NIMR

Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Prof. James Mdoe, leo tarehe 25 Julai 2025 amefanya ziara ya kikazi katika Kituo cha Utafiti cha NIMR Muhimbili, akiambatana na Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Prof. Said Aboud.
Katika ziara hiyo, Prof. Mdoe ametembelea Maabara Kuu ya Kifua Kikuu, ambayo inaendeshwa kwa ushirikiano kati ya Kituo cha NIMR Muhimbili na Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma wa Wizara ya Afya. Maabara hiyo ni miongoni mwa nguzo muhimu katika mapambano dhidi ya kifua kikuu nchini na kanda ya Afrika. Alisisitiza kuwa mwelekeo wa uongozi wake ni kuona NIMR inazidi kungโ€™ara kitaifa na kimataifa kupitia tafiti za afya zenye athari chanya kwa jamii.
Baada ya kutembelea maabara, Prof. Mdoe alipata nafasi ya kuzungumza na watumishi wa kituo hicho ambapo aliwatia moyo kuongeza tija na ubunifu katika kazi zao za utafiti, akisisitiza umuhimu wa kufikia malengo ambayo Taasisi imejiwekea. Aliahidi kushirikiana kwa karibu na menejimenti ya Taasisi katika kuhakikisha changamoto zilizopo zinatatuliwa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR Prof. Said Aboud alimpongeza Prof. Mdoe kwa kuteuliwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Baraza la NIMR.
Aidha aliwapongeza watumishi wa Kituo cha NIMR Muhimbili kwa mchango wao mkubwa katika kushiriki kutengeneza sera na miongozi ya tiba ya kifua kikuu na UKIMWI kitaifa na kimataifa kutokana na matokeo ya tafiti. Hata hivyo, aliwasihi kuongeza juhudi katika kuchapisha matokeo ya tafiti na kuandaa vijarida sera ili kuongeza ushahidi wa kisayansi kutoka katika kazi za utafiti wanazofanya. โ€œKatika mwaka wa fedha 2024/25, tumefanikiwa kuchapisha machapisho 46 ya tafiti za afya katika majarida ya kitaifa, kikanda na kimataifa na vijarida sera 12 kutoka katika kituo cha NIMR Muhimbili. Hili ni jambo la kujivunia lakini bado tuna nafasi ya kufanya vizuri zaidi,โ€ alisema Prof. Aboud.
Ziara hiyo imeonesha dhamira ya dhati ya uongozi wa juu wa NIMR katika kuimarisha usimamizi, kuongeza uwajibikaji na kuendeleza utafiti wa afya unaolenga kuboresha maisha ya Watanzania.

Section Title

NIMR Yapongezwa kwa Mchango Mkubwa Katika Kukuza Tiba Asili

Wananchi wanaendelea kunufaika na huduma za tiba asili kupitia tafiti, na uanzishwaji wa kiwanda cha kuzalisha dawa za tiba asili cha NIMR Mabibo kufuatia juhudi kubwa za Serikali kuhakikisha dawa...

Tiba Asili Yazidi Kungโ€™ara: Tafiti Zaidi Zahitajika

Imeelezwa kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuendeleza tafiti za tiba asili na kuwekeza zaidi katika viwanda vya kuzalisha dawa za tiba hizo nchini, ili kuongeza tija katika kuboresha huduma za afya kwa...

Tanzania to Learn on Traditional Medicine Sector from South Korea

The Ministry of Health and the National Institute for Medical Research (NIMR) together with partner institutions embarked on a study visit to the National Institute for Korean Medicine Development...

Ministry of Health, NIMR Visits South Korea to Strengthen Innovation and Product Development in Traditional Medicine

๐— ๐—ถ๐—ป๐—ถ๐˜€๐˜๐—ฟ๐˜† ๐—ผ๐—ณ ๐—›๐—ฒ๐—ฎ๐—น๐˜๐—ต, ๐—ก๐—œ๐— ๐—ฅ ๐—ฉ๐—ถ๐˜€๐—ถ๐˜ ๐—ฆ๐—ผ๐˜‚๐˜๐—ต ๐—ž๐—ผ๐—ฟ๐—ฒ๐—ฎ ๐˜๐—ผ ๐—ฆ๐˜๐—ฟ๐—ฒ๐—ป๐—ด๐˜๐—ต๐—ฒ๐—ป ๐—œ๐—ป๐—ป๐—ผ๐˜ƒ๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป ๐—ฎ๐—ป๐—ฑ ๐—ฃ๐—ฟ๐—ผ๐—ฑ๐˜‚๐—ฐ๐˜ ๐——๐—ฒ๐˜ƒ๐—ฒ๐—น๐—ผ๐—ฝ๐—บ๐—ฒ๐—ป๐˜ ๐—ถ๐—ป ๐—ง๐—ฟ๐—ฎ๐—ฑ๐—ถ๐˜๐—ถ๐—ผ๐—ป๐—ฎ๐—น ๐— ๐—ฒ๐—ฑ๐—ถ๐—ฐ๐—ถ๐—ป๐—ฒ The Director General of the National Institute for Medical Research (NIMR), Prof...

NIMR, Wizara ya Afya Watoa Mafunzo kwa Wataalamu wa Afya Kutumia Teknolojia ya Uchambuzi na Ufuatiliaji wa Vinasaba vya Magonjwa ya Mlipuko

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa Kushirikiana na Wizara ya Afya, tarehe 18/08/2025 imeanza mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa maabara na watafiti kutoka taasisi...

Heri ya Siku ya Wakulima “Nanenane”

Section Title Heri ya Siku ya Wakulima “Nanenane” ByErick Mboma August 8, 2025 Uncategorized The National Institute for Medical Research (NIMR), in partnership with the University of Oslo...

NIMR Hosts Pandemic Ethics Project General Assembly, Welcomes Experts from Six Countries

The National Institute for Medical Research (NIMR), in partnership with the University of Oslo, hosted a high-level Pandemic Ethics General Assembly today 30th July 2025, at its Sub Office in Dar es...

NIMR Management Trained on Corporate Entrepreneurship

In a strategic move to enhance institutional sustainability and increase revenue collections, the National Institute for Medical Research (NIMR) has conducted a high-level training on corporate...

NIMR Highlights Digital Health Solutions for HIV-Exposed Infants at National Child Health Congress

The National Institute for Medical Research (NIMR) played a pivotal role in the 2nd Tanzania Child Health and Welfare Congress, held from 23rd โ€“ 25th July 2025 in Arusha, by spotlighting cutting-edge...