NIMR

Erick Mboma

Eswatini Delegation Commends NIMR Ethical Oversight in Health Research

A delegation from the Eswatini Health and Human Research Review Board (EHHRB) has commended National Institute for Medical Research (NIMR) for its robust ethical review and approval systems in health research regulation. The commendation was made during a visit to NIMR Sub-office in Dar es Salaam. The visit which began on Monday 16th June 2025, was undertaken following a recommendation by the World Health Organization (WHO), which recognized Tanzania as a model country with well-established mechanisms in research ethics that other nations can learn from. The EHHRB team was led by Mr. Rudolph Maziya, Chairperson of the Board, and Ms. Babazile Hazel Shongwe, Executive Secretary. The primary objective of the visit was to learn about Tanzania’s ethical and regulatory framework, especially that managed by NIMR. The delegation was officially received by the Director General of NIMR, Prof. Said S. Aboud, who gave an overview of the Institute’s mandate in promoting, coordinating, and regulating health research in Tanzania. Also in attendance were Dr. Mary Mayige, the Director of Research Information and Regulatory Affairs, Dr. Obadia Bishoge, Head of the Health Research Regulation Section, and members of the National Health Research Ethics Committee (NatHREC) Secretariat. During the visit, the team was briefed on Tanzania’s health research regulatory framework, including the National Health Research Ethics Committee (NatHREC) protocol review process and the operation of the National Research Ethics Information Management System (NREIMS). NREIMS is a digital platform that enables researchers to submit proposals for ethical review by NatHREC and Institutional Review Boards (IRBs) across the country. The Eswatini delegation expressed admiration for the efficiency and success of NREIMS, describing it as a transformative tool that has streamlined ethical review processes and improved accountability in research oversight. They expressed strong interest in adopting a similar system in Eswatini to enhance their own research governance. Beyond the technical engagement, the visitors also acknowledged the warmth and professionalism extended to them by NIMR staff throughout their visit. They praised Tanzania’s leadership in health research regulation and emphasized the value of continued collaboration between the two institutions. During winding up of the visit, Prof. Aboud thanked the delegates for their visit and reaffirmed NIMR commitment to supporting regional partnerships and promoting excellence in ethical oversight across the continent.

Eswatini Delegation Commends NIMR Ethical Oversight in Health Research Read More »

NIMR Conducts Capacity Building Training on Knowledge Translation for Health Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR) successfully conducted a three-day training workshop on knowledge translation from 11th to 13th June 2025, at its Headquarters Sub-office in Dar es Salaam. The workshop brought together 19 research scientists from NIMR Muhimbili, Mbeya, Tanga, Mabibo, and Dodoma Centres, along with participants from the Zanzibar Health Research Institute (ZAHRI). The primary objective of the training was to strengthen researchers’ capacity to translate scientific knowledge into practical policy tools. The training workshop focused on the development of policy briefs and explored effective strategies for packaging and communicating research evidence to support evidence-informed decision-making and policy formulation in Tanzania. The training was officially opened by the Director for Research Coordination and Promotion, Dr. Nyanda Elias Ntinginya, on behalf of the Director General of NIMR, Prof. Said Aboud. In opening remarks, Dr. Ntinginya encouraged researchers to embrace policy brief development as a critical outcome of their research work and reminded them that producing policy briefs is among the key criteria for career advancement at NIMR. The training covered several thematic areas including identifying communication gaps between researchers and policy makers, defining health-related problems based on Tanzania’s National Health Research Agenda, using systematic reviews as a tool for evidence synthesis, and understanding the structure and content of effective policy briefs. Additionally, participants learned on how to present their research findings through various dissemination platforms such as policy dialogue meetings. By the end of the workshop, participants had developed a total of 19 policy briefs, each addressing specific health issues that are aligned with national priorities. Facilitation was provided by experts from NIMR including Dr. Elizabeth H. Shayo, Mr. Emanuel Makundi, Ms. Stella Kilima, and Dr. Marywinne Nanyaro. Workshop participants expressed appreciation to the NIMR Management for moral and financial support, which was instrumental in ensuring the successful delivery of the training. This training is part of NIMR ongoing efforts to bridge the gap between research and policy, reinforcing the role of scientific evidence in shaping public health interventions and national development.

