NIMR

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kupitia Kituo cha Muhimbili, imewajengea uwezo watumishi wa afya 18 wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana (Amana RRH) katika uandishi wa maandiko ya utafiti (Proposal Development), hatua inayolenga kuboresha huduma za afya kwa jamii kupitia tafiti zenye ubora na ushahidi wa kisayansi.

Mafunzo hayo ya siku nne yalifanyika kuanzia tarehe 26 hadi 29 Januari 2026 katika hospitali hiyo yakilenga kuwawezesha watoa huduma wa afya kubuni, kuandaa na kuwasilisha mapendekezo bora ya tafiti za kisayansi zinazoweza kupata ufadhili na kuleta matokeo chanya katika sekta ya afya.

Kupitia mafunzo hayo ya vitendo, washiriki walipata ujuzi wa kuandaa maandiko ya kisayansi yenye viwango, kuimarisha uwezo wa uandishi wa kitaaluma, kuelewa na kuzingatia maadili ya utafiti pamoja na kutumia takwimu sahihi katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili wananchi.

Akifungua mafunzo hayo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dkt. Bryceson Loti Kiweru, alisema utafiti ni nyenzo muhimu isiyoweza kuepukika katika sekta ya afya.

“Swala zima la utafiti haliepukiki katika sekta ya afya na inahitajika ushirikiano na taasisi zinazofanya utafiti ili kuboresha huduma za afya nchini,” alisema Dkt. Kiweru.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Idara ya Tafiti kutoka kituo cha NIMR Muhimbili, Dkt. Ester Mbutolwe, alisisitiza umuhimu wa matumizi sahihi ya takwimu katika kuibua suluhisho la changamoto za afya.

“Kila mtu akijengewa uwezo vizuri anaweza kutoa mchango wake katika kuboresha afya za wananchi. Takwimu sahihi ni msingi wa utafiti wenye matokeo ya kuaminika. Ushirikiano kati ya NIMR na hospitali za rufaa za mkoa ni muhimu,” alisisitiza Dkt. Mbutolwe.

Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za NIMR za kuimarisha tafiti za afya nchini kwa kuwajengea uwezo wataalamu walioko kwenye vituo vya kutolea huduma, ili tafiti zinazofanyika ziweze kutoa majibu ya changamoto halisi za jamii na kuboresha ubora wa huduma za afya nchini.

Section Title

NIMR Scientists Ranked Among Tanzania Top 50 by the AD Scientific Index 2026

The National Institute for Medical Research (NIMR) has once again demonstrated its leadership in scientific research with five of its distinguished scientists ranked among the Top 50 scientists in...

Decade-Long Research Led by NIMR Shapes Africa’s Push for Integrated HIV and NCD Care

New evidence from a decade of research led by Tanzania’s National Institute for Medical Research (NIMR) on integrated HIV and non-communicable disease (NCD) care is driving renewed efforts across...

Watumishi NIMR Wapatiwa Mafunzo ya Maadili ya Utumishi wa Umma, Rushwa Mahali pa Kazi na Afya ya Akili

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kujenga watumishi wenye weledi, uadilifu, uwajibikaji na afya njema kwa kuendesha mafunzo maalumu...

NIMR Researchers Shine with DZIF Early Career Scientists Grant

Researchers from the National Institute for Medical Research (NIMR), Mbeya Centre, have earned international recognition after five early career scientists were awarded the prestigious Deutsches...

NIMR Yasisitiza Tafiti Zinazotatua Changamoto za Afya Katika Maandalizi ya Bajeti ya 2026/2027

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said Aboud, ameitaka taasisi hiyo kuimarisha uwezo wake wa kifedha na kuwekeza katika tafiti zinazolenga kutatua...

Mkurugenzi Mkuu NIMR Aridhishwa na Maendeleo ya Utafiti na Huduma Kituo Kidogo cha Gonja.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Said S. Aboud, ameridhishwa na maendeleo ya shughuli za utafiti na utoaji wa huduma za maabara yanayoendelea...

Wanawake wa NIMR Mbeya Waadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake kwa Matendo ya Huruma na Elimu ya Uwiano wa Majukumu ya Kazi na Familia.

Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, tarehe 08 Machi, wanawake wa Taasisi ya Taifa ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Kituo cha Mbeya walionyesha mshikamano na kujitolea kwa jamii...

Wanawake wa NIMR Waadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa Kuwasaidia Watoto Yatima.

Katika kusheherekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, wanawake wa Kituo cha Utafiti cha NIMR Tanga wameadhimisha siku hiyo kwa kutembelea Kituo cha Watoto Yatima cha FURAHA, kilichopo Raskazone...

NIMR Yatoa Matokeo ya Utafiti Kuonyesha Mwelekeo Mpya wa Kujenga Ustahimilivu Dhidi ya Magonjwa ya Mlipuko Yanayosababishwa na Wadudu Dhurifu

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), tarehe 26 Februari 2026, kupitia mradi wa RAFT (Resilience Against Future Threats through Vector Control), imewasilisha matokeo ya utafiti...

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Ut elit tellus, luctus nec ullamcorper mattis, pulvinar dapibus leo.