NIMR

Imeelezwa kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuendeleza tafiti za tiba asili na kuwekeza zaidi katika viwanda vya kuzalisha dawa za tiba hizo nchini, ili kuongeza tija katika kuboresha huduma za afya kwa jamii. Kwa sasa, wananchi wengi wameonyesha mwamko mkubwa wa kutumia dawa za tiba asili.
Kauli hiyo imetolewa leo, Agosti 29, 2025 na Dkt. Ahmad Mohamed Makuwani Mkurugenzi wa Huduma ya Afya ya Uzazi, Magonjwa ya Wanawake na Watoto kutoka Wizara ya Afya, alipomuwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya katika Kongamano la Nne la Kisayansi la Tiba Asili lililoandaliwa na kuratibiwa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gaspar, jijini Dodoma.
Dkt. Makuani amewataka watafiti na wadau wa tiba asili kuwekeza nguvu katika kupata ushahidi wa kisayansi wa dawa hizo utakaosaidia kuimarisha sera za afya na kukuza ushirikiano kati ya wanasayansi na wataalamu wa tiba asili.
“Ili kuendeleza usawa wa afya, ni lazima dawa za tiba asili ambazo zimethibitishwa kuwa salama, zenye ufanisi na ubora ziingizwe rasmi kwenye mifumo ya utoaji huduma za afya. Tanzania tayari imeweka msingi imara kupitia Sheria ya Tiba Asili na Tiba Mbadala ya mwaka 2002 pamoja na Sheria ya NIMR ya mwaka 1980,” amesisitiza Dkt. Makuani.
Aidha, amependekeza kuundwa kwa mifumo ya ushirikiano na rufaa kati ya tiba asili na tiba za kisasa, kujumuisha tiba asili katika miongozo ya matibabu, na kujenga uaminifu kati ya wataalamu wa afya na waganga wa tiba asili.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud, amesema taasisi hiyo ina jukumu kubwa la kuhakikisha usalama, ufanisi na ubora wa dawa za tiba asili, ili kumlinda mwananchi dhidi ya madhara yanayoweza kusababishwa na dawa zisizo salama.
Prof. Aboud amewataka waganga na wataalamu wa tiba asili kupeleka dawa zao NIMR na katika taasisi zingine zenye mamlaka ili zipimwe na kuthibitishwa. “Hii itawezesha dawa hizo kuwa sehemu ya huduma jumuishi katika hospitali 14 za rufaa nchini,” amesisitiza Prof. Aboud.
Kongamano hilo la siku moja limewakutanisha wadau wa tiba asili kutoka ndani na nje ya nchi, ambapo walijadili matokeo ya tafiti mbalimbali. Kongamano hilo pia limeambatana na Maonesho ya Wiki ya Tiba Asili ya Mwafrika, yaliyofunguliwa

Section Title

NIMR Yaongoza Mdahalo wa Sera Kuhakikisha Ushahidi wa Kisayansi Unatumika Kukabili Milipuko ya Magonjwa

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo, tarehe 8 Januari 2026, imeendesha mkutano wa majadiliano ya sera uliowakutanisha watafiti, watunga sera, watoa maamuzi wa sekta ya afya...

NIMR Unveils Genomic Evidence Showing Predominance of Bacterial Pathogens in Acute Respiratory Infections in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR) disseminated on 22nd December 2025 research findings from the project titled Genomic characterization of Acute Respiratory Infections (ARI) Pathogens...

Beyond Clinical Surveillance: Wastewater and Environmental Monitoring Reveal Hotspots of Antimicrobial-Resistant “Superbugs”

A recent study presented at the 7th Africa Continental World Antimicrobial Awareness Week (WAAW) event has unveiled the “environmental resistome” in Tanzania. Using advanced genomic tools to analyse...

NIMR Disseminates Impactful Research Findings at the 7th Africa Continental World AMR Awareness Week

In a milestone event for the continent, Tanzania hosted the 7th Africa Continental World Antimicrobial Resistance (AMR) Awareness Week (WAAW) at the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam from 2nd to...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi wa Afya Temeke Kuandika Andiko la Utafiti ili Kuboresha Huduma za Afya za Jamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya...

NIMR Conducts Institutional Review Boards Training to Elevate Clinical Trial Standards Nationwide

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched a specialized training program to members and secretariats of Institutional Review Boards (IRBs), aimed at strengthening national...

𝗡𝗜𝗠𝗥 Conducts Capacity Building Training for Clinical Trials Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR), in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), on 24th November 2025 conducted a specialized capacity-building...

NIMR na Wadau wa Afya Wafanya Mkutano wa Uzinduzi wa Utekelezaji wa Tafiti zilizo chini ya Mradi wa TAKeOFF wa Kupambana na Ugonjwa wa Mabusha na Matende

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa...

New Hope for Malaria Treatment: Tanzanian Scientists Lead Groundbreaking Clinical Trial

The National Institute for Medical Research (NIMR) Tanga Medical Research Centre, led by Principal Investigator Dr. Samwel Gesase as the country Coordinator, has been instrumental in the...