NIMR Conducts Capacity Building Training on Knowledge Translation for Health Researchers Read More »

Waziri Simbachawene Aipongeza NIMR kwa Kufanya Utafiti wa Afya Unaogusa Jamii

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mheshimiwa George Simbachawene, ameipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa mchango wake mkubwa katika kufanya tafiti zinazogusa maisha ya Watanzania na kutoa bidhaa halisi zitokanazo na tafiti hizo, zenye lengo la kutatua changamoto mbalimbali za kiafya.Mheshimiwa Simbachawene ametoa pongezi hizo leo alipotembelea banda la NIMR katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. NIMR inashiriki katika maadhimisho hayo kwa kuonesha kazi zake za utafiti, ikiwemo bidhaa za tiba asili pamoja na kutoa elimu kuhusu taratibu za kupata vibali vya kufanya tafiti za afya nchini.Aidha Mhe. Simbachawene amesema kuwa ni jambo la kupongezwa kuona taasisi ya utafiti kama NIMR ikionesha bidhaa halisi zilizotokana na tafiti zake. Aliitaka NIMR kuhakikisha bidhaa hizo za tiba zinawafikia wananchi kwa kuzisambaza katika maduka makubwa ya dawa (pharmacy) katika kila mkoa.“Imekuwa ni fursa nzuri kwa kuweka bidhaa hizi hadharani. Ninyi mnafanya tafiti na tafiti ndiyo zinawapa uhalali kuliko wengine. NIMR ni chombo cha taifa kwa ajili ya kuhakikisha ubora na usalama wa huduma hizi. Onenekaneni masokoni, zinapopatikana huduma hizi kama kwenye pharmacy kubwa kubwa kila mkoa. Ni jambo jepesi, mkifanya hivyo, sisi wananchi tutanunua tu,” amesema Mheshimiwa Simbachawene.Kwa upande wake, Dkt. Akili Kalinga, Mtafiti Mkuu kutoka NIMR, amemshukuru Waziri kwa kutembelea banda la taasisi na kueleza kuwa NIMR imeendelea kufanya tafiti katika maeneo mbalimbali ya afya yakiwemo magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza, tiba asili, afya ya uzazi, lishe na mengineyo yenye lengo la kuboresha ustawi wa jamii.Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma hufanyika kila mwaka kuanzia Juni 16, na kuhitimishwa Juni 23. Husherehekewa na Wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kwa lengo la kutambua mchango wa Watumishi hao katika nchi zao. Maadhimisho huambatana na maonesho mbalimbali.

Waziri Simbachawene Aipongeza NIMR kwa Kufanya Utafiti wa Afya Unaogusa Jamii Read More »

NIMR Participates in International Steering Committee and Consortium Meeting at the UCL

The National Institute for Medical Research (NIMR), on 10th June 2025, participated in the annual scientific meeting of the RESPOND AFRICA partnership held at the University College London (UCL), Liverpool Campus. The meeting brought together international researchers, health professionals and policymakers to discuss progress and innovations in integrated care for chronic conditions such as HIV, diabetes and hypertension in sub-Saharan Africa.The NIMR team was led by Prof. Said Aboud, Director General of NIMR, along with Prof. Sayoki G. Mfinanga, Principal Investigator of RESPOND AFRICA project in Tanzania and Dr. Sokoine Kivuyo who is a senior researcher from NIMR Muhimbili Centre. The team actively participated in high-level discussions on strategies to improve chronic disease management through scalable, integrated healthcare system.During the meeting, NIMR researchers presented key findings from the ongoing META trial which investigates the use of metformin to prevent diabetes in people living with HIV. NIMR also shared progress from other related projects namely INTE-COMM which compares community-based integrated care with standard clinic-based services; MOCCA, which explores strategies to optimize long-term care for chronic diseases; and INTE AFRICA, a flagship initiative that has demonstrated the feasibility, efficiency, and scalability of integrated chronic disease services by combining HIV, diabetes, and hypertension care into a unified primary healthcare system.Through these interactive discussions, NIMR researchers highlighted how Tanzania is taking a leadership role in designing and implementing integrated health services that can serve as a model to other African countries. Prof. Aboud emphasized the importance of findings generated from research studies informing on policy change, formulation, best practices and ultimately improving healthcare system in the country and globally while Prof. Mfinanga and Dr. Kivuyo shared Tanzania’s experience in research management, data collection and long-term follow-up of participants in the trials. Prof Aboud further commented on the strengthened regulatory environment through utilisation of National Research Information Management System (NREIMS) and integration with other systems.NIMR participation in the meeting which began on 10th June 2025 and is expected to end on 12th June 2025, reflects the Institute commitment to advancing scientific research that improves public health in Tanzania and globally.

