NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeanza rasmi utekelezaji wa utafiti wa majaribio ya tiba ya kuharakisha kutokomeza maambukizi ya ugonjwa wa matende na mabusha. Hayo yamebainishwa wakati wa kuendesha mafunzo ya siku mbili ya kutekeleza utafiti kwa watafiti na watoa huduma wa afya kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara.
Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, yalifunguliwa rasmi na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Mwinjuma M. Mkungu. Katika hotuba yake, aliipongeza NIMR kwa kuwa kinara wa tafiti za afya nchini na kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya katika kuandaa tafiti zenye lengo la kumaliza kabisa magonjwa yanayosumbua jamii, hususani yale yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (NTDs).
โ€œNIMR ni nguzo muhimu katika sekta ya afya kwa kuwa inatoa ushahidi wa kisayansi unaosaidia kupanga na kutekeleza afua bora. Mafunzo haya ni sehemu ya juhudi hizo,โ€ alisema Mhe. Mkungu.
Mafunzo hayo yamefuatiwa na kuanza kwa uchukuaji wa sampuli kwa washiriki wa utafiti katika kijiji cha Ruaha, kata ya Mnazi Mmoja, Wilaya ya Lindi. Utafiti huu wa kisayansi unalenga kulinganisha tiba tofauti za magonjwa ya matende na mabusha, hususani dawa ya โ€œDoxycyclineโ€ na โ€œMoxidectin + Albendazoleโ€, dhidi ya Kingatiba iliyopo sasa ya โ€œIvermectin + Albendazoleโ€.
Mtafiti Mkuu wa mradi wa utafiti kutoka NIMR, Dkt. Akili Kalinga, alisema kuwa tafiti hizi zinalenga kutafuta tiba mbadala na bora zaidi ambazo zitaweza kuharakisha kutokomeza ugonjwa huo nchini. โ€œTumekuwa kwenye mapambano dhidi ya matende na mabusha kwa miaka mingi. Tunategemea kuwa utafiti huu utasaidia kuondoa kabisa vikwazo vinavyosababisha maambukizi ya Ugonjwa huu kuendelea katika baadhi ya maeneo.โ€ alisema Dkt. Kalinga.
Akizungumza wakati wa zoezi la uchukuaji wa sampuli, Mwenyekiti wa Kijiji cha Ruaha, Bi. Salima Kidamchong`we, alisema kuwa utafiti huo ni muhimu sana kwa jamii yao kwa sababu unawapa fursa ya kujua hali yao ya kiafya. โ€œTunatoa shukrani kwa NIMR na Wizara ya Afya kwa kutuletea utafiti huu. Ni jambo la maana na lenye manufaa kwa wananchi wetu,โ€ alisema.
Naye mmoja wa washiriki wa utafiti kutoka kijiji cha Ruaha kata ya Mnazi Mmoja, Bw. Ali Bakari Natulama, aliipongeza NIMR kwa juhudi zake na kusema kwamba tafiti kama hizi zinasaidia sana katika kuelimisha jamii na kuwakinga na magonjwa hatari kama matende na mabusha.
Kwa sasa, ugonjwa wa matende na mabusha bado upo katika baadhi ya Halmashauri za wilaya nchini Tanzania ikiwemo Lindi Manispaa, Mtama, Mikindani, Kinondoni na Pangani. Licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa Halmashauri 114 kutokomeza maambukizi ya Ugonjwa na kusitisha ugawaji wa kingatiba uliofanyika kwa miaka mingi.
NIMR inatarajia kutumia matokeo ya utafiti huu kuboresha miongozo ya kitaifa na kidunia ya tiba na udhibiti wa magonjwa haya, kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya na wadau wengine.

Section Title

NIMR Leads Global Effort to Combat Arboviral Diseases Using One Health Approach

In demonstration of leadership in global health research, the National Institute for Medical Research (NIMR) conducted a five-day Arboviral Workshop at NIMR Mbeya Medical Research Centre under the...

Baraza Jipya la NIMR Lapatiwa Mafunzo ya Uongozi na Utawala Bora kwa Taasisi za Umma

Baraza jipya la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) limepatiwa mafunzo ya uongozi na utawala bora siku tatu kuanzia tarehe 6 hadi 8 Oktoba 2025 na Taasisi ya Uongozi (Uongozi...

NIMR Strengthens Global Research Collaboration

The National Institute for Medical Research (NIMR) on 29th September 2025, launched a five-day research collaboration meeting at Mwanza Medical Research Centre, focusing on sharing research findings...

Wizara ya Afya Yazindua Baraza la Nimr Jipya

Wizara ya Afya leo tarehe 26/09/2025 imezindua Baraza jipya la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), hatua muhimu inayolenga kuimarisha utafiti wa kisayansi, kukuza ubunifu na...

CARDIOVASCULAR DISEASE SYMPOSIUM

Section Title CARDIOVASCULAR DISEASE SYMPOSIUM ByErick Mboma September 24, 2025 Uncategorized Section Title CARDIOVASCULAR DISEASE SYMPOSIUM ByErick Mboma September 24, 2025 Uncategorized Section...

NIMR Yapongezwa kwa Mchango Mkubwa Katika Kukuza Tiba Asili

Wananchi wanaendelea kunufaika na huduma za tiba asili kupitia tafiti, na uanzishwaji wa kiwanda cha kuzalisha dawa za tiba asili cha NIMR Mabibo kufuatia juhudi kubwa za Serikali kuhakikisha dawa...

Tiba Asili Yazidi Kungโ€™ara: Tafiti Zaidi Zahitajika

Imeelezwa kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuendeleza tafiti za tiba asili na kuwekeza zaidi katika viwanda vya kuzalisha dawa za tiba hizo nchini, ili kuongeza tija katika kuboresha huduma za afya kwa...

Tanzania to Learn on Traditional Medicine Sector from South Korea

The Ministry of Health and the National Institute for Medical Research (NIMR) together with partner institutions embarked on a study visit to the National Institute for Korean Medicine Development...

Ministry of Health, NIMR Visits South Korea to Strengthen Innovation and Product Development in Traditional Medicine

๐— ๐—ถ๐—ป๐—ถ๐˜€๐˜๐—ฟ๐˜† ๐—ผ๐—ณ ๐—›๐—ฒ๐—ฎ๐—น๐˜๐—ต, ๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ฉ๐—ถ๐˜€๐—ถ๐˜ ๐—ฆ๐—ผ๐˜‚๐˜๐—ต ๐—ž๐—ผ๐—ฟ๐—ฒ๐—ฎ ๐˜๐—ผ ๐—ฆ๐˜๐—ฟ๐—ฒ๐—ป๐—ด๐˜๐—ต๐—ฒ๐—ป ๐—œ๐—ป๐—ป๐—ผ๐˜ƒ๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป ๐—ฎ๐—ป๐—ฑ ๐—ฃ๐—ฟ๐—ผ๐—ฑ๐˜‚๐—ฐ๐˜ ๐——๐—ฒ๐˜ƒ๐—ฒ๐—น๐—ผ๐—ฝ๐—บ๐—ฒ๐—ป๐˜ ๐—ถ๐—ป ๐—ง๐—ฟ๐—ฎ๐—ฑ๐—ถ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป๐—ฎ๐—น ๐— ๐—ฒ๐—ฑ๐—ถ๐—ฐ๐—ถ๐—ป๐—ฒ The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof...