NIMR

Wananchi wanaendelea kunufaika na huduma za tiba asili kupitia tafiti, na uanzishwaji wa kiwanda cha kuzalisha dawa za tiba asili cha NIMR Mabibo kufuatia juhudi kubwa za Serikali kuhakikisha dawa salama na zenye ubora zinapatikana kwa wingi nchini.
Akizungumza tarehe 29 Agosti, 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Tiba Asili ya Mwafrika yaliyofanyika jijini Dodoma, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu, ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, aliipongeza Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa hatua kubwa zilizopigwa katika tafiti na uhamasishaji wa matumizi ya dawa za tiba asili.
Dkt. Kazungu alisema moja ya mafanikio makubwa ya NIMR ni uanzishwaji wa kiwanda cha Mabibo cha kuzalisha dawa za tiba asili ambacho kinatumia malighafi kutoka kwa wakulima wa miti dawa. “Kiwanda hiki hakijaishia tu kuzalisha dawa salama na zenye ufanisi na ubora, bali pia kimetoa fursa za ajira kwa wananchi na kuongeza kipato kwa wakulima wa malighafi hizo,” alisisitiza Dkt Kazungu.
Aidha, alitembelea banda la NIMR katika maonesho na kupongeza jitihada zilizofanywa huku akishauri kuimarisha tafiti zinazohusu tiba asili kwa magonjwa ya figo ambayo yanaongezeka kwa kasi katika siku za hivi karibuni.
Akitoa maelezo katika banda la NIMR Meneja wa kituo cha NIMR Mabibo Dkt. Emmanuel Peter alibainisha mchango wa NIMR katika kukuza tiba asili nchini kuwa ni pamoja na kufanya tafiti za tiba asili, kushiriki katika huduma jumuishi, kujenga kiwanda cha kuzalisha dawa za tiba asili, kuhamasisha tafiti, ugunduzi na matumizi ya dawa za tiba asili, kuimarisha ushirikiano na wadau wa tiba asili
Dkt. Peter alisema Kwa sasa, wananchi wanapata huduma jumuishi za tiba asili katika hospitali za rufaa za mikoa 14 ambapo mteja anaweza kuchagua tiba ya kisasa, tiba asili au kutumia zote kwa pamoja. “Huduma hii inamuwezesha mteja kufanyiwa vipimo vya kitaalamu na kupewa ushauri sahihi kuhusu tiba inayomfaa.
Maadhimisho hayo, yenye kaulimbiu “Tuimarishe Huduma za Tiba Asili Zenye Ushahidi wa Kisayansi,” yalianza tarehe 25 Agosti 2025 na yanatarajiwa kutamatika tarehe 31 Agosti 2025. Tukio hili limewakutanisha wataalamu wa tiba asili na tiba mbadala kutoka maeneo mbalimbali nchini, kwa lengo la kubadilishana uzoefu, na kuhamasisha matumizi ya dawa za tiba asili kwa manufaa ya jamii.

Section Title

NIMR Yaongoza Mdahalo wa Sera Kuhakikisha Ushahidi wa Kisayansi Unatumika Kukabili Milipuko ya Magonjwa

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) leo, tarehe 8 Januari 2026, imeendesha mkutano wa majadiliano ya sera uliowakutanisha watafiti, watunga sera, watoa maamuzi wa sekta ya afya...

NIMR Unveils Genomic Evidence Showing Predominance of Bacterial Pathogens in Acute Respiratory Infections in Tanzania

The National Institute for Medical Research (NIMR) disseminated on 22nd December 2025 research findings from the project titled Genomic characterization of Acute Respiratory Infections (ARI) Pathogens...

Beyond Clinical Surveillance: Wastewater and Environmental Monitoring Reveal Hotspots of Antimicrobial-Resistant “Superbugs”

A recent study presented at the 7th Africa Continental World Antimicrobial Awareness Week (WAAW) event has unveiled the “environmental resistome” in Tanzania. Using advanced genomic tools to analyse...

NIMR Disseminates Impactful Research Findings at the 7th Africa Continental World AMR Awareness Week

In a milestone event for the continent, Tanzania hosted the 7th Africa Continental World Antimicrobial Resistance (AMR) Awareness Week (WAAW) at the Hyatt Regency Hotel in Dar es Salaam from 2nd to...

NIMR Yawajengea Uwezo Watumishi wa Afya Temeke Kuandika Andiko la Utafiti ili Kuboresha Huduma za Afya za Jamii

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo chake cha Muhimbili, imeendesha mafunzo maalumu ya uandishi wa andiko la kitafiti kwa watumishi wa afya kutoka Hospitali ya...

NIMR Conducts Institutional Review Boards Training to Elevate Clinical Trial Standards Nationwide

The National Institute for Medical Research (NIMR) has launched a specialized training program to members and secretariats of Institutional Review Boards (IRBs), aimed at strengthening national...

𝗡𝗜𝗠𝗥 Conducts Capacity Building Training for Clinical Trials Researchers

The National Institute for Medical Research (NIMR), in collaboration with the Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA), on 24th November 2025 conducted a specialized capacity-building...

NIMR na Wadau wa Afya Wafanya Mkutano wa Uzinduzi wa Utekelezaji wa Tafiti zilizo chini ya Mradi wa TAKeOFF wa Kupambana na Ugonjwa wa Mabusha na Matende

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Mradi wa TAKeOFF awamu ya pili tarehe 20/11/2025 imefanya mkutano wa pamoja na kamati za afya za Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa...

New Hope for Malaria Treatment: Tanzanian Scientists Lead Groundbreaking Clinical Trial

The National Institute for Medical Research (NIMR) Tanga Medical Research Centre, led by Principal Investigator Dr. Samwel Gesase as the country Coordinator, has been instrumental in the...