NIMR Participates in International Steering Committee and Consortium Meeting at the UCL Read More »

NIMR Yagusa Maisha ya Wafungwa na Wanafunzi wa Shule ya Viziwi Dodoma kwa Msaada wa Kijamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imefanya ziara ya kijamii tarehe 6 Mei 2025 katika Gereza Kuu la Isanga na Shule ya Viziwi Dodoma, ambapo imetoa msaada wa vitu mbalimbali kwa ajili ya kuwafariji na kusaidia makundi yenye uhitaji katika jamii.Msaada huo ulijumuisha magodoro, shuka, dawa za meno, sabuni za kuogea, mafuta ya kupaka, vyakula kama mchele, unga wa ugali, maharage, mahindi, nyama, sukari, mafuta ya kupikia, mikate, unga wa lishe na maziwa ya kopo.Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Meneja wa Rasilimali Watu na Utawala, Bi. Bupe Ndelwa, alieleza kuwa Taasisi inaguswa na hali ya makundi hayo maalumu na kuona umuhimu wa kuwafariji na kuwaonesha 0upendo. Alisisitiza kuwa NIMR kama sehemu ya jamii iliona ni vyema kutumia kidogo walichokuwa nacho kuwafikia ndugu zao ili wasijihisi wametengwa na jamii na kuwatia moyo kuwa wapo pamoja nao na wanawapenda.Mkuu wa Gereza la Isanga, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Zephania Neligwa, aliishukuru NIMR kwa moyo wa huruma waliouonesha na kusisitiza umuhimu wa Taasisi na watu binafsi kuwa na utamaduni wa kusaidia makundi yenye uhitaji. Alisema, “Nawapongeza NIMR kwa hatua hii ya kugusa maisha ya wahitaji. Msaada huu si tu unaleta faraja kwa wafungwa, bali pia unaakisi uzalendo na upendo kwa jamii. Msipate hofu ya kutembelea magereza, ni sehemu rafiki, tunawakaribisha kuwatembelea ndugu zetu”.Kwa upande wake, Mkuu wa Gereza la Isanga, Sehemu ya Wanawake, Mrakibu wa Magereza Sifa Anyimike, alisema misaada kama hiyo husaidia kupunguza gharama kwa Serikali katika uendeshaji wa magereza na kuhakikisha mahitaji ya msingi ya wafungwa yanatimizwa.Baada ya ziara hiyo gerezani, NIMR pia ilitembelea Shule ya Viziwi Dodoma na kutoa msaada wa vyakula na mahitaji mengine kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia. Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Bw. Awadhi Mbogo, aliipongeza NIMR kwa kujitoa kwao na kuwataka kuendeleza moyo huo wa kutoa pale inapohitajika. “Hili ni tendo la kiutu ambalo limewagusa sana watoto wetu, huku hatufikiwi mara kwa mara, lakini NIMR mmefanya jitihada za kutufikia. Tunawashukuru kwa upendo wenu na tunawaombea muendelee kuwa na moyo wa huruma kwa jamii.” Alisema Mbogo.Misaada hiyo ni sehemu ya juhudi za taasisi kurudisha kwa jamii na kuonyesha mshikamano na upendo kwa makundi maalumu.

NIMR Yagusa Maisha ya Wafungwa na Wanafunzi wa Shule ya Viziwi Dodoma kwa Msaada wa Kijamii Read More »

