NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa Kushirikiana na Wizara ya Afya, tarehe 18/08/2025 imeanza mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa maabara na watafiti kutoka taasisi mbalimbali za afya, lengo likiwa ni kuimarisha uwezo wa Wizara ya Afya na taasisi zake katika kuchambua (Bioinformatics) takwimu za mpangilio wa vinasaba (NGS data) za magonjwa ya mlipuko zinazozalishwa nchini Tanzania, ili kutambua aina na kufuatilia mabadiliko ya vimelea hivyo vya maradhi.
Akifungua mafunzo hayo ya siku tano yanayofanyika mjini Morogoro, Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Epidemiolojia na Udhibiti wa Magonjwa kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Vida Mmbaga, amesema mafunzo hayo ni hatua muhimu katika kuimarisha uwezo wa wataalamu wa maabara kutumia teknolojia ya kisasa katika mapambano dhidi ya magonjwa ya mlipuko.

“Kuchakata takwimu hizi kutasaidia kutoa usaidizi kwa nguzo zingine za udhibiti ambazo zinafanya kazi kwa pamoja na maabara, kwani kazi ya utabibu inategemea utambuzi kutoka maabara. Hivyo, wataalamu hawa wakiboresha uchambuzi wa kina, utaalamu wao utasaidia zaidi katika kudhibiti magonjwa,” amesema Dkt. Mmbaga.

Ameongeza kuwa Serikali inalenga kuboresha uchakataji wa takwimu za vimelea vya maradhi kwa usahihi ili kusaidia kudhibiti magonjwa kwa ufanisi na uhakika.
Naye Dkt. Clara Lubinza Mtafiti kutoka NIMR na Mratibu Msaidizi wa Mradi wa Global Heath Security ambao NIMR inatekeleza kwa kushirikiana na Wizara ya Afya amesema mafunzo hayo yatawasaidia wataalamu wa afya na maabara kuweza kuvisoma vinasaba vya vimelea vya magonjwa, kuvielewa ni vimelea vya aina gani na kuvitambua vinapokua vinabadilika.
Aidha Dkt. Clara ameeleza kuwa matarajio baada ya mafunzo hayo ni kuhakikisha wataalamu wa afya wanapata uwezo wa kuchambua na kutambua vimelea vinavyosababisha magonjwa mbalimbali, kubaini tabia, aina na maeneo vinaposambaa, na kutambua mapema iwapo vitabadilika. “Hatua hii itawawezesha watalaamu wetu kutoa taarifa kwa Wizara ya Afya kwa wakati, ili kuchukua hatua za haraka za kudhibiti na kuzuia usambazaji zaidi wa vimelea hivyo.” Alieleza Dkt. Clara.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na NIMR kwa kushirikiana na Wizara ya Afya yamewakutanisha pamoja wataalamu kutoa NIMR, Wizara ya Afya, Maabara Kuu ya Taifa ya Afya ya Jamii, Hospital ya Magonjwa ya Mlipuko Kibong`oto, na Maabara ya Afya ya Jamii ya Zanzibar.

Section Title

Beyond Clinical Surveillance: Wastewater and Environmental Monitoring Reveal Hotspots of Antimicrobial-Resistant “Superbugs”

A recent study presented at the 7th Africa Continental World Antimicrobial Awareness Week (WAAW) event has unveiled the “environmental resistome” in Tanzania. Using advanced genomic tools to analyse...

NIMR Disseminates Impactful Research Findings at the 7th Africa Continental World AMR Awareness Week

In a milestone event for the continent, Tanzania hosted the 7th Africa Continental World Antimicrobial Resistance (AMR) Awareness Week (WAAW) at the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam from 2nd to...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi wa Afya Temeke Kuandika Andiko la Utafiti ili Kuboresha Huduma za Afya za Jamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya...

NIMR Conducts Institutional Review Boards Training to Elevate Clinical Trial Standards Nationwide

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched a specialized training program to members and secretariats of Institutional Review Boards (IRBs), aimed at strengthening national...

𝗡𝗜𝗠𝗥 Conducts Capacity Building Training for Clinical Trials Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR), in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), on 24th November 2025 conducted a specialized capacity-building...

NIMR na Wadau wa Afya Wafanya Mkutano wa Uzinduzi wa Utekelezaji wa Tafiti zilizo chini ya Mradi wa TAKeOFF wa Kupambana na Ugonjwa wa Mabusha na Matende

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa...

New Hope for Malaria Treatment: Tanzanian Scientists Lead Groundbreaking Clinical Trial

The National Institute for Medical Research (NIMR) Tanga Medical Research Centre, led by Principal Investigator Dr. Samwel Gesase as the country Coordinator, has been instrumental in the...

NIMR Yazidi Kung`ara Kimataifa

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kung’ara kimataifa iliposhiriki katika kongamano la kisayansi la American Society of Tropical Medicine and Hygiene (ASTMH) kwa...

NIMR Leads Global Effort to Combat Arboviral Diseases Using One Health Approach

In demonstration of leadership in global health research, the National Institute for Medical Research (NIMR) conducted a five-day Arboviral Workshop at NIMR Mbeya Medical Research Centre under the...