NIMR Yapongezwa kwa Mchango Mkubwa Katika Kukuza Tiba Asili
Wananchi wanaendelea kunufaika na huduma za tiba asili kupitia tafiti, na uanzishwaji wa kiwanda cha kuzalisha dawa za tiba asili cha NIMR Mabibo kufuatia juhudi kubwa za Serikali kuhakikisha dawa salama na zenye ubora zinapatikana kwa wingi nchini.Akizungumza tarehe 29 Agosti, 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Tiba Asili ya Mwafrika yaliyofanyika jijini Dodoma, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu, ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, aliipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa hatua kubwa zilizopigwa katika tafiti na uhamasishaji wa matumizi ya dawa za tiba asili. Dkt. Kazungu alisema moja ya mafanikio makubwa ya NIMR ni uanzishwaji wa kiwanda cha Mabibo cha kuzalisha dawa za tiba asili ambacho kinatumia malighafi kutoka kwa wakulima wa miti dawa. “Kiwanda hiki hakijaishia tu kuzalisha dawa salama na zenye ufanisi na ubora, bali pia kimetoa fursa za ajira kwa wananchi na kuongeza kipato kwa wakulima wa malighafi hizo,” alisisitiza Dkt Kazungu.Aidha, alitembelea banda la NIMR katika maonesho na kupongeza jitihada zilizofanywa huku akishauri kuimarisha tafiti zinazohusu tiba asili kwa magonjwa ya figo ambayo yanaongezeka kwa kasi katika siku za hivi karibuni.Akitoa maelezo katika banda la NIMR Meneja wa kituo cha NIMR Mabibo Dkt. Emmanuel Peter alibainisha mchango wa NIMR katika kukuza tiba asili nchini kuwa ni pamoja na kufanya tafiti za tiba asili, kushiriki katika huduma jumuishi, kujenga kiwanda cha kuzalisha dawa za tiba asili, kuhamasisha tafiti, ugunduzi na matumizi ya dawa za tiba asili, kuimarisha ushirikiano na wadau wa tiba asili Dkt. Peter alisema Kwa sasa, wananchi wanapata huduma jumuishi za tiba asili katika hospitali za rufaa za mikoa 14 ambapo mteja anaweza kuchagua tiba ya kisasa, tiba asili au kutumia zote kwa pamoja. “Huduma hii inamuwezesha mteja kufanyiwa vipimo vya kitaalamu na kupewa ushauri sahihi kuhusu tiba inayomfaa. Maadhimisho hayo, yenye kaulimbiu “Tuimarishe Huduma za Tiba Asili Zenye Ushahidi wa Kisayansi,” yalianza tarehe 25 Agosti 2025 na yanatarajiwa kutamatika tarehe 31 Agosti 2025. Tukio hili limewakutanisha wataalamu wa tiba asili na tiba mbadala kutoka maeneo mbalimbali nchini, kwa lengo la kubadilishana uzoefu, na kuhamasisha matumizi ya dawa za tiba asili kwa manufaa ya jamii. Section Title NIMR Yapongezwa kwa Mchango Mkubwa Katika Kukuza Tiba Asili ByErick Mboma August 31, 2025 Uncategorized Imeelezwa kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuendeleza tafiti za tiba asili na kuwekeza zaidi katika viwanda vya kuzalisha dawa za tiba hizo nchini, ili kuongeza tija katika kuboresha huduma za afya kwa… Read More Tiba Asili Yazidi Kung’ara: Tafiti Zaidi Zahitajika ByErick Mboma August 29, 2025 Uncategorized Imeelezwa kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuendeleza tafiti za tiba asili na kuwekeza zaidi katika viwanda vya kuzalisha dawa za tiba hizo nchini, ili kuongeza tija katika kuboresha huduma za afya kwa… Read More Tanzania to Learn on Traditional Medicine Sector from South Korea ByErick Mboma August 25, 2025 Uncategorized The Ministry of Health and the National Institute for Medical Research (NIMR) together with partner institutions embarked on a study visit to the National Institute for Korean Medicine Development… Read More Ministry of Health, NIMR Visits South Korea to Strengthen Innovation and Product Development in Traditional Medicine ByErick Mboma August 20, 2025 Uncategorized 𝗠𝗶𝗻𝗶𝘀𝘁𝗿𝘆 𝗼𝗳 𝗛𝗲𝗮𝗹𝘁𝗵, 𝗡𝗜𝗠𝗥 𝗩𝗶𝘀𝗶𝘁 𝗦𝗼𝘂𝘁𝗵 𝗞𝗼𝗿𝗲𝗮 𝘁𝗼 𝗦𝘁𝗿𝗲𝗻𝗴𝘁𝗵𝗲𝗻 𝗜𝗻𝗻𝗼𝘃𝗮𝘁𝗶𝗼𝗻 𝗮𝗻𝗱 𝗣𝗿𝗼𝗱𝘂𝗰𝘁 𝗗𝗲𝘃𝗲𝗹𝗼𝗽𝗺𝗲𝗻𝘁 𝗶𝗻 𝗧𝗿𝗮𝗱𝗶𝘁𝗶𝗼𝗻𝗮𝗹 𝗠𝗲𝗱𝗶𝗰𝗶𝗻𝗲 The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof… Read More NIMR, Wizara ya Afya Watoa Mafunzo kwa Wataalamu wa Afya Kutumia Teknolojia ya Uchambuzi na Ufuatiliaji wa Vinasaba vya Magonjwa ya Mlipuko ByErick Mboma August 20, 2025 Uncategorized Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa Kushirikiana na Wizara ya Afya, tarehe 18/08/2025 imeanza mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa maabara na watafiti kutoka taasisi… Read More Heri ya Siku ya Wakulima “Nanenane” ByErick Mboma August 8, 2025 Uncategorized Section Title Heri ya Siku ya Wakulima “Nanenane” ByErick Mboma August 8, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR), in partnership with the University of Oslo… Read More NIMR Hosts Pandemic Ethics Project General Assembly, Welcomes Experts from Six Countries ByErick Mboma July 30, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR), in partnership with the University of Oslo, hosted a high-level Pandemic Ethics General Assembly today 30th July 2025, at its Sub Office in Dar es… Read More NIMR Management Trained on Corporate Entrepreneurship ByErick Mboma July 30, 2025 Uncategorized In a strategic move to enhance institutional sustainability and increase revenue collections, the National Institute for Medical Research (NIMR) has conducted a high-level training on corporate… Read More NIMR Highlights Digital Health Solutions for HIV-Exposed Infants at National Child Health Congress ByErick Mboma July 27, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR) played a pivotal role in the 2nd Tanzania Child Health and Welfare Congress, held from 23rd – 25th July 2025 in Arusha, by spotlighting cutting-edge… Read More
NIMR Yapongezwa kwa Mchango Mkubwa Katika Kukuza Tiba Asili Read More »