NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo, tarehe 8 Januari 2026, imeendesha mkutano wa majadiliano ya sera uliowakutanisha watafiti, watunga sera, watoa maamuzi wa sekta ya afya na wadau mbalimbali, kwa lengo la kuimarisha matumizi ya ushahidi wa kisayansi katika kuandaa na kutekeleza sera zinazohusu maandalizi, kinga na mwitikio wa taifa dhidi ya magonjwa yanayolipuka na kurejea mara kwa mara.
Akifungua mkutano huo, Mgeni Rasmi Dkt. Ahmad Mohamed Makuwani, Mkurugenzi wa Huduma ya Afya ya Uzazi, Magonjwa ya Wanawake na Watoto kutoka Wizara ya Afya, akimwakilisha Mganga Mkuu wa Serikali, amesema kuwa majadiliano hayo yanakuja katika kipindi muhimu kwa taifa, ambapo kumekuwa na kuendelea kushuhudiwa kwa milipuko ya magonjwa kama kipindupindu, dengue, COVID-19 na Marburg. Amesema hali hiyo inaweka shinikizo kubwa kwa mifumo ya afya na hivyo kuhitaji sera zinazojengwa juu ya ushahidi madhubuti wa kisayansi.
“Mkutano huu ni jukwaa muhimu la kutafakari mazingira ya milipuko ya magonjwa nchini na kuimarisha uwezo wa pamoja wa taifa katika kuzuia, kugundua mapema na kukabiliana na vitisho vya afya ya jamii vya sasa na vya baadaye,” amebainisha Dkt. Makuwani. Ameongeza kuwa majadiliano ya sera ni nyenzo muhimu ya kuunganisha tafiti na maamuzi ya kisera ili kufanikisha uamuzi unaozingatia ushahidi.
Aidha, Dkt. Makuwani amesisitiza umuhimu wa kuimarisha tafiti za ndani, ikiwemo utafiti wa tiba asili, akibainisha kuwa uzoefu wa mlipuko wa UVIKO-19 umeonesha mchango wa tiba asili katika kupunguza madhara kwa jamii. Akitoa wito, ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika tafiti za tiba asili na mifumo ya kitaifa ya utafiti.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Profesa Said Aboud, amesema kuwa mkutano huo umeandaliwa mahsusi kushughulikia masuala nyeti yanayohusiana na magonjwa yenye uwezekano wa kusababisha milipuko, huku ukilenga kuhakikisha matokeo ya tafiti yanatafsiriwa na kutumika moja kwa moja katika sera na mipango ya kitaifa.
Prof. Aboud ameeleza kuwa mkutano huo ni jukwaa la tafsiri ya maarifa, linalowaunganisha watafiti, watunga sera na watekelezaji ili kujadili ushahidi uliopo, kubadilishana uzoefu na kuandaa mapendekezo yatakayosaidia kuimarisha maandalizi, kinga na mwitikio wa taifa dhidi ya milipuko ya magonjwa.
“Tafiti zinaonesha kuwa maandalizi madhubuti dhidi ya milipuko yanategemea mifumo imara ya ufuatiliaji wa magonjwa, nguvu kazi ya afya iliyo imara na minyororo thabiti ya upatikanaji wa vifaa tiba,” ameongeza Prof. Aboud.
James Tumain Tengia, mwakilishi kutoka Wizara ya TAMISEMI, ameipongeza NIMR kwa kuandaa mkutano huo, akisema kuwa umefanikiwa kuwakutanisha watafiti, watunga sera na watoa maamuzi ili kuchakata matokeo ya tafiti mbalimbali na kuja na maoni yatakayosaidia kuboresha sera na miongozo ya utoaji wa huduma za afya.
Elizabeth Shayo, Mtafiti Mkuu kutoka NIMR, amesema kuwa mkutano huo umekuwa na manufaa makubwa kwa kuwa umetoa fursa ya kujadili namna bora ya kupambana na magonjwa ya mlipuko yanayoweza kutokea nchini.
Akitoa majumuisho ya mkutano huo, Dkt. Ernest Mazigo, mtafiti kutoka NIMR na mratibu wa mdahalo huo amesema kuwa wadau ambao ni watunga sera na watoa maamuzi wamepokea mapendekezo mbalimbali yaliyotolewa na wameanza kuangalia namna ya kuyaingiza katika mifumo na utekelezaji wa sera za afya.
Mdahalo huo wa siku moja uliofanyika katika Ukumbi wa CEEMI, ofisi ndogo za NIMR jijini Dar es Salaam, ulijikita katika kuangalia namna ushahidi wa kisayansi unavyoweza kuboresha sera na miongozo ya utoaji wa huduma za afya nchini, pamoja na kubaini vipaumbele vya tafiti na mapungufu ya utekelezaji. Mdahalo huo uliandaliwa kwa ushirikiano wa wataalamu kutoka Kurugenzi ya Kuratibu na Kukuza Utafiti ya NIMR akiwemo Mr. Emmanuel Makundi, Dkt. Stellah Kilima na Dkt. Elizabeth Shayo, huku Profesa Moshi Ntabaye aliyeendesha mjadala huo akishiriki kikamilifu katika kufanikisha mdahalo huo wa sera.

Section Title

NIMR Yaongoza Mdahalo wa Sera Kuhakikisha Ushahidi wa Kisayansi Unatumika Kukabili Milipuko ya Magonjwa

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo, tarehe 8 Januari 2026, imeendesha mkutano wa majadiliano ya sera uliowakutanisha watafiti, watunga sera, watoa maamuzi wa sekta ya afya...

NIMR Unveils Genomic Evidence Showing Predominance of Bacterial Pathogens in Acute Respiratory Infections in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR) disseminated on 22nd December 2025 research findings from the project titled Genomic characterization of Acute Respiratory Infections (ARI) Pathogens...

Beyond Clinical Surveillance: Wastewater and Environmental Monitoring Reveal Hotspots of Antimicrobial-Resistant “Superbugs”

A recent study presented at the 7th Africa Continental World Antimicrobial Awareness Week (WAAW) event has unveiled the “environmental resistome” in Tanzania. Using advanced genomic tools to analyse...

NIMR Disseminates Impactful Research Findings at the 7th Africa Continental World AMR Awareness Week

In a milestone event for the continent, Tanzania hosted the 7th Africa Continental World Antimicrobial Resistance (AMR) Awareness Week (WAAW) at the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam from 2nd to...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi wa Afya Temeke Kuandika Andiko la Utafiti ili Kuboresha Huduma za Afya za Jamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya...

NIMR Conducts Institutional Review Boards Training to Elevate Clinical Trial Standards Nationwide

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched a specialized training program to members and secretariats of Institutional Review Boards (IRBs), aimed at strengthening national...

𝗡𝗜𝗠𝗥 Conducts Capacity Building Training for Clinical Trials Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR), in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), on 24th November 2025 conducted a specialized capacity-building...

NIMR na Wadau wa Afya Wafanya Mkutano wa Uzinduzi wa Utekelezaji wa Tafiti zilizo chini ya Mradi wa TAKeOFF wa Kupambana na Ugonjwa wa Mabusha na Matende

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa...

New Hope for Malaria Treatment: Tanzanian Scientists Lead Groundbreaking Clinical Trial

The National Institute for Medical Research (NIMR) Tanga Medical Research Centre, led by Principal Investigator Dr. Samwel Gesase as the country Coordinator, has been instrumental in the...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.