NIMR

Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James Mdoe, leo tarehe 25 Julai 2025 amefanya ziara ya kikazi katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Muhimbili, akiambatana na Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud.
Katika ziara hiyo, Prof. Mdoe ametembelea Maabara Kuu ya Kifua Kikuu, ambayo inaendeshwa kwa ushirikiano kati ya Kituo cha NIMR Muhimbili na Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma wa Wizara ya Afya. Maabara hiyo ni miongoni mwa nguzo muhimu katika mapambano dhidi ya kifua kikuu nchini na kanda ya Afrika. Alisisitiza kuwa mwelekeo wa uongozi wake ni kuona NIMR inazidi kung’ara kitaifa na kimataifa kupitia tafiti za afya zenye athari chanya kwa jamii.
Baada ya kutembelea maabara, Prof. Mdoe alipata nafasi ya kuzungumza na watumishi wa kituo hicho ambapo aliwatia moyo kuongeza tija na ubunifu katika kazi zao za utafiti, akisisitiza umuhimu wa kufikia malengo ambayo Taasisi imejiwekea. Aliahidi kushirikiana kwa karibu na menejimenti ya Taasisi katika kuhakikisha changamoto zilizopo zinatatuliwa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR Prof. Said Aboud alimpongeza Prof. Mdoe kwa kuteuliwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Baraza la NIMR.
Aidha aliwapongeza watumishi wa Kituo cha NIMR Muhimbili kwa mchango wao mkubwa katika kushiriki kutengeneza sera na miongozi ya tiba ya kifua kikuu na UKIMWI kitaifa na kimataifa kutokana na matokeo ya tafiti. Hata hivyo, aliwasihi kuongeza juhudi katika kuchapisha matokeo ya tafiti na kuandaa vijarida sera ili kuongeza ushahidi wa kisayansi kutoka katika kazi za utafiti wanazofanya. “Katika mwaka wa fedha 2024/25, tumefanikiwa kuchapisha machapisho 46 ya tafiti za afya katika majarida ya kitaifa, kikanda na kimataifa na vijarida sera 12 kutoka katika kituo cha NIMR Muhimbili. Hili ni jambo la kujivunia lakini bado tuna nafasi ya kufanya vizuri zaidi,” alisema Prof. Aboud.
Ziara hiyo imeonesha dhamira ya dhati ya uongozi wa juu wa NIMR katika kuimarisha usimamizi, kuongeza uwajibikaji na kuendeleza utafiti wa afya unaolenga kuboresha maisha ya Watanzania.

Section Title

Beyond Clinical Surveillance: Wastewater and Environmental Monitoring Reveal Hotspots of Antimicrobial-Resistant “Superbugs”

A recent study presented at the 7th Africa Continental World Antimicrobial Awareness Week (WAAW) event has unveiled the “environmental resistome” in Tanzania. Using advanced genomic tools to analyse...

NIMR Disseminates Impactful Research Findings at the 7th Africa Continental World AMR Awareness Week

In a milestone event for the continent, Tanzania hosted the 7th Africa Continental World Antimicrobial Resistance (AMR) Awareness Week (WAAW) at the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam from 2nd to...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi wa Afya Temeke Kuandika Andiko la Utafiti ili Kuboresha Huduma za Afya za Jamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya...

NIMR Conducts Institutional Review Boards Training to Elevate Clinical Trial Standards Nationwide

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched a specialized training program to members and secretariats of Institutional Review Boards (IRBs), aimed at strengthening national...

𝗡𝗜𝗠𝗥 Conducts Capacity Building Training for Clinical Trials Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR), in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), on 24th November 2025 conducted a specialized capacity-building...

NIMR na Wadau wa Afya Wafanya Mkutano wa Uzinduzi wa Utekelezaji wa Tafiti zilizo chini ya Mradi wa TAKeOFF wa Kupambana na Ugonjwa wa Mabusha na Matende

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa...

New Hope for Malaria Treatment: Tanzanian Scientists Lead Groundbreaking Clinical Trial

The National Institute for Medical Research (NIMR) Tanga Medical Research Centre, led by Principal Investigator Dr. Samwel Gesase as the country Coordinator, has been instrumental in the...

NIMR Yazidi Kung`ara Kimataifa

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kung’ara kimataifa iliposhiriki katika kongamano la kisayansi la American Society of Tropical Medicine and Hygiene (ASTMH) kwa...

NIMR Leads Global Effort to Combat Arboviral Diseases Using One Health Approach

In demonstration of leadership in global health research, the National Institute for Medical Research (NIMR) conducted a five-day Arboviral Workshop at NIMR Mbeya Medical Research Centre under the...