NIMR Yapongezwa kwa Kufufua Kituo cha Utafiti Gonja

Katika kuimarisha ushirikiano na jamii, Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) tarehe 29/05/2025 imekutana na timu ya viongozi kutoka kata mbili zinazozunguka kituo cha utafiti cha NIMR Gonja.Ujumbe huo ulioongozwa na Mheshimiwa Issa Jasper Rashid, Diwani wa Kata ya Maore, ulihusisha Mtendaji wa Kata, Wenyeviti wa Vijiji, Watendaji na Wenyeviti wa Vitongoji 11. Viongozi hao walitembelea kituo cha NIMR Gonja na kujionea maendeleo makubwa ya ufufuaji wa kituo hicho.Wameipongeza NIMR kwa hatua hiyo muhimu na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano katika shughuli za utafiti sanjari na kuwa mabalozi wa kuelimisha jamii juu ya shughuli zitakazotekelezwa kituoni hapo.Mkuu wa kituo cha NIMR Gonja, Bw. Said Frank Magogo, aliwashukuru viongozi hao kwa kutambua umuhimu wa kutembelea kituo hicho, akibainisha kuwa wao kama wawakilishi wa wananchi ni wadau muhimu wa Taasisi. Alisisitiza kuwa ushirikiano wa karibu kati ya NIMR na jamii unachagiza mafanikio ya Taasisi katika kutekeleza jukumu lake kuu la kufanya tafiti mbalimbali kwa lengo la kuboresha afya ya Watanzania.Akijibu maombi ya viongozi hao waliotaka tafiti zaidi zifanyike juu ya magonjwa kama homa ya ini ambayo imeisumbua jamii hiyo kwa muda mrefu, Bw. Magogo alieleza kuwa ushirikiano wa karibu na jamii huchangia kwa kiasi kikubwa katika kuibua maeneo mapya ya kufanya tafiti za afya. Aliahidi kuwa NIMR itaendelea kushirikiana na wananchi ili kuhakikisha utafiti unagusa mahitaji halisi ya jamii.

NIMR Yapongezwa kwa Kufufua Kituo cha Utafiti Gonja Read More »

NIMR Yaketi Kuandaa Mpango wa Manunuzi wa Mwaka 2025/26

Wataalamu kutoka idara mbalimbali za Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), wakiongozwa na Idara ya Manunuzi na Ugavi wamekutana kuandaa Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2025/26 kwa lengo la kuongeza ufanisi na tija katika Taasisi.   Akizungumza leo tarehe 29 Mei 2025 alipotembelea timu ya washiriki wa kuandaa mpango huo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud amesisitiza umuhimu wa kuwa na Mpango wa Manunuzi wa Mwaka ulioandaliwa kwa ushirikishwaji wa idara tumizi na umakini mkubwa ili kuweza kuutekeleza kwa wakati na kufikia malengo ya Taasisi. Amewakumbusha washiriki kuandaa mpango wenye uhalisia, kuzingatia sheria ya manunuzi ya umma na kanuni zake na kuchakata maombi kupitia mfumo wa NeST. “Mpango wa manunuzi wa mwaka ukiandaliwa na kutekelezwa vizuri unawezesha Taasisi kufikia malengo yake ya mwaka kwa wakati,” amesema, Prof. Aboud huku akiwapongeza watumishi kwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii, kuwajibika, uadilifu na weledi.   Mkutano huo wa kuandaa Mpango wa Manunuzi wa Mwaka unaofanyika mjini Morogro ulianza tarehe 26 na unatarajia kumalizika 30/05/2025 ambapo umewakutanisha maafisa manunuzi, bajeti, TEHAMA, watafiti wanasayansi, Meneja wa Manunuzi na Ugavi, Meneja wa Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Makao Makuu, Kituo cha Muhimbili, Tanga, Amani, Korogwe, Mbeya na Mwanza na Mbeya.  

NIMR Yaketi Kuandaa Mpango wa Manunuzi wa Mwaka 2025/26 Read More »

