, Tanzania hosted the 7th Africa Continental World Antimicrobial Resistance (AMR) Awareness Week (WAAW) at the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam from 2nd to...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi wa Afya Temeke Kuandika Andiko la Utafiti ili Kuboresha Huduma za Afya za Jamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya...

NIMR Conducts Institutional Review Boards Training to Elevate Clinical Trial Standards Nationwide

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched a specialized training program to members and secretariats of Institutional Review Boards (IRBs), aimed at strengthening national...

𝗡𝗜𝗠𝗥 Conducts Capacity Building Training for Clinical Trials Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR), in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), on 24th November 2025 conducted a specialized capacity-building...

NIMR na Wadau wa Afya Wafanya Mkutano wa Uzinduzi wa Utekelezaji wa Tafiti zilizo chini ya Mradi wa TAKeOFF wa Kupambana na Ugonjwa wa Mabusha na Matende

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.