NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeanza rasmi utekelezaji wa utafiti wa majaribio ya tiba ya kuharakisha kutokomeza maambukizi ya ugonjwa wa matende na mabusha. Hayo yamebainishwa wakati wa kuendesha mafunzo ya siku mbili ya kutekeleza utafiti kwa watafiti na watoa huduma wa afya kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara.
Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, yalifunguliwa rasmi na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Mwinjuma M. Mkungu. Katika hotuba yake, aliipongeza NIMR kwa kuwa kinara wa tafiti za afya nchini na kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya katika kuandaa tafiti zenye lengo la kumaliza kabisa magonjwa yanayosumbua jamii, hususani yale yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (NTDs).
“NIMR ni nguzo muhimu katika sekta ya afya kwa kuwa inatoa ushahidi wa kisayansi unaosaidia kupanga na kutekeleza afua bora. Mafunzo haya ni sehemu ya juhudi hizo,” alisema Mhe. Mkungu.
Mafunzo hayo yamefuatiwa na kuanza kwa uchukuaji wa sampuli kwa washiriki wa utafiti katika kijiji cha Ruaha, kata ya Mnazi Mmoja, Wilaya ya Lindi. Utafiti huu wa kisayansi unalenga kulinganisha tiba tofauti za magonjwa ya matende na mabusha, hususani dawa ya “Doxycycline” na “Moxidectin + Albendazole”, dhidi ya Kingatiba iliyopo sasa ya “Ivermectin + Albendazole”.
Mtafiti Mkuu wa mradi wa utafiti kutoka NIMR, Dkt. Akili Kalinga, alisema kuwa tafiti hizi zinalenga kutafuta tiba mbadala na bora zaidi ambazo zitaweza kuharakisha kutokomeza ugonjwa huo nchini. “Tumekuwa kwenye mapambano dhidi ya matende na mabusha kwa miaka mingi. Tunategemea kuwa utafiti huu utasaidia kuondoa kabisa vikwazo vinavyosababisha maambukizi ya Ugonjwa huu kuendelea katika baadhi ya maeneo.” alisema Dkt. Kalinga.
Akizungumza wakati wa zoezi la uchukuaji wa sampuli, Mwenyekiti wa Kijiji cha Ruaha, Bi. Salima Kidamchong`we, alisema kuwa utafiti huo ni muhimu sana kwa jamii yao kwa sababu unawapa fursa ya kujua hali yao ya kiafya. “Tunatoa shukrani kwa NIMR na Wizara ya Afya kwa kutuletea utafiti huu. Ni jambo la maana na lenye manufaa kwa wananchi wetu,” alisema.
Naye mmoja wa washiriki wa utafiti kutoka kijiji cha Ruaha kata ya Mnazi Mmoja, Bw. Ali Bakari Natulama, aliipongeza NIMR kwa juhudi zake na kusema kwamba tafiti kama hizi zinasaidia sana katika kuelimisha jamii na kuwakinga na magonjwa hatari kama matende na mabusha.
Kwa sasa, ugonjwa wa matende na mabusha bado upo katika baadhi ya Halmashauri za wilaya nchini Tanzania ikiwemo Lindi Manispaa, Mtama, Mikindani, Kinondoni na Pangani. Licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa Halmashauri 114 kutokomeza maambukizi ya Ugonjwa na kusitisha ugawaji wa kingatiba uliofanyika kwa miaka mingi.
NIMR inatarajia kutumia matokeo ya utafiti huu kuboresha miongozo ya kitaifa na kidunia ya tiba na udhibiti wa magonjwa haya, kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya na wadau wengine.

Section Title

NIMR Yaongoza Mdahalo wa Sera Kuhakikisha Ushahidi wa Kisayansi Unatumika Kukabili Milipuko ya Magonjwa

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo, tarehe 8 Januari 2026, imeendesha mkutano wa majadiliano ya sera uliowakutanisha watafiti, watunga sera, watoa maamuzi wa sekta ya afya...

NIMR Unveils Genomic Evidence Showing Predominance of Bacterial Pathogens in Acute Respiratory Infections in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR) disseminated on 22nd December 2025 research findings from the project titled Genomic characterization of Acute Respiratory Infections (ARI) Pathogens...

Beyond Clinical Surveillance: Wastewater and Environmental Monitoring Reveal Hotspots of Antimicrobial-Resistant “Superbugs”

A recent study presented at the 7th Africa Continental World Antimicrobial Awareness Week (WAAW) event has unveiled the “environmental resistome” in Tanzania. Using advanced genomic tools to analyse...

NIMR Disseminates Impactful Research Findings at the 7th Africa Continental World AMR Awareness Week

In a milestone event for the continent, Tanzania hosted the 7th Africa Continental World Antimicrobial Resistance (AMR) Awareness Week (WAAW) at the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam from 2nd to...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi wa Afya Temeke Kuandika Andiko la Utafiti ili Kuboresha Huduma za Afya za Jamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya...

NIMR Conducts Institutional Review Boards Training to Elevate Clinical Trial Standards Nationwide

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched a specialized training program to members and secretariats of Institutional Review Boards (IRBs), aimed at strengthening national...

𝗡𝗜𝗠𝗥 Conducts Capacity Building Training for Clinical Trials Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR), in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), on 24th November 2025 conducted a specialized capacity-building...

NIMR na Wadau wa Afya Wafanya Mkutano wa Uzinduzi wa Utekelezaji wa Tafiti zilizo chini ya Mradi wa TAKeOFF wa Kupambana na Ugonjwa wa Mabusha na Matende

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa...

New Hope for Malaria Treatment: Tanzanian Scientists Lead Groundbreaking Clinical Trial

The National Institute for Medical Research (NIMR) Tanga Medical Research Centre, led by Principal Investigator Dr. Samwel Gesase as the country Coordinator, has been instrumental in the...