NIMR Leads Launch of BREEDIME Workshop to Strengthen Health Emergency Data Management in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR) on 20th May 2025 organized a workshop that focused on health data management and the sharing of research materials during public health emergencies. The workshop was officiated by Dr. Loishooki Saitore Laizer, Director of Human Resources Development at the Ministry of Health representing the Chief Medical Officer Dr. Grace Magembe. Dr. Laizer emphasized the need for strong collaboration among researchers in responding to emerging and re-emerging diseases and health outbreaks. “The BREEDIME project will help us build regulatory capacity that enables Tanzania to collect, utilize, and share research data that informs evidence-based policy making and accelerates decision-making processes both during normal times and in public health emergencies,” said Dr. Laizer. He further emphasized that “Globally, data use and sharing have become crucial in addressing health challenges through the contribution of information to international databases. I urge all participants to remain committed to our national values, safeguard research participants and promote inclusive and transparent collaboration with both local and international stakeholders.” Dr. Nyanda Ntinginya, NIMR Director of Research Coordination and Promotion representing NIMR Director General explained that the BREEDIME project began in June 2023 and it is structured around eight work packages that are implemented by various partner institutions. “The project partners include TMDA, NIMR, MUHAS, KCRI, ZAHRI, ZFDA, and Rwanda FDA, along with international collaborators namely University of St. Andrews (UK) and the Karolinska Institute (Sweden). NIMR is leading Work Package 3 which focuses on health data management during emergency periods,” said Dr. Nyanda. He added that through BREEDIME, Tanzania is building national capacity to respond effectively to public health emergencies by strengthening clinical trial regulatory systems and establishing a research ethics framework for the storage, access, and sharing of health data and materials within and beyond national borders. Dr. Nyanda also expressed deep appreciation to the Ministry of Health and the Government of Tanzania for their continued support in advancing scientific research, and extended sincere gratitude to EDCTP for providing the financial support to implement the project. Also in attendance was Dr. Elisha Osati, Chairperson of the National Health Research Ethics Committee (NatHREC), along with other key stakeholders including clinical researchers, regulatory officials, laboratory scientists, epidemiologists, and statisticians from both public and private institutions across Tanzania Mainland and Zanzibar. The workshop held in Morogoro, was organized under the BREEDIME project (Building Resilient Research Ethics, Diagnostics and Medicines Regulatory Capacity during Routine and Public Health Emergency Periods) aims to strengthen ethical research systems, diagnostic capacities, and medicines regulation to better manage both routine and emergency public health situations

NIMR Leads Launch of BREEDIME Workshop to Strengthen Health Emergency Data Management in Tanzania Read More »

NIMR Yawasilisha Matokeo ya Utafiti wa Tathmini ya Maambukizi ya Ugonjwa wa Usubi Katika Eneo la Tukuyu

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya imefanya mkutano tarehe 21 Mei 2025 kwa ajili ya kuwasilisha matokeo ya utafiti wa tathmini ya maambukizi ya ugonjwa wa Usubi katika eneo la Tukuyu. Eneo hilo linajumuisha halmashauri za wilaya ya Kyela, Busokelo, Rungwe, Ileje na Ludewa.Mkutano huo wa siku moja umefanyika katika Wilaya ya Kyela na kuwahusisha viongozi wa Serikali za Mitaa, wataalamu wa afya, wawakilishi wa Wizara ya Afya na watafiti kutoka NIMR.Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Mhe. Katule Kingamkono ambaye alikuwa mgeni rasmi ameipongeza NIMR na Wizara ya Afya kwa juhudi kubwa walizofanya katika kupambana na ugonjwa wa Usubi kwa zaidi ya miaka 20.Amesema kuwa hatua ya kusitisha umezeshaji wa dawa kwa wananchi ni ishara ya mafanikio makubwa baada ya kushuka kwa kiwango cha maambukizi. “Tunaishukuru NIMR kwa kuendelea na tathmini ya kina ili kupata majibu ya uhakika yatakayowezesha kutangaza rasmi kutokomezwa kwa ugonjwa wa Usubi katika eneo hili” amesema Mhe. Kingamkono.Aidha, ametoa wito kwa madiwani, maafisa tarafa, watendaji wa kata na vijiji, wenyeviti wa vijiji, wahudumu wa afya na wadau wengine kushirikiana kikamilifu na wataalamu wa afya wakati wa utekelezaji wa tathmini ya mwisho ya maambukizi ya ugonjwa huo.Kwa upande wake, Mtafiti Mkuu kutoka NIMR, Dkt. Akili Kalinga, amesema kuwa lengo la mkutano huo ni kuwafahamisha wananchi kuhusu maendeleo ya utafiti wa tathmini ya maambukizi ya Usubi baada ya kusitishwa kwa umezeshaji wa dawa za kingatiba uliodumu kwa miaka 21.“Tathmini ya awali ilionesha kuwa maambukizi yameshuka hadi kufikia kiwango cha chini karibu na asilimia 0.01 – kiwango kinachopendekezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa ajili ya kutangaza kutokomezwa kwa ugonjwa,” amesema Dkt. Kalinga. Aliongeza kuwa tathmini ya mwisho itakayofanyika sasa itaelekeza kama ni lazima kuendelea na ugawaji wa dawa au kutangaza rasmi kuwa ugonjwa huo umetokomezwa katika eneo la Tukuyu.Akizungumza kwa niaba ya Meneja wa Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele Bi. Toyi V. Midaba kutoka Wizara ya Afya amesema kuwa Wizara imeandaa mikakati maalum ya kufuatilia magonjwa kama Usubi ambayo awali hayakuwa yanapewa uzito ili kuhakikisha yanatokomezwa kabisa.Naye Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Ushirika, Andendekisye Jeremia Mwakalinga, ameishukuru NIMR kwa kutoa elimu na kushirikisha jamii katika matokeo ya utafiti huo. Amesema taarifa hizo zitasaidia kuwapa matumaini wananchi walioteseka na ugonjwa huo kwa miaka mingi.Mkutano huo umehudhuriwa na madiwani wa Halmashauri za Kyela na Ileje, waganga wakuu wa wilaya, maafisa wa Mpango wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, watafiti wa NIMR, wataalamu wa afya, maafisa elimu, maafisa tarafa, watendaji wa kata, wenyeviti wa vijiji na watendaji wa vijiji kutoka wilaya ya Kyela na Ileje.

