NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa Kushirikiana na Wizara ya Afya, tarehe 18/08/2025 imeanza mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa maabara na watafiti kutoka taasisi mbalimbali za afya, lengo likiwa ni kuimarisha uwezo wa Wizara ya Afya na taasisi zake katika kuchambua (Bioinformatics) takwimu za mpangilio wa vinasaba (NGS data) za magonjwa ya mlipuko zinazozalishwa nchini Tanzania, ili kutambua aina na kufuatilia mabadiliko ya vimelea hivyo vya maradhi.
Akifungua mafunzo hayo ya siku tano yanayofanyika mjini Morogoro, Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Epidemiolojia na Udhibiti wa Magonjwa kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Vida Mmbaga, amesema mafunzo hayo ni hatua muhimu katika kuimarisha uwezo wa wataalamu wa maabara kutumia teknolojia ya kisasa katika mapambano dhidi ya magonjwa ya mlipuko.

โ€œKuchakata takwimu hizi kutasaidia kutoa usaidizi kwa nguzo zingine za udhibiti ambazo zinafanya kazi kwa pamoja na maabara, kwani kazi ya utabibu inategemea utambuzi kutoka maabara. Hivyo, wataalamu hawa wakiboresha uchambuzi wa kina, utaalamu wao utasaidia zaidi katika kudhibiti magonjwa,โ€ amesema Dkt. Mmbaga.

Ameongeza kuwa Serikali inalenga kuboresha uchakataji wa takwimu za vimelea vya maradhi kwa usahihi ili kusaidia kudhibiti magonjwa kwa ufanisi na uhakika.
Naye Dkt. Clara Lubinza Mtafiti kutoka NIMR na Mratibu Msaidizi wa Mradi wa Global Heath Security ambao NIMR inatekeleza kwa kushirikiana na Wizara ya Afya amesema mafunzo hayo yatawasaidia wataalamu wa afya na maabara kuweza kuvisoma vinasaba vya vimelea vya magonjwa, kuvielewa ni vimelea vya aina gani na kuvitambua vinapokua vinabadilika.
Aidha Dkt. Clara ameeleza kuwa matarajio baada ya mafunzo hayo ni kuhakikisha wataalamu wa afya wanapata uwezo wa kuchambua na kutambua vimelea vinavyosababisha magonjwa mbalimbali, kubaini tabia, aina na maeneo vinaposambaa, na kutambua mapema iwapo vitabadilika. โ€œHatua hii itawawezesha watalaamu wetu kutoa taarifa kwa Wizara ya Afya kwa wakati, ili kuchukua hatua za haraka za kudhibiti na kuzuia usambazaji zaidi wa vimelea hivyo.โ€ Alieleza Dkt. Clara.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na NIMR kwa kushirikiana na Wizara ya Afya yamewakutanisha pamoja wataalamu kutoa NIMR, Wizara ya Afya, Maabara Kuu ya Taifa ya Afya ya Jamii, Hospital ya Magonjwa ya Mlipuko Kibong`oto, na Maabara ya Afya ya Jamii ya Zanzibar.

Section Title

NIMR Yapongezwa kwa Mchango Mkubwa Katika Kukuza Tiba Asili

Wananchi wanaendelea kunufaika na huduma za tiba asili kupitia tafiti, na uanzishwaji wa kiwanda cha kuzalisha dawa za tiba asili cha NIMR Mabibo kufuatia juhudi kubwa za Serikali kuhakikisha dawa...

Tiba Asili Yazidi Kungโ€™ara: Tafiti Zaidi Zahitajika

Imeelezwa kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuendeleza tafiti za tiba asili na kuwekeza zaidi katika viwanda vya kuzalisha dawa za tiba hizo nchini, ili kuongeza tija katika kuboresha huduma za afya kwa...

Tanzania to Learn on Traditional Medicine Sector from South Korea

The Ministry of Health and the National Institute for Medical Research (NIMR) together with partner institutions embarked on a study visit to the National Institute for Korean Medicine Development...

Ministry of Health, NIMR Visits South Korea to Strengthen Innovation and Product Development in Traditional Medicine

๐— ๐—ถ๐—ป๐—ถ๐˜€๐˜๐—ฟ๐˜† ๐—ผ๐—ณ ๐—›๐—ฒ๐—ฎ๐—น๐˜๐—ต, ๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ฉ๐—ถ๐˜€๐—ถ๐˜ ๐—ฆ๐—ผ๐˜‚๐˜๐—ต ๐—ž๐—ผ๐—ฟ๐—ฒ๐—ฎ ๐˜๐—ผ ๐—ฆ๐˜๐—ฟ๐—ฒ๐—ป๐—ด๐˜๐—ต๐—ฒ๐—ป ๐—œ๐—ป๐—ป๐—ผ๐˜ƒ๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป ๐—ฎ๐—ป๐—ฑ ๐—ฃ๐—ฟ๐—ผ๐—ฑ๐˜‚๐—ฐ๐˜ ๐——๐—ฒ๐˜ƒ๐—ฒ๐—น๐—ผ๐—ฝ๐—บ๐—ฒ๐—ป๐˜ ๐—ถ๐—ป ๐—ง๐—ฟ๐—ฎ๐—ฑ๐—ถ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป๐—ฎ๐—น ๐— ๐—ฒ๐—ฑ๐—ถ๐—ฐ๐—ถ๐—ป๐—ฒ The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof...

NIMR, Wizara ya Afya Watoa Mafunzo kwa Wataalamu wa Afya Kutumia Teknolojia ya Uchambuzi na Ufuatiliaji wa Vinasaba vya Magonjwa ya Mlipuko

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa Kushirikiana na Wizara ya Afya, tarehe 18/08/2025 imeanza mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa maabara na watafiti kutoka taasisi...

Heri ya Siku ya Wakulima “Nanenane”

Section Title Heri ya Siku ya Wakulima “Nanenane” ByErick Mboma August 8, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR), in partnership with the University of Oslo...

NIMR Hosts Pandemic Ethics Project General Assembly, Welcomes Experts from Six Countries

The National Institute for Medical Research (NIMR), in partnership with the University of Oslo, hosted a high-level Pandemic Ethics General Assembly today 30th July 2025, at its Sub Office in Dar es...

NIMR Management Trained on Corporate Entrepreneurship

In a strategic move to enhance institutional sustainability and increase revenue collections, the National Institute for Medical Research (NIMR) has conducted a high-level training on corporate...

NIMR Highlights Digital Health Solutions for HIV-Exposed Infants at National Child Health Congress

The National Institute for Medical Research (NIMR) played a pivotal role in the 2nd Tanzania Child Health and Welfare Congress, held from 23rd โ€“ 25th July 2025 in Arusha, by spotlighting cutting-edge...