NIMR

Wizara ya Afya leo tarehe 26/09/2025 imezindua Baraza jipya la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), hatua muhimu inayolenga kuimarisha utafiti wa kisayansi, kukuza ubunifu na kuhakikisha mafanikio ya Taasisi kwa ustawi wa watanzania.
Akizindua Baraza hilo katika ofisi ndogo za NIMR Jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe ambaye alimwakilisha Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama, amesisitiza umuhimu wa Baraza kutoa ushauri wa kitaalamu, kusimamia utendaji wa NIMR, na kuhakikisha matokeo ya tafiti yanachangia kuboresha huduma za afya nchini.
Aidha Dkt. Shekalaghe amesisitiza kuwa ushirikiano baina ya Baraza, Menejimenti na Wizara ya Afya ni muhimu ili kuimarisha tafiti za afya na kuhakikisha matokeo yanatumiwa ipasavyo katika kutatua changamoto za kiafya za wananchi.
Akimkaribisha Katibu Mkuu kuzindua Baraza, Mwenyekiti wa Baraza jipya Prof. James Mdoe, ameahidi kuliongoza Baraza kwa weledi na uadilifu, akisisitiza kuwa litahakikisha NIMR inatoa ushauri sahihi kwa Serikali. Amesema pia Taasisi itatumia teknolojia za kisasa na fursa za Mapinduzi ya Nne ya Viwanda (Fourth Industrial Revolution) kuongeza tija katika shughuli za utafiti.
“Mheshimiwa Katibu MkuuTunapenda kukuhakikishia kuwa, tupo tayari kwa kazi. Tutaweka juhudi zaidi na maarifa katika kutoa mchango wetu wa ushauri kwa mapana zaidi ili Taasisi iendelee kufanya kazi zake kwa ubora zaidi siku hadi siku ili kufikia malengo yake kwa faida ya Watanzania”. Amesisitiza Prof. Mdoe
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, aliwasilisha mafanikio ya Taasisi kwa kipindi cha miaka mitatu (2022/23 hadi 2024/25), akibainisha kuwa NIMR imeongeza idadi ya Miradi ya Utafiti na kufikia 150, huku machapisho ya kisayansi yameongezeka hadi 220 kwa mwaka. Aidha, vijarida sera vimefika 40 kwa mwaka lengo likiwa ni kutumika na watunga sera na wafanya maamuzi ili kuboresha huduma za afya nchini.
Prof. Aboud pia alibainisha mafanikio katika ubunifu wa tiba ikiwemo ugunduzi na uendelezaji wa broadly neutralizing antibodies (bNab) katika kituo cha NIMR Mbeya kwa ajili ya tiba ya VVU na UKIMWI. Taasisi pia imeboresha utoaji wa vibali vya utafiti na kupunguza muda kutoka miezi mitatu hadi ndani ya mwezi mmoja, kukarabati majengo chakavu ya vituo vya Gonja (Same), Amani Hill (Muheza), Ngongongare (Arusha) na Tabora, kukamilisha kusimika mitambo ya uzalishaji katika kituo cha tiba asili NIMR Mabibo, kupata ithibati ya kimataifa ya majaribio nasibu katika dawa za wadudu dhurifu (Efficacy Studies on Insecticidal Products) toka SANAS katika maabara ya NIMR Amani (Muheza), kuongezeka kwa makusanyo kutoka vyanzo vya ndani vya mapato na bajeti ya Taasisi kukua kutoka Sh. bilioni 51.5 hadi Sh. bilioni 89.7 bilioni huku ikiongeza rasilimali za ndani kwa ajili ya uendeshaji wa vituo vyake.
Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Mwenyekiti mpya wa Baraza, wajumbe wapya, Menejimenti ya NIMR pamoja na mwakilishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina. Hatua hizi inachagiza umuhimu wa kuendelea kufanya mageuzi ya Taasisi iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Bunge Na. 23 ya mwaka 1979.

Section Title

NIMR Yaongoza Mdahalo wa Sera Kuhakikisha Ushahidi wa Kisayansi Unatumika Kukabili Milipuko ya Magonjwa

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo, tarehe 8 Januari 2026, imeendesha mkutano wa majadiliano ya sera uliowakutanisha watafiti, watunga sera, watoa maamuzi wa sekta ya afya...

NIMR Unveils Genomic Evidence Showing Predominance of Bacterial Pathogens in Acute Respiratory Infections in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR) disseminated on 22nd December 2025 research findings from the project titled Genomic characterization of Acute Respiratory Infections (ARI) Pathogens...

Beyond Clinical Surveillance: Wastewater and Environmental Monitoring Reveal Hotspots of Antimicrobial-Resistant “Superbugs”

A recent study presented at the 7th Africa Continental World Antimicrobial Awareness Week (WAAW) event has unveiled the “environmental resistome” in Tanzania. Using advanced genomic tools to analyse...

NIMR Disseminates Impactful Research Findings at the 7th Africa Continental World AMR Awareness Week

In a milestone event for the continent, Tanzania hosted the 7th Africa Continental World Antimicrobial Resistance (AMR) Awareness Week (WAAW) at the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam from 2nd to...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi wa Afya Temeke Kuandika Andiko la Utafiti ili Kuboresha Huduma za Afya za Jamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya...

NIMR Conducts Institutional Review Boards Training to Elevate Clinical Trial Standards Nationwide

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched a specialized training program to members and secretariats of Institutional Review Boards (IRBs), aimed at strengthening national...

𝗡𝗜𝗠𝗥 Conducts Capacity Building Training for Clinical Trials Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR), in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), on 24th November 2025 conducted a specialized capacity-building...

NIMR na Wadau wa Afya Wafanya Mkutano wa Uzinduzi wa Utekelezaji wa Tafiti zilizo chini ya Mradi wa TAKeOFF wa Kupambana na Ugonjwa wa Mabusha na Matende

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa...

New Hope for Malaria Treatment: Tanzanian Scientists Lead Groundbreaking Clinical Trial

The National Institute for Medical Research (NIMR) Tanga Medical Research Centre, led by Principal Investigator Dr. Samwel Gesase as the country Coordinator, has been instrumental in the...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.