NIMR Yaanza Utekelezaji wa Utafiti wa Majaribio ya Dawa Kutokomeza Maambukizi ya Ugonjwa wa Matende na Mabusha Lindi na Mtwara
Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeanza rasmi utekelezaji wa utafiti wa majaribio ya tiba ya kuharakisha kutokomeza maambukizi ya ugonjwa wa matende na mabusha. Hayo yamebainishwa wakati wa kuendesha mafunzo ya siku mbili ya kutekeleza utafiti kwa watafiti na watoa huduma wa afya kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara.Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, yalifunguliwa rasmi na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Mwinjuma M. Mkungu. Katika hotuba yake, aliipongeza NIMR kwa kuwa kinara wa tafiti za afya nchini na kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya katika kuandaa tafiti zenye lengo la kumaliza kabisa magonjwa yanayosumbua jamii, hususani yale yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (NTDs).“NIMR ni nguzo muhimu katika sekta ya afya kwa kuwa inatoa ushahidi wa kisayansi unaosaidia kupanga na kutekeleza afua bora. Mafunzo haya ni sehemu ya juhudi hizo,” alisema Mhe. Mkungu.Mafunzo hayo yamefuatiwa na kuanza kwa uchukuaji wa sampuli kwa washiriki wa utafiti katika kijiji cha Ruaha, kata ya Mnazi Mmoja, Wilaya ya Lindi. Utafiti huu wa kisayansi unalenga kulinganisha tiba tofauti za magonjwa ya matende na mabusha, hususani dawa ya “Doxycycline” na “Moxidectin + Albendazole”, dhidi ya Kingatiba iliyopo sasa ya “Ivermectin + Albendazole”.Mtafiti Mkuu wa mradi wa utafiti kutoka NIMR, Dkt. Akili Kalinga, alisema kuwa tafiti hizi zinalenga kutafuta tiba mbadala na bora zaidi ambazo zitaweza kuharakisha kutokomeza ugonjwa huo nchini. “Tumekuwa kwenye mapambano dhidi ya matende na mabusha kwa miaka mingi. Tunategemea kuwa utafiti huu utasaidia kuondoa kabisa vikwazo vinavyosababisha maambukizi ya Ugonjwa huu kuendelea katika baadhi ya maeneo.” alisema Dkt. Kalinga.Akizungumza wakati wa zoezi la uchukuaji wa sampuli, Mwenyekiti wa Kijiji cha Ruaha, Bi. Salima Kidamchong`we, alisema kuwa utafiti huo ni muhimu sana kwa jamii yao kwa sababu unawapa fursa ya kujua hali yao ya kiafya. “Tunatoa shukrani kwa NIMR na Wizara ya Afya kwa kutuletea utafiti huu. Ni jambo la maana na lenye manufaa kwa wananchi wetu,” alisema.Naye mmoja wa washiriki wa utafiti kutoka kijiji cha Ruaha kata ya Mnazi Mmoja, Bw. Ali Bakari Natulama, aliipongeza NIMR kwa juhudi zake na kusema kwamba tafiti kama hizi zinasaidia sana katika kuelimisha jamii na kuwakinga na magonjwa hatari kama matende na mabusha.Kwa sasa, ugonjwa wa matende na mabusha bado upo katika baadhi ya Halmashauri za wilaya nchini Tanzania ikiwemo Lindi Manispaa, Mtama, Mikindani, Kinondoni na Pangani. Licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa Halmashauri 114 kutokomeza maambukizi ya Ugonjwa na kusitisha ugawaji wa kingatiba uliofanyika kwa miaka mingi.NIMR inatarajia kutumia matokeo ya utafiti huu kuboresha miongozo ya kitaifa na kidunia ya tiba na udhibiti wa magonjwa haya, kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya na wadau wengine. Section Title NIMR Yaanza Utekelezaji wa Utafiti wa Majaribio ya Dawa Kutokomeza Maambukizi ya Ugonjwa wa Matende na Mabusha Lindi na Mtwara ByErick Mboma July 16, 2025 Uncategorized aasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendesha mafunzo maalumu kwa watafiti vijana 13 kuhusu namna ya kuandaa maandiko ya tafiti za afya kwa madhumuni ya kuvutia washirika wa… Read More NIMR Yawanoa Watafiti Vijana Kuandika Maandiko ya Tafiti za Afya Yanayoweza Kushindana Kimataifa ByErick Mboma July 1, 2025 Uncategorized aasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendesha mafunzo maalumu kwa watafiti vijana 13 kuhusu namna ya kuandaa maandiko ya tafiti za afya kwa madhumuni ya kuvutia washirika wa… Read More NIMR Amani Centre Passes OECD GLP Surveillance Inspection, Reaffirms Position as Leading Public Test Facility in East Africa ByErick Mboma June 30, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR) Amani Research Centre has completed a rigorous annual surveillance and inspection by the South African National Accreditation System (SANAS)… Read More Kamishna Jenerali wa DCEA Aipongeza NIMR kwa Kuunga Mkono Juhudi za Serikali za Kupiga Vita Dawa za Kulevya ByErick Mboma June 27, 2025 Uncategorized Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Bw. Aretas Lyimo ameipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa kuunga mkono mapambano… Read More NIMR Advocates for Broader One Health Strategy at Regional Health Conference in Juba ByErick Mboma June 26, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR) has called for a bold expansion of the One Health approach to address both communicable and non communicable diseases (NCDs) in Africa during the… Read More Mkurugenzi Mkuu NIMR Atoa Wito wa Uadilifu kwa Watumishi wa Umma ByErick Mboma June 23, 2025 Uncategorized Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. Said Aboud, amewapongeza watumishi wa NIMR kwa kufanya kazi kwa bidii, weledi, uwajibikaji na uadilifu. Vilevile… Read More NIMR Yadhamiria Kuiboresha Tabora kuwa Kitovu cha Utafiti wa Afya Kanda ya Magharibi Mwa Tanzania ByErick Mboma June 22, 2025 Uncategorized Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. Said Aboud, tarehe 21 Juni 2025, amefanya ziara ya kikazi katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Tabora, kwa lengo la… Read More Eswatini Delegation Commends NIMR Ethical Oversight in Health Research ByErick Mboma June 21, 2025 Uncategorized A delegation from the Eswatini Health and Human Research Review Board (EHHRB) has commended National Institute for Medical Research (NIMR) for its robust ethical review and approval systems in health… Read More NIMR Conducts Capacity Building Training on Knowledge Translation for Health Researchers ByErick Mboma June 21, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR) successfully conducted a three-day training workshop on knowledge translation from 11th to 13th June 2025, at its Headquarters Sub-office in Dar es… Read More