NIMR Yawasilisha Matokeo ya Utafiti wa Tathmini ya Maambukizi ya Ugonjwa wa Usubi Katika Eneo la Tukuyu Read More »

Baraza Kuu la Wafanyakazi wa NIMR la 16 Lakutana Jijini Dar es Salaam

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo tarehe 12 Mei, 2025 imefanya kikao chake cha 16 cha Baraza Kuu la Wafanyakazi katika ukumbi wa CEEMI, ofisi ndogo za taasisi zilizopo jijini Dar es Salaam. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Profesa Said Aboud ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo, amewataka wafanyakazi kuwajibika ipasavyo kwa kuzingatia bajeti na mpango kazi wa Taasisi, maadili ya kazi, kutunza mali za umma na kuepuka matumizi yasiyo ya lazima yanayoongeza gharama za uendeshaji. Prof. Aboud amewakumbusha wajumbe kuwa Baraza ni jukwaa muhimu linalowezesha mashirikiano kati ya menejimenti, Chama cha Wafanyakazi na Wafanyakazi wenyewe kwa lengo la kuboresha mazingira ya kazi na utendaji wa Taasisi. Vilevile Prof. Aboud amesema kuwa Taasisi itaendelea kuweka vipaumbele katika tafiti za magonjwa yasiyoambukiza kama Saratani na Afya ya akili, magonjwa ya kuambukiza ikiwemo ya milipuko, Usugu wa vimelea dhidi ya dawa, Tiba Asili na Tiba Mbadala na matumizi ya matokeo ya tafiti hizo katika kuboresha sera, kufanya maamuzi kwa kutumia ushahidi wa kisayansi na hatimaye kuboresha huduma kwa wananchi. Hali kadhalika, Taasisi itaendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato toka vyanzo vyake vya ndani na matumizi ya TEHAMA ili kuongeza ufanisi na tija katika Taasisi na kuendelea kuchangia katika mfuko mkuu wa Serikali. Ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuupa kipaumbele utafiti wa kisayansi. Naye katibu wa Chama cha Wafanyakazi RAAWU Bwa. Joseph Sayo Mwita   akizungumza katika kikao hicho amewataka wafanyakazi kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za kazi ili kutimiza malengo ya Taasisi. Aidha, kikao hicho kilijadili na kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 yaliyotayarishwa kwa kuzingatia Mpango Mkakati wa sita wa taasisi na Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020–2025. Kikao hicho pia kimefanya uchaguzi wa Katibu na Naibu Katibu wa Baraza, Uchaguzi wa Wajumbe wa Kamati Tendaji ya Baraza Kuu la Wafanyakazi sambamba na kuhuishwa kwa Mkataba Mpya wa Baraza kwa kipindi cha mwaka 2025 hadi 2028. Kikao hicho kimehudhuriwa na wajumbe kutoka vituo vinane vya utafiti vya NIMR nchini, pamoja na wawakilishi kutoka Ofisi ya Kamishna wa Kazi na chama cha wafanyakazi wa RAAWU Kanda ya Mashariki.

Baraza Kuu la Wafanyakazi wa NIMR la 16 Lakutana Jijini Dar es Salaam Read More »