NIMR

Mwenyekiti mpya wa Baraza la Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James Mdoe, amefurahishwa na kazi inayofanywa na Kituo cha Utafiti wa Dawa za Tiba Asili cha NIMR Mabibo katika kuendeleza tafiti za tiba mbadala kwa afya ya Watanzania.
Pongezi hizo alizitoa tarehe 24 Juni, 2025 alipofanya ziara ya kikazi kituoni hapo. Prof. Mdoe alitembelea kituo hicho kwa ajili ya kujitambulisha na kuona maendeleo ya tafiti, ugunduzi na uzalishaji wa tiba asili.
Akimkaribisha katika kituo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud alimpongeza Prof. James Mdoe kwa kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi na kumuahidi kumpa ushirikiano ili kufanikisha malengo ya Taasisi. Aliwasilisha taarifa ya kituo iliyoeleza mafanikio mbalimbali katika maeneo ya rasilimali watu, vitendea kazi, miundombinu ya majengo na maabara pamoja na maendeleo ya uzalishaji ya dawa za tiba asili. Akizungumza na watumishi wa kituo hicho, Mwenyekiti wa Baraza alielekeza Taasisi kuandaa mpango mkakati wa kutofautisha huduma na biashara, watafiti kuongeza machapisho ya tafiti, kusajili haki miliki, kuongeza ushirikiano na taasisi nyingine za tiba asili kama ITM na watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufanikisha malengo ya Taasisi.
Prof. Mdoe alisisitiza kuwa tiba asili ni hazina muhimu inayoweza kutoa suluhisho la changamoto nyingi za kiafya na akahimiza juhudi zaidi katika kukuza ubunifu na utafiti katika eneo hilo. Pia alishukuru kwa mapokezi mazuri na kuahidi kuendelea kushirikiana na Taasisi katika kuhakikisha kituo kinapiga hatua zaidi.

Section Title

Beyond Clinical Surveillance: Wastewater and Environmental Monitoring Reveal Hotspots of Antimicrobial-Resistant “Superbugs”

A recent study presented at the 7th Africa Continental World Antimicrobial Awareness Week (WAAW) event has unveiled the “environmental resistome” in Tanzania. Using advanced genomic tools to analyse...

NIMR Disseminates Impactful Research Findings at the 7th Africa Continental World AMR Awareness Week

In a milestone event for the continent, Tanzania hosted the 7th Africa Continental World Antimicrobial Resistance (AMR) Awareness Week (WAAW) at the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam from 2nd to...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi wa Afya Temeke Kuandika Andiko la Utafiti ili Kuboresha Huduma za Afya za Jamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya...

NIMR Conducts Institutional Review Boards Training to Elevate Clinical Trial Standards Nationwide

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched a specialized training program to members and secretariats of Institutional Review Boards (IRBs), aimed at strengthening national...

𝗡𝗜𝗠𝗥 Conducts Capacity Building Training for Clinical Trials Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR), in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), on 24th November 2025 conducted a specialized capacity-building...

NIMR na Wadau wa Afya Wafanya Mkutano wa Uzinduzi wa Utekelezaji wa Tafiti zilizo chini ya Mradi wa TAKeOFF wa Kupambana na Ugonjwa wa Mabusha na Matende

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa...

New Hope for Malaria Treatment: Tanzanian Scientists Lead Groundbreaking Clinical Trial

The National Institute for Medical Research (NIMR) Tanga Medical Research Centre, led by Principal Investigator Dr. Samwel Gesase as the country Coordinator, has been instrumental in the...

NIMR Yazidi Kung`ara Kimataifa

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kung’ara kimataifa iliposhiriki katika kongamano la kisayansi la American Society of Tropical Medicine and Hygiene (ASTMH) kwa...

NIMR Leads Global Effort to Combat Arboviral Diseases Using One Health Approach

In demonstration of leadership in global health research, the National Institute for Medical Research (NIMR) conducted a five-day Arboviral Workshop at NIMR Mbeya Medical Research Centre under the...